Thursday 27 July 2017

Wanawake watano wafariki kwa kuchomwa moto Tabora

Watu watano wamefariki dunia kwa kuchomwa moto na watu wanaosaidikiwa kuwa ni sungusungu katika kata ya Uchama wilayani Nzega mkoani Tabora.

 

Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri, amezitaka Kamati za Ulinzi na usalama ngazi ya mkoa na ile ya Wilaya ya Nzega kusitisha shughuli zote zilizokuwa zikifanywa na sungusungu katika kijiji hicho.

Mwanri amesema kuwa amechukua hatua hiyo baada ya sungusungu hao kutekeleza mauaji hayo ya watu watano ambao wote ni wanawake wakituhumiwa kuwa ni washirikina.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Wilbroad Mutafungwa amesema kuwa katika kuendelea kuchunguza tukio hilo jeshi hilo linawashikilia baadhi ya viongozi wa kijiji hicho ili kuweza kubaini waliotekeleza tukio hilo.

 

0 comments:

Post a Comment