Monday 31 July 2017

Aliyeanzisha kampeni ya 'Magufuli Baki' akimbilia TCRA

Mmalaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeombwa kufuatilia kwa makini  mawasiliano ya simu za mkononi ili kubaini watu wanaotumia mitandao hiyo  kinyume na sheria.

Ombi hilo limetolewa na mwanaharakati Lawrence Mabawa  jijini Dar es salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari vitisho anavyopata kupitia simu ya mkoni baada ya kutambulisha kampeni yake ya ‘BAKI MAGUFULI’.

Kwa mujibu wa Mabawa, baadhi ya wananchi wameelewa vibaya kampeni hiyo na kufikia hatua ya kutoa maneno ya matusi na kejeli kwake.

Akifafanua lengo la kampeni yake, Mabawa amesema alimaanisha  kuwa Rais abaki na msimamo wake ambao kwa kiasi kikubwa unapeleka taifa la Tanzania mbele kimaendeleo, na si kama ambavyo watu hao wameichukulia.

0 comments:

Post a Comment