Wednesday 31 May 2017

Jeshi la Polisi Tanzania, latoa onyo

Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania Simon Sirro
Image captionMkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania Simon Sirro
Jeshi la Polisi nchini Tanzania limetoa onyo kwa wale wote wanaojihusisha na vitendo vya uhalifu na kusababisha mauaji ya raia na polisi.
Akizungumza kwa mara ya kwanza, mbele ya vyombo vya habari, baada ya kuteuliwa katika nafasi hiyo, siku chache zilizopita, Mkuu wa Jeshi la polisi Simon Sirro amesema changamoto iliyopo kwa sasa ni tatizo la mkoa wa Pwani ambako raia wema wamekuwa wakiuawa.
Katika kukabiliana na hali hiyo amesema wanaendelea na operesheni mbalimbali kuhakikisha kwamba vitendo hivyo haviendelei na wanaojihusisha na mauaji wakikamatwa hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.
''..Suala la Ikwiriri suala la Rufiji ni suala la muda mfupi...'' Alisema Sirro
Amesisitiza kuwa wahalifu ni kikundi cha watu wachache na kijue kuwa wao ni Watanzania, hivyo haoni sababu waendelee kuwafanyia wenzao ubaya.
Rais wa Tanzania John MagufuliHaki miliki ya pichaAFP
Image captionRais wa Tanzania John Magufuli
Katika hatua nyingine, Jeshi la Polisi Tanzania limetangaza kutoa takriban dola elfu 5, ama shilingi milioni 10, kwa yeyote atakayetoa taarifa zitakazofanikishwa kukamatwa kwa wahalifu wa mauaji ya wananchi na polisi mkoani Pwani.
Katika siku za hivi karibuni Tanzania imeshuhudia mauaji yanayofanywa na watu wasio julikana katika wilaya za Rufiji, Mkuranga na Kibiti mkoani Pwani, hali ambayo imeleta wasiwasi kwa raia.

source:bbc

Reli mpya ya kisasa SGR yazinduliwa Kenya

Reli mpya ya SGR yazinduliwa Kenya
Image captionReli mpya ya SGR yazinduliwa Kenya
Kenya imezindua reli mpya kati ya mji wa Mombasa hadi Nairobi ikiwa ni miezi 18 mapema.
Reli hiyo iliotengezwa kupitia ufadhili wa shilingi bilioni 3.2 kutoka serikali ya China ndio mradi mkubwa wa miundo msingi kuwahi kutekelezwa na serikali tangu taifa hilo lijipatie uhuru wake.
Mradi huo umechukua takriban miaka mitatu na nusu kwa kutumia teknolojia ya ujenzi wa reli ya China kukamilika.
Wanawake watakaoendesha treni za kisasa Kenya
Reli hiyo inatarajiwa kuunganisha Sudan Kusini, DR Congo ,Burundi na Mombasa.
Reli mpya ya SGR iliozinduliwa na rais wa Kenya Uhuru Kenyatta
Image captionReli mpya ya SGR iliozinduliwa na rais wa Kenya Uhuru Kenyatta
Ni reli ya kwanza katika kipindi cha karne moja.
Safari ya kutoka Mombasa kuelekea Nairobi na treni ya kisasa itachukua saa nne na nusu ikilinganishwa na saa tisa kwa kutumia basi na saa 12 kwa kutumia treni ya zamani.
Nauli ya watu watakaokalia viti vya kawaida ni shilingi 900 huku wale watakaosafiri kwa kutumia business class wakilipa shilingi 3,000.
Rais Uhuru Kenyatta alisema wakati wa uzinduzi wa reli hiyo ambayo imeanzishwa mwamko mpya katika historia ya Kenya.
Behewa la Ist Class ambalo Wakenya watakaosafiria watalipa shilingi 3000
Image captionBehewa la Ist Class ambalo Wakenya watakaosafiria watalipa shilingi 3000
''Historia ilianzwa miaka122 iliopita wakati Waingereza waliokuwa wametawala taifa hili walipoanzisha treni hiyo iliokuwa haijulikani inakokwenda na kupewa jina Lunatic Express
''Leo licha ya kukosolewa pakubwa tunasherehekea Madaraka Express {ikitajwa baada ya siku ambayo Wakenya walijipatia uhuru wao kikamilifu} badala ya Lunatic Express.
Gharama ya mradi huo imekosolewa na upinzani ambao unasema mradi huo umeigharimu Kenya fedha nyingi mno.
Vilevile wamemshutumu rais Kenyatta kwa kuomba fedha kutoka China bila mpango.
Serikali nayo inasema kuwa ni sharti iwekeze katika miundo msingi ili kuvutia wawekezaji.

