Wednesday 2 August 2017

Watoto walioungana kutengenishwa baada ya miezi sita

Daktari Bingwa Hospitali ya Taifa Muhimbili aliyebobea katika fani ya upasuaji wa watoto Afrika Mashariki, Zaituni Bokhari amesema baada ya kufanya vipimo, imegundulika kuna uwezekano wa kuwatenganisha watoto mapacha waliozaliwa wakiwa wameungana.

Dk Bokhari ameyasema hayo leo Jumatano alipokuwa akitoa majibu ya vipimo vilivyochukuliwa hospitalini hapo kwa takriban wiki nzima.

“Vipimo vya damu vimeonyesha kila mtoto ana mfumo wake na hawana maambukizi ya aina yoyote, ugumu unakuja kwenye ini na moyo ambapo wanategemeana ila uwezekano wa kutenganishwa upo,” amesema Dk Bokhari.

Majibu hayo yamekuja siku chache baada ya pacha hao kupimwa vipimo vya radiolojia ikiwemo CT Scan, MRI, X Ray kipimo cha moyo (ECO) pamoja na vipimo vyote vya damu.

Watoto hao waliozaliwa katika hospitali ya Misheni ya Berega iliyopo Kanda ya Mashariki mkoani Morogoro, Julai 21 mwaka huu wamenaza kuchukuliwa vipimo mbalimbali vya awali.

0 comments:

Post a Comment