Friday, 26 May 2017

Gereza siyo hoteli - Mrema

Mwenyekiti wa bodi ya Parole Taifa Mh. Augustino Lyatonga Mrema amewaonya wananchi kuacha kutenda makosa yatakayo wafanya kukataliwa kurudi kwenye jamii pindi watakapohitaji kupata msamaha 'Parole' na kusisitiza gerezani siyo hoteli.

Mapema wiki akifanya mahojiano EATV, Mhe. Mrema ameweka wazi kuwa hakuna mfungwa anayeweza kupatiwa msamaha na bodi ya Parole ikiwa tayari jamii yake haimtaki na kuongeza kuwa mfungwa atalazimika kutumikia kifungo chake.

Aidha Mrema ameongeza kwamba watu wamekuwa wakifanya makosa makubwa kwenye jamii hali ambayo inawanyima nafasi za misamahaa ambayo ni haki yao na kwamba tatizo linakuja wakati wakupata ruhusa kwa jamii anayoishi kukataa kutoa ruhusa.

"Huwa tunaauenda eneo analoishi au alipozaliwa kuwaeleza watu juu ya msamaha wanaotaka kuutoa na kama wakikataa kwa sababu na wao haki yao kukubali aua kukataa basi mtuhumiwa utarudishwa tu magereza. Nataka kuwaasa acheni kufanya mambo yatakayowafanya mkatliwe, jiepusheni na makosa yatakaowafanya mkose haki yenu labda itokee bahati mbaya" Mh. Mrema alifunguka.

Pamoja na hayo ameongeza kwamba jamii haipaswi kuwakataa watu wao walipo magereza kwani baada ya kumaliza kifungo watarudi kwenye maeneo yao na hawatakuwa na uwezo wa kuzuia waendelee kukaa magereza.

"Jamii inatakuwa ifahamu hawa watu waliopo magereza ni bdugu zao na ni watu wao. Tengezenezeni mahusiano mazuri na siyo kwamba mtu akishafungwa ndio anageuka mnyama mnatakiwa mtambue ni binadamu na ana haki zake zote za kimsingi" aliongeza Mrema.

Related Posts:

  • HALI TETE:Chenge agoma kuzungumza Vigogo waliotajwa katika ripoti ya pili ya kuchunguza makontena yenye mchanga wa madini (makinikia)  kuisababishia Serikali hasara ya matrilioni ya fedha kupitia sekta ya madini, walipokuwa wakihudumu katika nyadhifa … Read More
  • AJALI:Gari la polisi laua bodaboda Gari la Polisi MTU mmoja amefariki dunia na mwingine kujeruhiwa baada ya pikipiki maarufu kwa jina la bodaboda waliyokuwa wakitumia kusafiri, kugongana uso kwa uso na gari la Jeshi la Polisi katika wilaya ya Rorya… Read More
  • Mzee Akilimali ataka kumpiku Manji, atangaza kuwania uenyekiti Yanga AKILIMALI Katibu Mkuu wa Baraza la Wazee wa Yanga, Ibrahimu Akilimali ametangaza kuwania nafasi ya uenyekiti wa klabu ya hiyo iliyoachwa wazi hivi karibuni na aliyekuwa mwenyekiti wa klabu hiyo, Yusuf Manji.Hivi karibuni M… Read More
  • Lissu Amtolea Uvivu JK kuhusu kusaini mikataba ya Madini Mwanasheria Mkuu wa Chadema Tundu Lissu ameitaka Serikali kumjumuisha Rais Mstaafu kwenye tuhuma za Makontena ya Mchenga wa Dhahabu,Akichangia bungeni katika hotuba ya bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2017/18, Lissu am… Read More
  • HIKI HAPA: alichokisema John Bocco Bocco (kulia) akikabidhiwa jezi ya Simba na rais wa klabu hiyo Evans Aveva, imeteka vichwa vya habari vya mitandao mbalimbali ambapo mashabiki wa Simba wameonyesha kufurahishwa na usajili huyo. UONGOZI wa Simba, jana umeta… Read More

0 comments:

Post a Comment