Friday 26 May 2017

Yanga yapigwa faina ya milioni moja na TFF

Kamati ya Saa 72 imekaa kupitia mambo mbalimbali na moja ya uamuzi wake ni kuhusiana na Yanga kugoma kuingia vyumbani.

Mechi namba 206 (Yanga 1 Vs Toto Africans 0).

Klabu ya Yanga imepigwa faini ya sh. 1,000,000 (milioni moja) kutokana na timu yake kutoingia vyumbani wakati wa mechi hiyo iliyochezwa Mei 9, 2017 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.


Adhabu hiyo imetolewa kwa mujibu wa Kanuni ya 14(48) ya Ligi Kuu. Uamuzi huo umezingatia pia kuwa Yanga imekuwa ikirudia kosa hilo mara kwa mara.

0 comments:

Post a Comment