Dar es Salaam. Watanzania 27 wamejeruhiwa katika ajali ya basi kampuni ya Falcon walilokuwa wakisafiria kutokea Tanzania kuelekea Uganda, baada ya kuangukia upande wa kushoto njia kuu ya Masaka, Uganda.
Abiria hao walikuwa njiani kuelekea Namugongo katika sherehe za siku ya Martyrs ambayo ahudhimisha na waumini wa Kanisa Katoliki kote duniani kila ifikapo Juni 3.
Polisi nchini Uganda wanasema basi hilo lenye usajili namba T967-BTA lilishindwa kupanda mlima iliyopo kati ya eneo la Kyatera na Masaka baada ya breki ya gari hizo kufeli na kusababisha ajali.
Hata hivyo polisi hao wamesema hakuna majeruhi walio kwenye hali mbaya.
Miongoni mwa waliojeruhiwa ni Maria Ngonyari, Robert Imman (40), Alex Rono (64), Angela Kigulwe Biringi (65), Gloria Mwisa (29), Emiyana Babweiga (65) na Julliet Arshdes (40).
Kamanda wa polisi kikosi cha usalama barabarani nchini, Mohamed Mpinga amesema ni kweli ajali hiyo imetokea na kwamba majeruhi wapo katika hali nzuri.
“Majeruhi walitibiwa na kisha kuendelea na safari hakuna aliyeumia sana,” amesema Mpinga
Tuesday, 30 May 2017
Home »
» Basi la Falcon lapata ajali Uganda, Watanzania 27 wajeruhiwa
Basi la Falcon lapata ajali Uganda, Watanzania 27 wajeruhiwa
Related Posts:
Milio ya risasi yatanda miji mikuu Ivory Coast
Ufyatulianaji mkali wa risasi umezuka katika miji miwili mikuu nchini Ivory Coast, wanajeshi wakiendelea kuasi kwa siku ya nne mtawalia.
Wanajeshi hao waliogoma wamefunga barabara nje ya kambi za jeshi katika mtaa wa kifah… Read More
DIPLOMA AJUCO WAICHAPA SECOND YEAR AJUCOLigi ya AJUCO (inter class) imeendelea leo katika viwanja vya RMA ambapo mechi nne zilichezwa na mechi ya kwanza ilichezwa kati ya AJUCO second year na AJUCO diploma majira ya saa nane mchana.
Lakini kwa upande w… Read More
Korea Kaskazini: Kombora jipya lina uwezo wa kubeba nyuklia
Gwaride la kijeshi lililofanywa na Korea Kaskazini hivi karibuni
Korea Kaskazini imedai kwamba kombora la masafara marefu ililolifanyia majaribio siku ya Jumapili ni kombora jipya linaloweza kubeba kichwa cha nyuklia .
Kom… Read More
Trump atakiwa kusalimisha kanda za mazungumzo na James Comey
Wabunge waandamizi nchini Marekani wamemtaka rais Donald Trump kusalimisha mazungumzo yoyote yaliorekodiwa kati yake na aliyekuwa mkurugenzi wa shirika la FBI James Comey aliyemfuta kazi.
Kiongozi wa Democrats katika bunge… Read More
Microsoft: Shambulizi la Kompyuta liwe funzo
Shambulizi la uhalifu wa mitandaoni lililoathiri mataifa 150 tangu siku ya Ijumaa linafaa kuchukuliwa kama funzo, Microsoft imesema.
Kampuni hiyo ya kompyuta inasema kuwa hatua ya serikali hizo kutoimarisha programu zao m… Read More







0 comments:
Post a Comment