Kahama. Meneja Ufanisi na Maendeleo ya Jamii wa mgodi wa Bulyanhulu, Elias Kastila amesema kilichosababisha Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Terrack na msafara wake kushindwa kuingia ndani ya mgodi huo ni mfumo wa ulinzi unaotegeshwa muda maalumu usioweza kubadilika hadi muda huo ufike.
Kastila amesema isingewezekana msafara huo kuingia mgodini kwa sababu mtambo huo maalumu wa ulinzi ulikuwa umetegeshwa kufunguka saa 12.00 asubuhi ya leo, Ijumaa.
Kwa misingi hiyo, Kastila amesema hakukuwa na namna nyingine ya kufungua mlango wa kuingilia mgodini, labda kulipua kwa bomu au baruti.
Akizungumzia uamuzi wa Mkuu wa Mkoa kuweka ulinzi wa polisi kuzuia mtu kuingia wala kutoka mgodini, Kastila amesema huo umetokana lengo la kujiridhisha hakuna tu labda kuna njama za kutorosha mali, jambo alilosema uongozi wa mgodi hauwezi kufanya kwa sababu hakuna kitu cha kutorosha wala kuficha kutokana na shughuli zote kufanyika kwa uwazi na utaratibu unaoruhusiwa kisheria.
Kwa misingi hiyo, iwapo uongozi wa Serikali mkoani Shinyanga utataka kutembelea na kukagua shughuli mgodini hapo kama ilivyofanya kwa mgodi wa Buzwagi, basi ulipaswa kwenda eneo hilo kuanzia saa 12.00 asubuhi ya leo.
Friday, 26 May 2017
Home »
» Hizi ndizo sababu za Bulyanhulu kumzuia RC
Hizi ndizo sababu za Bulyanhulu kumzuia RC
Related Posts:
Picha: Gari ya kifahari zaidi duniani Huenda ukawa umesikia story nyingi kuhusu magari yaliyoingia sokoni 2017 ila hii ikawa ilikupita. Ni kampuni ya kutengeneza magari ya kifahari dunia Rolls Royce imeingiza sokoni gari ghali zaidi dunia inayoitwa Rolls … Read More
Kalapina awapa salamu hizi waliomteka Roma Mkatoliki Msanii wa muziki wa Bongo Fleva na mmoja wa Watu wanaoaminika kuwa ni Mbabe kama siyo Mtemi na Ngumi Jiwe wa kutukuka Kalapina jana wakati akihojiwa na Kipindi cha XXL kinachorushwa na Clouds fm aliamua kutema nyongo / kuvu… Read More
Kauli ya Zitto Kabwe kufuatia kufungiwa kwa Gazeti la Mawio Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto kabwe amepinga vikali hatua ya kufungiwa kwa gazeti la MAWIO na kudai kuwa hatua hiyo inawanyima Wananchi mawazo mbadala. ==>Kupitia ukurasa wake wa Facebook, … Read More
Kagera Sugar yaibua mapya kuhusu mshambuliaji Mbaraka Yusuf Kegera Sugar hawaelewi lolote kuhusiana na mshambuliaji Mbaraka Yusuf, wanasema ni mali yao.Msisitizo wa Kegera Sugar wanasema wanataka walipwe shilingi milioni 150 ili imuachie mshambuliaji huyo kwenda Azam FC ambako tayar… Read More
Kikwete uso kwa uso na Kardinali Pengo Dubai Dar es Salaam. Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete amemtembelea Mhadhama Polycarp Kardinali Pengo, nchini Dubai leo.Kikwete ameandika katika mtandao wake wa kijamii wa Twitter leo(Ijumaa) na kueleza kuwa amemkuta Kardinali Pengo a… Read More
0 comments:
Post a Comment