Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Moshi Mjini na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Kilimanjaro, Mzee Philemone Ndesamburo amefariki Dunia asubuhi ya leo katika Hospitali ya KCMC, Mkoani humo.
Katibu wa Chadema mkoa wa Kilimanjaro, Basil Lema amethibitisha muda huu juu ya kifo hicho na kwamba bado haijafahamika chanzo cha kifo chake.
Kwa sasa mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti hospitali ya rufaa ya KCMC.
Ndugu wakiwemo watoto wa marehemu wamefika Hospitalini hapo na kuomba mwili wa marehemu kufanyiwa uchunguzi kutokana na kifo kuwa ni cha ghafla.
Lema alisema, Mzee Ndesamburo alifika ofisini kwake majira ya asubuhi na alionekana mwenye afya njema, ilipofika majira ya saa nne hali ilibadilika na kushindwa kuendelea na majukumu yake.
Ndipo walipomkimbiza KCMC kwa ajili ya matibabu na alifariki dunia akiwa kitengo cha wagonjwa mahututi, Taarifa zaidi tutajulishana kadri zitakapokuwa zikitufikia.
SOURCE:MUUNGWANA
Wednesday, 31 May 2017
Home »
» BAADA YA KIFO:ndugu wataka uchunguzi kifo cha Ndesamburo
BAADA YA KIFO:ndugu wataka uchunguzi kifo cha Ndesamburo
Related Posts:
BAADA YA KUISHINDWA KOREA KASKAZINI:Marekani kuwawekea vikwazo washirika wa kibiashara wa Korea KaskaziniHaki miliki ya pichaREUTERSImage captionRex Tillerson Marekani inasema itaziwekea vikwaza nchi ambazo zinafanya biashara haramu na Korea Kaskazini, kwa mujibu wa waziri wa mashuri ya nchi za kigeni Rex Tillerson Alisema kuwa… Read More
Mwanafunzi mgonjwa mmarekani aliechiliwa kutoka Korea Kaskazini alazwa hospitaliniHaki miliki ya pichaREUTERSImage captionWarmbier alikuwa amehukumiwa kifungo cha miaka 15 jela na kazi ngumu Mwanafunzi raia wa Marekani ambaye aliachiliwa kutoka gerezani nchini Korea Kaskazini, amepelekwa hospitalini nchini… Read More
Aliyekuwa gavana wa Rio de Janeiro afungwa miaka 14 kwa ufisadiHaki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionSergio Cabral alihudumu mihula miwili kama gavana wa Rio kuanzia mwaka 2007 hadi 2014. Aliyekuwa gavana wa jimbo la Rio de Janeiro nchini Brazil, amehukumiwa kifungo cha miaka 14 g… Read More
Muasi Bosco Ntaganda kutoa ushahidiHaki miliki ya pichaAFPImage captionBosco Ntaganda maarufu 'Terminator' Aliyekua kiongozi wa waasi nchini Congo, Bosco Ntaganda anatarajiwa kutoa ushahidi leo katika mahakama ya kimatafa ya ICC. Ntaganda aliyepewa jina la 'T… Read More
TAMBUA:Aspirin ni hatari kwa watu wenye umri mkubwaHaki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionVidonge vya Aspirin ni hatari kwa watumiaji wa umri wa zaidi ya miaka 75 Watu walio na umri wa zaidi ya miaka 75 ambao hutumia dawa aina ya Aspirin baada ya kupata kiharusi au mara… Read More
0 comments:
Post a Comment