source:bbc

Wanajeshi wakichoma moto kituo cha polisi Nigeria

Kituo cha polisi kilichochomwa moto NigeriaHaki miliki ya pichaNIGERIAN POLICE
Image captionKituo cha polisi kilichochomwa moto Nigeria
Ripoti kutoka nchini Nigeria zinasema Maafisa wa jeshi la Wanamaji wamevamia na kuchoma moto kituo cha polisi mjini Calabar kusini mwa nchi hiyo.
Maafisa wa polisi watatu wanaripotiwa kuuawa, ingawa bado haijafahamia vifo hivyo vimetokeaje.
Tukio hilo limetokea kufuatia mabishano yaliyotokea katika wanajeshi hao wa majini na maafisa wa polisi.
Ripoti zaidi zinasema maafisa hao wa jeshi la maji walirudi tena katika eneo hilo wakiwa wamejiimarisha zaidi na kuanza kushambulia kituo cha polisi, na baadaye kukichoma moto.

source:bbc

Simba yapania Kumsajili Aishi Manula na kumtema Agyei


SIMBA inataka kumuacha kipa Mghana, Daniel Agyei ili imsajili kipa wa Azam FC, Aishi Manula.
Na hiyo ni kufuatia habari za Aishi kutokubaliana na Azam kuongeza mkataba, baada ya kumalizika kwa mkataba wake wa sasa mwezi ujao.

Uongozi wa Simba SC unaamini ukimpata Aishi hautakuwa na sababu ya kuingia gharama za ziada kwa kuendelea kuwa na kipa wa kigeni, Agyei aliyejiunga na Wekundu hao wa Msimbazi Desemba mwaka jana kutoka Medeama SC ya Ghana.

Hata hivyo, wazo hilo linapingwa na baadhi ya viongozi wa Simba, wanaoamini Agyei ni bora zaidi ya Aishi na ndiye anayeIfaa klabu hIyo kwa sasa ikirejea kwenye michuano ya Afrika.

Simba ilikata tena tiketi ya kurudi kwenye michuano ya Afrika, baada ya kutwaa Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) kufuatia ushindi wa 2-1 dhidi ya Mbao FC ya Mwanza Uwanja wa Jamhuri Dodoma Jumamosi iliyopita.

Na kwa ushindi huo, Simba imekata tiketi ya kucheza michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika mwakani na pia itafungua msimu ujao kwa kumenyana na mahasimu, Yanga SC katika mechi ya Ngao ya Jamii. 

Simba ilicheza michuano ya Afrika kwa mara ya mwisho, mwaka 2013 na kutolewa na Recreativo de Lobolo ya Angola Raundi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa vipigo vya nyumbani na ugenini, ikifungwa 1-0 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na 4-0 ugenini.

Na Agyei ameidakia Simba jumla ya mechi 25 za mashindano yote, akifungwa mabao 10 huku mechi 16 akidaka bila kuruhusu nyavu zake kuguswa.

Alisajiliwa kuchukua nafasi ya kipa Muivory Coast, Vincent Angban ambaye naye pia aliachwa akiwa ana rekodi nzuri.

Kipa Mcameroon aomba Kibarua Yanga




KIPA Youthe Rostand amewaambia viongozi wa Yanga SC waache kumuogopa na wamuite mezani wazungumze kama kweli wana nia ya kumsajili.

Kumekuwa na tetesi za muda mrefu kwamba kipa huyo Mcameroon ambaye timu yake iliyomleta nchini, African Lyon imeteremka daraja kutoka Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara anatakiwa na Yanga SC.

Na akizungumzia na Bin Zubeiry Sports – Online leo mjini Dar es Salaam, Rostande amesema kwamba uwezekano way eye kubaki African Lyon ni mdogo kwa sababu ni vigumu kwake kuendelea kuchezea timu hiyo baada ya kushuka daraja.

Kwa sasa naangali uwezekano wa kupata timu ya Ligi Kuu, ili nijiunge nayo, lakini kubaki Lyon baada ya kushuka daraja ni ngumu,”amesemaa.

