Sunday, 28 May 2017

Bomba la kupitisha pombe kujengwa Ujerumani

Pombe itakuwepo kwa wingi katika tamasha hiloHaki miliki ya pichaAFP
Image captionPombe itakuwepo kwa wingi katika tamasha hilo
Waandalizi wa Tamasha maarufu la muziki wa rock nchini Ujerumani wamewahakikishia wateja zaidi ya elfu 75 kwamba, katu! hawatokumbwa na kiu ya pombe.
Wanajenga bomba kubwa la kusafirisha pombe katika eneo la tamasha hilo.
Waandalizi wa tamsha hilo maarufu kwa jina, Wacken Open Air festival, wanasema bomba hilo litakuwa na uwezo wa kufikisha glasi sita za pombe kwa kila sekunde.
Bomba hilo litakuwa na urefu wa kilomita 7 na upana wa inchi 14.
Bomba hili litazuia uharibifu unaotokana na mgari ya kusafirisha pombe kila sikuHaki miliki ya pichaWOA WEBSITE
Image captionBomba hili litazuia uharibifu unaotokana na mgari ya kusafirisha pombe kila siku
Watu elfu 75 huwa wanahudhuria tamasha hilo kila mwaka, na inakadiriwa kwamba kila mmoja huwa anabugia lita tano za pombe katika kipindi cha siku tatu.
Zaidi ya watu 75,000 huwa wanahudhuria tamasha hilo kila mwakaHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionZaidi ya watu 75,000 huwa wanahudhuria tamasha hilo kila mwaka

Related Posts:

  • Kutana na Msikiti unaojengwa ila mafundi hawaonekani Uliwahi kusikia jengo linalojengwa kwa muda mrefu zaidi na mafundi hawaonekani, iwe usiku au mchana jengo linazidi kupanda juu, pia ata magari ya kubeba kokoto, mchanga hata matofari yasionekane...!!! Hii ni mpya kutok… Read More
  • "Manji anatikisa kibiriti" Katibu wa baraza la wazee wa Yanga Mzee Ibrahim Akilimali amesema, huenda kujiuzulu kwa mwenyekiti wa klabu hiyo Yusuf Manji ni kutikisa kibiriti tu lakini atarejea tena kwenye nafasi yake kwa sababu tayari alishawahi kuta… Read More
  • Professa Muhongo amemuibua Kafulila Alikuwa Mbunge Kigoma Kusuni,  David Kafulila ameibuka na kutoa kauli yake maamuzi yaliyofanywa na Rais Magufuli baada ya kupokea ripoti ya Kamati Maalum kuhusiana na uchunguzi wa makontena 272 ya makinikia yaliyokuwa … Read More
  • Meri ya kivita ya Marekani imeonakana karibu na visiwa vya Uchina Maafisa wa Marekani wanasema manowari ya wanamaji wa Marekani imetekeleza oparesheni maalum ya 'uhuru wa ubaharia' karibu na visiwa vinavyozozaniwa vya bahari ya kusini mwa china. Oparesheni hiyo karibu na kisiwa kimoja… Read More
  • Ratiba ya Sportpesa Super Cup Sport Pesa Cup 5/6 Singida united Vs FC leopardYanga Vs Tusker fc6/5 Simba Vs Nakuru All StarJang`ombe boys vs Gor mahiaNusu fainali tarehe 8Bingwa wa mechi kati ya Singida united vs AFC leopard atacheza na bingwa kati ya… Read More

0 comments:

Post a Comment