Monday 21 August 2017

JPM amteua brigedia kuwa naibu mkurugenzi TAKUKURU

Rais John Magufuli leo Agosti 21, amemteua brigedia jenerali John Julius Mbungo, kuwa naibu mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mkurugenzi wa mawasiliano ya rais Ikulu, Gerson Msigwa, uteuzi wa brigedia Mbungo, umeanza leo.

Taasisi ya Kuzuia na Kupamabana na Rushwa (TAKUKURU) ni ya umma, iliyoanzishwa chini ya Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Namba 11 ya Mwaka 2007.

Sheria hiyo ilitungwa baada ya kufutwa kwa Sheria ya Kuzuia Rushwa (TAKURU) sura ya 329, iliyofanyiwa marejeo mwaka 2002.

Kuanzishwa kwa chombo hicho kulikuja baada ya Bunge la Tanzania, kupitisha muswada wa sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa wa mwaka 2007 mnamo Aprili 6.

Muswada huo ulisainiwa na rais wa awamu ya nne Jakaya Kikwete, na kuwa sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa mnamo Juni 11, 2007 na ilianza kufanya kazi Julai mwaka huo.

0 comments:

Post a Comment