Hata hivyo, Rostande ameshangaa kusikia kwa muda mrefu kwamba  anatakiwa na mabingwa wa Ligti Kuu nchini, Yanga lakini wanasita kumuita kwa mazungumzo yoyote na yeye hivyo kama wana nia na huduma yake wafike mezani wazungumze.

"Sizani kama nitacheza ligi ya chini zaidi ya hapa, inabidi itambulike kuwa nimeshamaliza mkataba na timu hii hivyo ni rahisi kwangu mimi kupata timu nyingine ya ligi na nina imani nitazipata tu,"alisema.

"Mimi hakuna klabu ambayo imefika mezani kuzungumza na mimi masuala ya kimkataba hata hao Yanga hawajafika, kwa hiyo kama kuna timu inanihitaji basi wafike mezani tuzungumze tukikubaliana nitasaini lakini iwe ya ligi kuu,"alisema.

Africa Lyon inaweza kupoteza wachezaji wake wengi nyota baada ya kushuka daraja  na tayari klabu mbalimbali za Ligi Kuu zimeonyesha nia ya dhati ya kuwachukua wachezaji hodari wa timu hiyo.

SOURCE:MUUNGWANA

PICHA: Kwa mara ya kwanza Rayvanny amempost mtoto wake na Ujumbe mzito


 Mwimbaji staa wa Bongofleva kutoka WCB Rayvanny leo May 31, 2017 kupitia account yake ya Instagram kwa mara ya kwanza amepost picha ya mtoto wake Jaydan ikiwa ni kumtambulisha kwa mashabiki wake.
Rayvanny aliandika kwenye picha hiyo:>>>“Mungu Akukukuze Mwanangu, Katika Mema na Mafanikio Katika Maisha Yako.Wewe Nifuraha Yangu Na pia Wewe Ndio sababu Ya Mimi kumwaga Jasho Nakufanya Kazi kwa Bidii Kila Siku. Ni bora Nikose Vyote Lakini Sio Wewe Mwanangu. I LOVE YOU SON” – Rayvanny


SOURCE:MUUNGWANA

HATIMAYE:Niko tayari kuondoka Barcelona- Iniesta


Nohodha wa Barcelona, Andres Iniesta bado ana ndoto za kuzeekea kwenye Liga ya La Liga, huku akisema kwamba iwapo atatakiwa kuondoka yupo tayari kufanya hivyo.

Iniesta mwenye miaka 33 mkataba wake unamalizika katikati ya mwaka 2018 na hatima yake imebaki njiapanda. Msimu huu alianza mechi 13 za ligi msimu huu.

Kiungo huyo alisema bado ndoto zake ni kustaafu maisha ya soka akiwa kwenye klabu yake ya Barcelona ambayo alijiunga  tangu akiwa na miaka 12, akichezea timu ya vijana.

Imevujaa!! Kumbe John Bocco alikuwa anahitajika Azam

Golikipa namba moja wa Azam FC Aishi Manula amesema, John Bocco ‘Adebayor’ bado alikuwa anahitajika ndani ya kikosi cha Azam.

Manula amesema, licha ya timu yake kusajili wachezaji wengi wa kigeni miaka ya hivi karibuni bado Bocco amekuwa mhimili muhimu ndani ya timu yao kutoka na uwezo wake wa kutupia kambani.

“Unapokuwa na mtu kama Bocco katika timu ni kitu kikubwa sana kwa sababu ametoka mbali na Azam na amefanya mengi makubwa, makombe mengi yaliyopatikana ndani ya Azam FC  nadhani ni katika uongozi wake yeye kama nahodha, ni mtu muhimu sana.

“Bocco ni mchezaji ambaye bado alikuwa anahitajika katika klabu ya Azam, kwa sababu unaweza ukaona wachezaji wengi wanaokuja Azam katika nafasi yake hawafanyi vizuri. Wamesajiliwa wachezaji wengi professional waje waisaidie klabu na hawaisaidii mara zote Bocco anakuwa mkombozi na tegemeo.”

“Kitu cha kufikiria ni kwamba, leo Bocco anaondoka nani anakuja? Tunamuona Shabani Idd anakuja vizuri lakini bado ni kijana mdogo anahitaji support kubwa kutoka Bocco kama alivyokuwa anapewa awali. Nilikuwa nawaona wanakaa pamoja na kuzungumza, tukiwa mazoezini anajaribu kumuelewesha kwahiyo walikuwa ni marafiki.”

