Wednesday, 2 August 2017

Watoto walioungana kutengenishwa baada ya miezi sita

Daktari Bingwa Hospitali ya Taifa Muhimbili aliyebobea katika fani ya upasuaji wa watoto Afrika Mashariki, Zaituni Bokhari amesema baada ya kufanya vipimo, imegundulika kuna uwezekano wa kuwatenganisha watoto mapacha waliozaliwa wakiwa wameungana.

Dk Bokhari ameyasema hayo leo Jumatano alipokuwa akitoa majibu ya vipimo vilivyochukuliwa hospitalini hapo kwa takriban wiki nzima.

“Vipimo vya damu vimeonyesha kila mtoto ana mfumo wake na hawana maambukizi ya aina yoyote, ugumu unakuja kwenye ini na moyo ambapo wanategemeana ila uwezekano wa kutenganishwa upo,” amesema Dk Bokhari.

Majibu hayo yamekuja siku chache baada ya pacha hao kupimwa vipimo vya radiolojia ikiwemo CT Scan, MRI, X Ray kipimo cha moyo (ECO) pamoja na vipimo vyote vya damu.

Watoto hao waliozaliwa katika hospitali ya Misheni ya Berega iliyopo Kanda ya Mashariki mkoani Morogoro, Julai 21 mwaka huu wamenaza kuchukuliwa vipimo mbalimbali vya awali.

Related Posts:

  • Askofu Gwajima afunguka juu ya sakata la madini Dar es Salaam, Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amesema ni muhimu madini yasichimbwe hadi itakapowekwa mashine za kuchenjua makinikia.                   &nbs… Read More
  • Mgeja akasirishwa na kauli ya Polepole Morogoro. Mwenyekiti wa Tanzania Mzalendo Foundation, Khamis Mgeja amemuonya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Hampyrey Polepole aache mara moja kugeuza matukio ya kuuawa Watanzania katika Wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani… Read More
  • Askofu Gwajima: nitawavua mataulo wanaonichokoza Dar es Salaam. Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amewatahadharisha wanaomchokoza akisema ni sawa na mtu anayeanzisha ugomvi huku akiwa amevaa taulo.Akihubiri leo, Gwajima amesema wakiendelea atawavu… Read More
  • Mkapa na Kikwete watajwa ishu ya mchanga Mwenyekiti  wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amesema marais wastaafu, Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete, wanahusika na sakata la mchanga wa madini (makinikia) unaosafirishwa nje ya nchi. … Read More
  • Simba wapata mualiko bungeni kesho Jumatatu Dodoma. Siku moja baada ya klabu ya Simba kutwaa ubingwa wa Kombe la Shirikisho, imepata mwaliko bungeni.Simba iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Mbao FC ya jijini Mwanza, bao lililopatikana ndani ya dakika ngumu 120… Read More

0 comments:

Post a Comment