Dar es Salaam. Watanzania 27 wamejeruhiwa katika ajali ya basi kampuni ya Falcon walilokuwa wakisafiria kutokea Tanzania kuelekea Uganda, baada ya kuangukia upande wa kushoto njia kuu ya Masaka, Uganda.
Abiria hao walikuwa njiani kuelekea Namugongo katika sherehe za siku ya Martyrs ambayo ahudhimisha na waumini wa Kanisa Katoliki kote duniani kila ifikapo Juni 3.
Polisi nchini Uganda wanasema basi hilo lenye usajili namba T967-BTA lilishindwa kupanda mlima iliyopo kati ya eneo la Kyatera na Masaka baada ya breki ya gari hizo kufeli na kusababisha ajali.
Hata hivyo polisi hao wamesema hakuna majeruhi walio kwenye hali mbaya.
Miongoni mwa waliojeruhiwa ni Maria Ngonyari, Robert Imman (40), Alex Rono (64), Angela Kigulwe Biringi (65), Gloria Mwisa (29), Emiyana Babweiga (65) na Julliet Arshdes (40).
Kamanda wa polisi kikosi cha usalama barabarani nchini, Mohamed Mpinga amesema ni kweli ajali hiyo imetokea na kwamba majeruhi wapo katika hali nzuri.
“Majeruhi walitibiwa na kisha kuendelea na safari hakuna aliyeumia sana,” amesema Mpinga
Tuesday, 30 May 2017
Home »
» Basi la Falcon lapata ajali Uganda, Watanzania 27 wajeruhiwa
Basi la Falcon lapata ajali Uganda, Watanzania 27 wajeruhiwa
Related Posts:
Mbunifu wa Nembo ya Taifa ahamishiwa Hosptali ya Muhimbili Mzee Francis Ngosha ndiye mchoraji na mbunifu wa nembo ya taifa maarufu kama Bibi na Bwana, S iku mbili zilizopita aliliripotiwa kuwa anaishi maisha ya Magumu huko Buguruni jijini Dar es salaam. Kibanda alichokuwa akiishi… Read More
Nyalandu: Majeruhi wa Lucky Vicent kuruhusiwa Hospotali kesho Hospitali ya Mercy ya Marekani, imebainisha kuwa huenda watoto wawili majeruhi wa ajali ya gari la Shule ya Lucky Vincent wakaruhusiwa kutoka hospitali wakati wowote kuanzia kesho.Mbunge wa Singida Kaskazini, La… Read More
Mauaji Pwani yamepangwa: Mbunge Dodoma. Mauaji katika wilaya za Kibiti na Rufiji jana yaliibuka bungeni kwa mara ya pili, wakati mbunge wa Rufiji (CCM), Mohamed Mchengerwa alipoeleza siri ya mipango na kiini chake.“Nataka niseme na Rais wangu ajue. Mambo … Read More
Wajumbe wa kamati Iliyomng'oa Muhongo walitishwa RAIS Dk. John Magufuli amebainisha kuwa licha ya kamati ya Kuchunguza Makontena ya Mchanga wenye Madini (makinikia) kupewa ulinzi mkali, kulikuwapo vitisho na hata baadhi ya wajumbe kutaka kuhongwa. Akizungumza jana wak… Read More
Ujumbe wa Diamond Baada ya Ivan kufariki Dunia Kupitia ukurasa wake wa Instagram Diamond Platnumz ameandika ujumbe huu "Mbele yako, Nyuma yetu" Ujumbe huo ni baada ya Aliyekuwa mume wa Zarina Hassan ‘Zari The Bosslady’, Ivan Semwanga kufariki dunia akiwa hospitali nchi… Read More
0 comments:
Post a Comment