“Kuondoka kwa Bocco yule kijana anabaki pekeake kusimama mwenyewe itamuwia vigumu. Bocco anaondoka akiwa anategemewa kama top striker na utaona hata wakati yupo nje anasumbuliwa na majeraha timu ilikuwa inayumba.”

“Bocco kaondoka Azam kwa sababu ya maslahi yake hajaondoka kwa sababu Azam wamemchoka au hawahitaji tena kuwa na yeye kwa sababu uwezo wake umeshuka, uwezo wake haujashuka licha ya kusumbuliwa na mejeruhi.”

“Namtakia maisha mema huko anapokwenda na hata tukikutana nadhani hakutakuwa na uadui kwa sababu soka si uadui.”

Juma lililopita afisa habari wa Azam FC Jafar Idd alithibitisha klabu hiyo kuachana rasmi na Bocco baada ya mshambuliaji huyo kudumu kwa muda mrefu ndani ya Azam.

Daktari wa upasuaji matiti afungwa jela miaka 15

 Daktari wa upasuajia wa matiti Ian Paterson amefungwa jela miaka 15 kwa kufanya upasuaji usio muhimu.

Paterson, mwenye umri wa miaka 59, aliwafanyia upasuaji wanawake tisa na mwanamume mmoja baada ya kuwadanganya kuwa walikuwa na saratani ya matiti.

Amepatikana na hatia ya mashtaka 17 ya kujeruhi kwa makusudi, baada ya kesi iliyodumu kwa mwezi mmoja uliopita.

Jopo la mahakama ya Nottingham liliambiwa kuwa Paterson alizidisha ama kubuni hatari ya saratani.

Mahakama iliambiwa kuwa alifanya upasuaji wa matiti kwa "sababu zisizojulikana" ambazo ni pamoja na shauku ya "kupata pesa za ziada".

BAADA YA KIFO:ndugu wataka uchunguzi kifo cha Ndesamburo

Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Moshi Mjini na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Kilimanjaro, Mzee Philemone Ndesamburo amefariki Dunia asubuhi ya leo katika Hospitali ya KCMC, Mkoani humo.

Katibu wa Chadema mkoa wa Kilimanjaro, Basil Lema amethibitisha muda huu juu ya kifo hicho na kwamba bado haijafahamika chanzo cha kifo chake.

Kwa sasa mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti hospitali ya rufaa ya KCMC.

Ndugu wakiwemo watoto wa marehemu wamefika Hospitalini hapo na kuomba mwili wa marehemu kufanyiwa uchunguzi kutokana na kifo kuwa ni cha ghafla.

Lema alisema, Mzee Ndesamburo alifika ofisini kwake majira ya asubuhi na alionekana mwenye afya njema, ilipofika majira ya saa nne hali ilibadilika na kushindwa kuendelea na majukumu yake.

Ndipo walipomkimbiza KCMC kwa ajili ya matibabu na alifariki dunia akiwa kitengo cha wagonjwa mahututi, Taarifa zaidi tutajulishana kadri zitakapokuwa zikitufikia.
SOURCE:MUUNGWANA

Kambi ya Upinzani Bungeni uvunjwe

MBUNGE wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbles Lema (Chadema), amelitaka Bunge kuvunja Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kutokana na maoni ya kambi hiyo kutosikilizwa.
Lema amedai kuna kuchujwa kwa maneno yanayochangiwa na wabunge wa kambi hiyo katika mijadala katika taarifa za kumbukumbu za Bunge(hansard), alikodai kunafanywa na wafanyakazi wa Studio ya Bunge.

Aliyasema hayo bungeni mjini hapa jana asubuhi aliposimama na kuomba mwongozo wa Kiti cha Spika akidai kuwa michango ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni imekuwa ikihaririwa na baadhi ya maneno yamekuwa yakiondolewa na hivyo kutorushwa kwenye studio hiyo na hata kwenye taarifa wanazopewa waandishi wa habari wa redio na televisheni.

