Monday, 21 August 2017

JPM amteua brigedia kuwa naibu mkurugenzi TAKUKURU

Rais John Magufuli leo Agosti 21, amemteua brigedia jenerali John Julius Mbungo, kuwa naibu mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mkurugenzi wa mawasiliano ya rais Ikulu, Gerson Msigwa, uteuzi wa brigedia Mbungo, umeanza leo.

Taasisi ya Kuzuia na Kupamabana na Rushwa (TAKUKURU) ni ya umma, iliyoanzishwa chini ya Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Namba 11 ya Mwaka 2007.

Sheria hiyo ilitungwa baada ya kufutwa kwa Sheria ya Kuzuia Rushwa (TAKURU) sura ya 329, iliyofanyiwa marejeo mwaka 2002.

Kuanzishwa kwa chombo hicho kulikuja baada ya Bunge la Tanzania, kupitisha muswada wa sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa wa mwaka 2007 mnamo Aprili 6.

Muswada huo ulisainiwa na rais wa awamu ya nne Jakaya Kikwete, na kuwa sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa mnamo Juni 11, 2007 na ilianza kufanya kazi Julai mwaka huo.

Related Posts:

  • Simba wapata mualiko bungeni kesho Jumatatu Dodoma. Siku moja baada ya klabu ya Simba kutwaa ubingwa wa Kombe la Shirikisho, imepata mwaliko bungeni.Simba iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Mbao FC ya jijini Mwanza, bao lililopatikana ndani ya dakika ngumu 120… Read More
  • Askofu Gwajima afunguka juu ya sakata la madini Dar es Salaam, Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amesema ni muhimu madini yasichimbwe hadi itakapowekwa mashine za kuchenjua makinikia.                   &nbs… Read More
  • Mgeja akasirishwa na kauli ya Polepole Morogoro. Mwenyekiti wa Tanzania Mzalendo Foundation, Khamis Mgeja amemuonya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Hampyrey Polepole aache mara moja kugeuza matukio ya kuuawa Watanzania katika Wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani… Read More
  • Askofu Gwajima: nitawavua mataulo wanaonichokoza Dar es Salaam. Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amewatahadharisha wanaomchokoza akisema ni sawa na mtu anayeanzisha ugomvi huku akiwa amevaa taulo.Akihubiri leo, Gwajima amesema wakiendelea atawavu… Read More
  • Mkapa na Kikwete watajwa ishu ya mchanga Mwenyekiti  wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amesema marais wastaafu, Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete, wanahusika na sakata la mchanga wa madini (makinikia) unaosafirishwa nje ya nchi. … Read More

0 comments:

Post a Comment