Tuesday, 30 May 2017

Mbunge Peter Serukamba asema Rais Magufuli ataigwa duniani kote

Mbunge wa Kigoma Vijijini (CCM), Peter Serukamba amefunguka na kusema jambo alilofanya Rais Magufuli kuzuia mchanga litakwenda kuigwa duniani kote na kuleta mapinduzi katika 'Extractive Industries' kwa kazi kubwa aliyofanya.

Serukamba alisema hayo jana bungeni na kusema ukiona mpinzani wako anakupinga katika jambo lolote lile basi ujue umefanya jambo ambalo ni sahihi ila ukiona mpinzani wako anakusifu ujue umefanya jambo baya, hivyo kwa kuwa wapinzani wanalalamika basi Rais amepatia katika maamuzi yake, na anatakiwa kupewa ushirikiano wa wananchi na wabunge.

"Mimi kama mwanasiasa ukiona mtu ambaye ni adui yako umefanya jambo akakusifia ujue lipo tatizo, ila ukiona umefanya jambo adui yako akasema umekosea maana yake umepatia sana. Mimi naomba nimpongeze Rais Magufuli kwa kazi kubwa aliyofanya na niwaambie waheshimiwa wabunge, duniani kote 'Extractive Industries' inaenda kubadilika atakaye kuwa kwenye historia ya kubadilisha Extractive Industries ni Rais Magufuli, leo duniani kote kila kwenye migodi mambo yatabadilika kwa sababu ya Magufuli amefungua milango, niwaambieni watanzania tusiogope kwenye hili lazima tuwe nyuma ya Rais tumuunge mkono aendelee na nina hakika wawekezaji watakuja mezani" alisisitiza Serukamba 

Related Posts:

  • Kisa cha Polisi kuwapiga Mabomu ya Machozi Walemavu Dar POLISI jana walitumia mabovu ya machozi kutawanya watu wenye ulemavu waliokuwa wamekusanyika na kufunga barabara ya Sokoine jijini Dar es Salaam.Mabomu hayo yalizua taharuki kwa watumiaji wa njia hiyo na kusababisha usumbuf… Read More
  • Takukuru: Tunaendelea Kuwahoji watuhumiwa wa Makinikia TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Takukuru imesema kuwa inaendelea kuwahoji watuhumiwa wote walitajwa kwenye sakata la kusafirisha Makinikia ya madini nje ya nchiOfisa Habari wa  (Takukuru), Mussa Misalaba, ames… Read More
  • Bungeni hapatoshi Sakata la Makinikia BUNGE limeingia siku ya nne jana kujadili Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka 2017/18, huku wabunge kadhaa wakiraruana kuhusu ripoti ya pili ya kamati iliyoundwa na Rais Dk. John Magufuli, kuhusu mchanga wa dhahabau (makinikia)… Read More
  • ida Kaloli: Nibebeni Mkongwe wa muziki wa asili, Saida Karoli amewataka wapenzi wote wa muziki waweze kumbeba ili asipotee tena kama ilivyokuwa hapo awali baada ya kukosa sapoti pamoja na ukosefu wa fedha.Saida amesema baada ya kupata matatizo … Read More
  • Mbunge ataka Zitto, Kafulila waombwe radhi kuhusu Sakata la Makinikia Akichangia mjadala huo wa bajeti, Mbunge wa Viti Maalum, Riziki Ngwali (CUF) alisema wabunge warudi majimboni wakaombe radhi wananchi kwani wao ndiyo walipitisha sheria za madini. “Tuliapa kwa kushika kurani na biblia, kur… Read More

0 comments:

Post a Comment