Hata hivyo, katika mwongozo wake kuhusu suala hilo muda mfupi kabla ya kuahirisha shughuli za Bunge jana mchana, Mwenyekiti wa Bunge, Najma Murtaza Giga, aliyekuwa akiongoza kikao cha jana, alisema Studio ya Bunge haina utaratibu wa kuchuja michango ya wapinzani isipokuwa kwa maelekezo ya Kiti cha Spika.

Katika hoja yake, Lema alisema ni bora Bunge lingetoa mwongozo wa kuivunja Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na lisipokee tena maoni yoyote kutoka kwao kutokana na maoni yao kutosikilizwa.

"Mwongozo wangu Mheshimiwa Mwenyekiti kupitia Kanuni ya 68(7) cha jambo lilotokea jana (juzi) jioni, michango ya wabunge tunayochangia humu ndani ni rekodi ya wabunge kama ambayo inavyoingia katika ‘Hansard’ na ni rekodi kwa matumizi yetu binafsi," alisema.

Waziri Kivuli wa Mambo ya Ndani ya Nchi huyo alisema zaidi: "Lakini baadhi ya michango yetu ukifuatilia kule ambako inahifadhiwa kama kumbukumbu zetu binafsi kwa matumizi yetu, Mheshimiwa 'wana-edit' (wanahariri) kwa zaidi ya asilimia 70 na wanaweka mambo ambayo wanayataka wao.

"Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nimechangia Wizara ya Mambo ya Nje na (Ushirikiano wa) Afrika Mashariki, nikaenda nikaambiwa nijaze fomu, nimejaza kutaka kumbukumbu ya mchango wangu, mchango ambao haukuwa hata na mwongozo, haukuwa na taarifa wala utaratibu (bungeni).

"Nimekwenda mambo yote yanayohusu mambo ya Acacia na Diplomasia ya Uchumi yametolewa, wamenibakizia pale panaposema tu kupinga na mtu yoyote anayepinga rasilimali ni mwendawazimu na kipande hicho ndiyo kinazungushwa.

"Sasa Mheshimiwa Mwenyekiti, michango yetu hapa bungeni ni kumbukumbu zetu na hili Bunge Mheshimiwa Mwenyekiti, limeondolewa kuwa 'live' (matangazo ya moja kwa moja) na uhuru wake umeminywa halafu michango yetu ambayo ni halali tukiifuatilia kwa kumbukumbu zetu 'mna-edit'.

"Sasa Mheshimiwa Mwenyekiti, ni bora Bunge hili likatoa mwongozo wa kuvunja Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na msipokee maono yoyote kutoka kwetu."
Awali akijibu mwongozo huo asubuhi, Giga alisema angefuatilia kama madai ya Lema yana ukweli au la na baadaye kutoa majibu bungeni.

"Ni kwamba michango ambayo tunachangia kwa maandishi tunaletewa kwanza hapa kwa ajili ya kuweza kurekebisha lakini kama ni ‘clip’, basi hili suala itabidi nilifuatilie kwa sababu sina uhakika nalo kama ni kweli au siyo kweli, baadaye tutaweza kuleta majibu yangu. Huo ndiyo mwongozo wangu," alisema Giga.

Ndipo kabla ya kuahirisha shughuli za Bunge mchana, Mwenyekiti wa Bunge huyo alisema amefuatilia na kupata maelekezo kwamba studio ya chombo hicho cha kutunga sheria na Ofisi ya Bunge kwa ujumla hawana utaratibu wa kuchuja michango ya wabunge isipokuwa tu kwa maelekezo ya Kiti cha Spika yanayotolewa bungeni.

Alisema taarifa zinazokuwa kwenye 'hansard' zinapaswa kuwiana na 'clip' za mchango wa mbunge husika.

"Kilichotokea kwa mchango wa Mheshimiwa Lema ni kosa la kiufundi na linafanyiwa kazi na likitatuliwa, anaweza kuomba na kupewa mchango wake wote," alisema.

Giga aliongeza kuwa mbunge yeyote atayekumbana na changamoto kama iliyompata Lema, awasilishe malalamiko yake kwenye Ofisi ya Katibu wa Bunge.

Ndugai amkumbuka kwa majonzi Ndesamburo


Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema anamkumbuka marehemu Phillemon  Ndesamburo aliyekuwa mbunge wa Moshi  Mjini (Chadema) kwa uchapakazi wake na mapenzi yake makubwa kwa wapiga kura wake.

“Nimepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha Mheshimiwa Ndesamburo ambaye pia ni baba wa Mbunge wa Viti Maalum,  Lucy Owenya kilichotokea leo Mkoani Kilimanjaro, hakika ni pigo kubwa,”amesema Spika katika taarifa iliyotumwa leo  na Kitengo cha Mawasiliano cha ofisi yake

Ndesamburo amefariki leo wakati akipata matibabu katika hospitali ya Rufaa ya KCMC.

Taarifa hiyo imeongeza; "Namkumbuka vyema marehemu Ndesamburo na tuliingia Bungeni pamoja mwaka 2000, alikuwa na mapenzi makubwa kwa wapiga Kura wake."

Rais Magufuli amlilia Mwasisi wa Chadema



Rais John Magufuli amepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha  mmoja wa waasisi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo, (Chadema) Phillemon Ndesamburo huku akimtaja marehemu kuwa alikuwa kiongozi mwenye hekima na aliyezingatia siasa za kistaarabu.

Taarifa iliyotumwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Gerson Msigwa  leo Jumatano imeeleza kuwa Rais Magufuli , ametuma salamu za rambirambi kwa viongozi na wanachama  wa Chadema pamoja na ndugu, jamaa na marafiki wote walioguswa na kifo hicho.

“Kwa masikitiko nimepokea taarifa za kifo cha Mbunge Mstaafu wa Jimbo la Moshi Mjini, Mzee wangu Philemon Ndesamburo. Namkumbuka Mzee Ndesamburo kwa hekima zake na uongozi wake uliozingatia siasa za kistaarabu,”imesema taarifa hiyo

Rais Magufuli amesema alifanya kazi na Ndesamburo wakati wote wakiwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wakati wote walishirikiana, kutaniana na anamkumbuka kwa namna ambavyo alitumia muda wake bungeni kupigania mambo yenye maslahi kwa wananchi wa jimbo lake la Moshi Mjini.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Magufuli ameitaka familia ya Ndesamburo na wote walioguswa na msiba huu kuwa na moyo wa subira na uvumilivu.
source:muungwana

Mbunifu wa Android azindua simu mpya ya Essential

Essential PhoneHaki miliki ya pichaESSENTIAL PHONE
Image captionSinu ya Essential hutumia mfumo wa Android na imeanza kuuzwa nchini Marekani kwa dola $699.
Andy Rubin, ambaye ni miongoni mwa watu waliobuni programu ya software Android ya Google, amezindua simu yake ya smartphone yenye ncha ndefu.
Bwana Rubin aliacha kazi katika Google mwaka 2014 kwa ajili ya kubuni kampuni yake ya uwekezaji wa kiteknolojia.
Essential ni moja wapo ya kampuni zinazodhaminiwa na kampuni ya Rubin - na simu ya Essential ni moja ya bidhaa zake.
Simu hiyo hutumia mfumo wa Android na imeanza kuuzwa nchini Marekani kwa dola $699.
Hata hivyo, itakuwa ni vigumu kwa kampuni hiyo kujipenyeza katika masoko makubwa ya ambayo tayari yameimarisha mauzo ya bidhaa zake nchini humo.
Samsung kwa sasa ndio yenye soko kubwa la hisa katika soko la simu za Smart, ikiwa na mauzo ya asilimia 21% kote duniani, kulingana na mchambuzi wa masuala ya makampuni Gartner. Apple ina soko la asilimia 14%.
simu ya EssentialHaki miliki ya pichaESSENTIAL PHONE
Image captionKioo cha simu ya Essential kimefunika karibu uso wote wa simu
Licha ya makampuni makubwa ya Uchina yanayouza simu zenye gharama ya chini, viwanda vidogo vidogo vimepata ugumu wa kupata walau asilimia moja ya hisa kwenye soko za bidhaa zao  na bei ya simu ya Essential inaiweka kwenye hali ya changamoto kubwa zaidi
Lakini Bwana Rubin aliiambia hadhira ya watu mjini California kwamba anaamini kuna nafasi ya soko la Android kwa muuzaji mwingine licha ya Samsung, na kwamba Essential inalenga kuwa kampuni kuu inayotoa aina mbali mbali za bidhaa kwa mnunuzi
Essential phone imetengenezwa kwa madini ya titanium na ina kioo kilichoenea sehemu kubwa ya simu na sehemu isiyo na kioo ni ndogo zaidi.