Mwanamke mmoja amekutwa akiwa amefariki dunia chumbani kwake huku mwili wake ukiwa na majeraha baada ya kupigwa na mumewe, wilayani ilemela mkoani Mwanza.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza DCP Ahmed Msangi amesema kwamba tukio hilo limetokea leo tarehe 30, Mei 2015 saa 9:09 alfajiri katika mtaa wa Pasiansi Mashariki wilayani humo.
Kamanda Msangi amesema tukio hilo limetokea baada ya kuzuka kwa ugomvi kati yao ambapo mwanamke huyo aliyefahamika kwa jina la Ester Charles (30) alipigwa na mumewe na baadaye mwanamume huyo anayefahamika kwa jina la Charles John (35) kutoroka kusiko julikana.
Inadaiwa kuwa marehemu alikuwa akiishi nyumbani kwao na mumewe lakini kwa kipindi chote wakiwa kwenye mahusiano wawili hao walikuwa kwenye migogoro ya mara kwa mara ya ndani ya familia kwani mwanamke alikuwa akimtuhumu mumewake kwamba anatoka nje ya ndoa.
JINSI ILIVYOKUWA
Inasemekana kuwa usiku huo majirani walisikia ugomvi ukiendelea kati ya wawili hao huku mwanamke akipiga kelele akiomba msaada, lakini majirani hawakwenda kuwasaidia kwani walizoea kuwasikia wakipigana na baadaye kuelewana kisha kuendelea na maisha kama kawaida.
Baada ya muda kupita hapakusikika tena ugomvi hivyo majirani walijua tayari wameelewana, lakini baadaye alisikika mtoto akilia kwa muda mrefu ndipo walipata mashaka kisha walitoa taarifa kituo cha polisi.
Polisi walifika eneo la tukio kisha kumkuta mwanamke huyo akiwa tayari amepoteza maisha, huku mwili wake ukiwa na majeraha ya kupigwa na kitu kizito maeneo mbalimbali ya mwili wake na shingoni kwake kukionekana kukabwa na kitambaa kigumu na mumewe aliyekuwa wakipigana kisha baada ya kuona mkewe amefariki dunia alitoroka kusiko julikana.
Amesema polisi wapo kwenye msako mkali wa kuhakikisha mtuhumiwa wa mauji hayo anakamtwa, huku upelelezi ukiwa unaendelea.
source:muungwana
Tuesday, 30 May 2017
Home »
» Mume amuua mkewe kwa kipigo
Mume amuua mkewe kwa kipigo
Related Posts:
Mwigizaji maarufu wa filamu za James Bond Roger Moore amefariki Mwigizaji maarufu wa filamu za James Bond Roger Moore amefariki.Katika taarifa ya familia yake marehemu iliochapishwa katika mtandao wake wa Twitter, walisema ''ni vigumu kutangaza kifo cha baba yetu Roger Moore ambaye amef… Read More
Polisi watangaza dau la Mil. 60 Ukiwakamatisha hawa JESHI la Polisi mkoa wa Pwani limetangaza zawadi ya Sh. milioni tano kwa mwananchi ambaye atafanikisha kukamatwa kwa watuhumiwa 12 ambao limedai wanajihusisha na mtandao wa mauaji yanayoendelea katika Wilaya za Kibiti, Mku… Read More
Nape amemjibu Makonda, Picha limeanza upyaaa Siku moja baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam kuhojiwa na kituo cha Star Tv kuhusu mambo kadha wa kadha likiwemo suala la uvamizi wa Clouds Media na kusema Hakupaswa kumuingilia kwakuwa wote ni watumishi... Basi Nape ame… Read More
Korea Kusini yashambulia kifaa cha Korea Kaskazini Korea Kusini inasema kuwa imekishambulia ''kifaa'' kutoka Korea Kaskazini kilichorushwa katika eneo lisilo la kijeshi.Takriban risasi 90 zilifyatuliwa zikielekezwa kwa kifaa hicho ambacho kufikia sasa hakijajulikana kilikuw… Read More
Madhara ya Mvua ya siku sita yaua 10, yabomoa nyumba 44 Tanga. Tathmini ya madhara yaliyotokana na na mvua zilizonyesha kwa siku sita mfululizo wiki iliyopita mkoani hapa zimeonyesha kuwa hadi sasa watu 10 wamekufa huku nyumba 44 zikibomoka na nyingine 218 zikizingirw… Read More
0 comments:
Post a Comment