Wednesday, 31 May 2017
Home »
» Simba yapania Kumsajili Aishi Manula na kumtema Agyei
Simba yapania Kumsajili Aishi Manula na kumtema Agyei
SIMBA inataka kumuacha kipa Mghana, Daniel Agyei ili imsajili kipa wa Azam FC, Aishi Manula.
Na hiyo ni kufuatia habari za Aishi kutokubaliana na Azam kuongeza mkataba, baada ya kumalizika kwa mkataba wake wa sasa mwezi ujao.
Uongozi wa Simba SC unaamini ukimpata Aishi hautakuwa na sababu ya kuingia gharama za ziada kwa kuendelea kuwa na kipa wa kigeni, Agyei aliyejiunga na Wekundu hao wa Msimbazi Desemba mwaka jana kutoka Medeama SC ya Ghana.
Hata hivyo, wazo hilo linapingwa na baadhi ya viongozi wa Simba, wanaoamini Agyei ni bora zaidi ya Aishi na ndiye anayeIfaa klabu hIyo kwa sasa ikirejea kwenye michuano ya Afrika.
Simba ilikata tena tiketi ya kurudi kwenye michuano ya Afrika, baada ya kutwaa Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) kufuatia ushindi wa 2-1 dhidi ya Mbao FC ya Mwanza Uwanja wa Jamhuri Dodoma Jumamosi iliyopita.
Na kwa ushindi huo, Simba imekata tiketi ya kucheza michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika mwakani na pia itafungua msimu ujao kwa kumenyana na mahasimu, Yanga SC katika mechi ya Ngao ya Jamii.
Simba ilicheza michuano ya Afrika kwa mara ya mwisho, mwaka 2013 na kutolewa na Recreativo de Lobolo ya Angola Raundi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa vipigo vya nyumbani na ugenini, ikifungwa 1-0 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na 4-0 ugenini.
Na Agyei ameidakia Simba jumla ya mechi 25 za mashindano yote, akifungwa mabao 10 huku mechi 16 akidaka bila kuruhusu nyavu zake kuguswa.
Alisajiliwa kuchukua nafasi ya kipa Muivory Coast, Vincent Angban ambaye naye pia aliachwa akiwa ana rekodi nzuri.
Related Posts:
GEOGRAPHY U.E PAPERS SOLVED (PROF.MUSHALA) COURSE NAME: PROJECT PLANNING AND MANAGEMENT COURSE CODE:GE : 349 LECTURER: PROF.MUSHALA TASK : SOLVED U.E 2 PAPERS OF 2014/2015-2015/2016 1. Discuss the Basic Roles and Responsibilities of a Project Manager… Read More
ALIVYOAPISHWA RAIS WA CHUO KIKUU CHA AJUCO RAIS WA AJUCO NA MAKAMU WAKE Hatimaye ile siku iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu ni leo tarehe 1/7/2017 katika ukumbi wa NYERERE 0NE ,ambapo rais aliyeshinda kiti cha urais katka chuo kikuu cha AJUCO MR. SUNGURA amea… Read More
Shilingi 180,000 za mjamzito zamtokea puani mganga mkuu Waziri wa afya, Ummy Mwalimu amemsimamisha kazi mganga mfawidhi wa Kituo cha Afya Mlandizi, Stanley Mpola kwa kushindwa kutekeleza majukumu yake. Waziri Ummy ametoa agizo hilo alipotembelea kituo hicho cha afya kabla ya… Read More
Ukosefu wa bangi wasababisha dharura kutangwazwa Nevada, MarekaniMaafisa katika jimbo la Nevada nchini Marekani wanachukua hatua za dharura kukabiliana na uhaba wa bangi. Mahitaji yamekuwa ya juu tangu bangi ihalalishwe kwa matumizi ya kujiburudisha tarehe mosi mwezi huu. Hii imetokana na … Read More
Serikali yatangaza ajira 3,152 sekta ya afya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto leo imetangaza ajira 3,152 kwa ajili ya wahitimu wa kada mbalimbali za afya nchini. Kwa mujibu wa tangazo lililotolewa na wizara hiyo, ajira hizo ambazo zinatolewa k… Read More
0 comments:
Post a Comment