Wednesday, 2 August 2017

Marekani yakana kutaka kuing’oa Korea Kaskazini

Serikali ya Marekani kupitia waziri wa maswala ya kigeni Rex Tillerson, imesema haina dhamira ya kuing’oa madarakani utawala wa Korea Kaskazini, wakati huu ambao kumekuwa na hali ya wasiwasi juu ya mpango wa silaha za nyuklia wa Pyongyang.

 “Sisi siyo maadui” alisema Tillerson na kuongeza kuwa Marekani ilihitaji majadiliano kwa kiasi fulani.

Pamoja na kauli ya waziri huyo, seneta mmoja mwandamizi wa Chama cha Republican amesema rais Trump amelipa uzito suala la kuingia kwenye vita na taifa hilo la Korea Kaskazini, akiamini kuwa hilo ndilo chaguo sahihi.

Yenyewe Korea Kaskazini inadai kuwa jaribio lake la hivi karibuni la kombora la masafa marefu, linaweza kupiga pwani ya Magharibi ya Marekani na sehemu nyingine.

“Hatutafuti mabadiliko ya madaraka, hatutafuti anguko la utawala, sisi siyo maadui zenu, sisi siyo tishio kwenu, lakini mnawasilisha tishio lisilokubalika kwetu na tunapaswa kujibu,” alisema Tillerson akiiambia Korea Kaskazini.

Related Posts:

  • Polisi 4 wauawa katika mlipuko Garissa KenyaHaki miliki ya pichaEPAImage captionMaafisa wa usalama katika shambulio la 2015 ambapo watu 147 waliuawa katika shambulio la al Shabaab dhidi ya chuo kikuu cha Garissa Kenya Maafisa 4 wa polisi wameuawa na wengine 4 kujeruhiw… Read More
  • Muungano wa wafanyakazi wampiga marufuku rais ZumaImage captionMuungano wa wafanyikazi nchini Afrika Kusini Cosatu Baraza la Muungano wa wafanyikazi nchini Afrika Kusini Cosatu ambalo ni mshirika mkuu wa chama tawala cha ANC limempiga marufuku rais Jacob Zuma kuhutubia katik… Read More
  • Alberto Msando ajiuzulu Ushauri wa chama cha Act-Wazalendo Mkuu wa Chama Cha Act-Wazalendo Zitto Kabwe amethibitisha kupokea barua ya kujiuzulu kwa mshauri mteule wa Chama hicho Albarto Msando."Nimepokea barua ya Wakili Albert G. Msando kuomba kujiuzulu nafasi yake ya Ushauri wa Ch… Read More
  • Manji amethibitisha tena kujiuzulu Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga, Yusuf Manji amethibitisha kuachia ngazi katika nafasi ya Uenyekiti wa klabu hiyo, uamuzi ambao aliuchukua tangu Mei 20, mwaka huu. Kutokana na uamuzi huo wa Manji sasa Yanga itakuwa chin… Read More
  • Je unawajua wakongwe waliozoea kufanya kazi duniani?Haki miliki ya pichaAFP/GETTY IMAGESImage captionMwanamfalme Philip anasema atajiuzulu baadaye mwaka huu Wakati Mwanamfalme Philip, anayeingia miaka 96 mwezi Juni anastaafu majukumu yake ya kifalme baadaye mwaka huu, tunawaan… Read More

0 comments:

Post a Comment