Thursday, 24 August 2017

Ndugu wasusia mwili wa jamaa yao aliyefariki kwa utata

Ndugu wa marehemu Shinje Charles mwenye umri wa miaka 25, mkazi wa mtaa wa Uwanja, kata ya Nyankumbu mjini Geita, wamesusia kuchukua mwili wa ndugu yao, kutokana na utata wa kifo chake mpaka uchunguzi utakapokamilika.                        Inadaiwa marehemu Charles amefariki dunia kufuatia kipigo alichopokea kutoka kwa walinzi wa mgodi...

Monday, 21 August 2017

JPM amteua brigedia kuwa naibu mkurugenzi TAKUKURU

Rais John Magufuli leo Agosti 21, amemteua brigedia jenerali John Julius Mbungo, kuwa naibu mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU). Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mkurugenzi wa mawasiliano ya rais Ikulu, Gerson Msigwa, uteuzi wa brigedia Mbungo, umeanza leo. Taasisi ya Kuzuia na Kupamabana na Rushwa (TAKUKURU) ni ya umma, iliyoanzishwa chini ya Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Namba 11 ya Mwaka 2007. Sheria...

Sunday, 6 August 2017

TCAA YAKANA KUITAMBUA NDEGE YA GWAJIMA

Serikali kupitia Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) imekana kuwa na taarifa ya ndege iliyonunuliwa na Askofu wa Kanisa Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima nchini Marekani. Juzi, Askofu Gwajima alithibitisha kununua ndege hiyo aina ya GulfStream N60983 yenye thamani ya Sh2.64 bilioni kwa ajili ya kuitumia kusambaza injili. Ili kuonyesha msisitizo, Askofu Gwajima aliweka picha kwenye mitandao ya kijamii iliyomwonyesha mbele ya ndege hiyo. Kiongozi huyo...

Wednesday, 2 August 2017

Urusi: Marekani imetangaza ''vita vya kibiashara'' kwetu

Waziri mkuu wa Urusi Dmitry Medvedev amesema kuwa vikwazo vipya vilivyowekwa na Marekani dhidi ya taifa hilo ni sawa na kutangaza vita vya kibiashara. Amesema kuwa mikakati iliotiwa saini na rais Trump inaonyesha udhaifu wa rais huyo wa Marekani ambaye alisema ameaibishwa na bunge la Congress. Sheria hiyo inalenga kuiadhibu Urusi kwa kuingilia uchaguzi wa Marekani wa 2016 pamoja na vitendo vyake dhidi ya Ukraine. Katika kutia saini makubaliano hayo...

Marekani yakana kutaka kuing’oa Korea Kaskazini

Serikali ya Marekani kupitia waziri wa maswala ya kigeni Rex Tillerson, imesema haina dhamira ya kuing’oa madarakani utawala wa Korea Kaskazini, wakati huu ambao kumekuwa na hali ya wasiwasi juu ya mpango wa silaha za nyuklia wa Pyongyang.  “Sisi siyo maadui” alisema Tillerson na kuongeza kuwa Marekani ilihitaji majadiliano kwa kiasi fulani. Pamoja na kauli ya waziri huyo, seneta mmoja mwandamizi wa Chama cha Republican amesema rais Trump amelipa...

Watoto walioungana kutengenishwa baada ya miezi sita

Daktari Bingwa Hospitali ya Taifa Muhimbili aliyebobea katika fani ya upasuaji wa watoto Afrika Mashariki, Zaituni Bokhari amesema baada ya kufanya vipimo, imegundulika kuna uwezekano wa kuwatenganisha watoto mapacha waliozaliwa wakiwa wameungana. Dk Bokhari ameyasema hayo leo Jumatano alipokuwa akitoa majibu ya vipimo vilivyochukuliwa hospitalini hapo kwa takriban wiki nzima. “Vipimo vya damu vimeonyesha kila mtoto ana mfumo wake na hawana maambukizi...