Friday 26 May 2017

Rais wa FIFA aipongeza Yanga

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Kimataifa (FIFA), Gianni Infantino, Mei 24, mwaka huu alituma ujumbe Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuipongeza Young Africans ya Dar es Salaam kwa kutwaa ubingwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu wa 2016/17.

Young Africans imetwaa Kombe hilo ikiwa ni mara tatu mfululizo na katika salamu za pongezi, Rais Gianni Infantino amesema ubingwa huo wa Young Africans ni kielelezo cha ushirikiano baina ya wachezaji, kocha, utawala, matabibu pamoja na mashabiki.

Katika pongezi zake Rais Infantino ameishukuru Young Africans na shirikisho la mpira wa miguu la nchi kwa kusadia kupeleka ujumbe chanya kwa jamii kuhusiana na mpira wa miguu.

0 comments:

Post a Comment