JESHI la Polisi mkoani Morogoro linamshikilia Pastory Chilangazi (37), mkazi wa Kijiji cha Mamvisi, Wilaya ya Gairo kwa tuhuma za kumuua mkewe kwa kipigo kutokana na kile kinachoelezwa ni kutofautiana baada ya mkewe huyo kudai fedha za matibabu ya mtoto wao.
Ilielezwa zaidi kuwa baada ya kufanya mauaji hayo, mtuhumiwa aliutupa mwili wa mkewe mtoni.
Akizungumza ofisini kwake jana, Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei, alisema tukio hilo lilitokea Mei 22, majira ya asubuhi.
Kamanda Matei alisema mwanaume huyo alimpiga ngumi na mateke mkewe, Edina Mazengo (32), katika sehemu mbalimbali za mwili wake na kusababisha kifo kabla ya kwenda kuutupa mwili wake katika Mto Chumvi.
“Taarifa tulizopata huko ni kwamba mwanamke huyo alimwomba mumewe fedha za kumpeleka mtoto hospitalini.
Hapo ndipo kulipotokea vurugu na mwanaume kuanza kumpiga mke wake hadi kumsababishia umauti,” alisema Kamanda Matei, akimtaja mtoto wa wawili hao aliyekuwa akitakiwa kupelekwa hospitalini kuwa ni Emmanuel Pastory (4).
Alisema tayari mtuhumiwa ameshakamatwa na polisi na anaendelea kuhojiwa kabla ya kufikishwa mahakamani.
source:muungwana
Friday, 26 May 2017
Home »
» Aua mkewe kisa pesa ya matibabu
Aua mkewe kisa pesa ya matibabu
Related Posts:
Qatar yaapa kutosalimu amri mzozo wake na nchi za KiarabuHaki miliki ya pichaREUTERSImage captionSaudi Arabia na nchi nyingine kadha za Kiarabu zimesitisha safari za ndege kuingia na kuondoka Qatar Qatar imeapa kwamba haitasalimu amri katika mzozo wake kuhusu sera yake ya kigeni na… Read More
Nini kitafanyika sasa baada ya uchaguzi Uingereza?Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES Nini kitafanyika kukikosekana mshindi wa moja kwa moja katika uchaguzi mkuu? Chama chenye wabunge wengi kitaunda serikali? Si lazima. Chama chenye wabunge wengi baada ya kura zote kuhesabiwa… Read More
Mwanasheria Mkuu wa TBS Afikishwa Mahakamani Mwanasheria Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Baptister Marco (54) amepandishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu mashtaka matatu ya kuishi na kufanya kazi nchini bila kuwa na kibali.Mwendesha Mashtaka w… Read More
Wakamatwa na dawa za kulevya Mwanza Jeshi la Polisi Mwanza linawashikilia watu wanne baada ya kuwakuta na dawa za kulevya aina ya Mirungi mafungu 57 yenye ukubwa wa kilogramu 56.75 ambayo yalikuwa yamewekwa kwenye mabegi na magunia.Kamanda wa Polisi Mwanza, A… Read More
Dkt Mpango awasilisha taarifa ya hali ya uchumi kwa mwaka 2016 Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango. Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango amewasilisha taarifa ya hali ya uchumi kwa mwaka 2016 na Mpango wa maendeleo ya uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2017/2018. Akiwa… Read More
0 comments:
Post a Comment