Sunday, 28 May 2017

Trump 'atengwa' na wenzake G7

Rais Trump ametengwa na wenzake kuhusiana na makubaliano ya tabia nchi yaliofakiwa mjini Paris
Image captionRais Trump ametengwa na wenzake kuhusiana na makubaliano ya tabia nchi yaliofakiwa mjini Paris
Viongozi katika mkutano wa G7 wametofautiana kuhusu taarifa ya mabadiliko ya tabia nchi.
Viongozi sita walikubaliana kuunga mkono makubaliano ya mjini Paris ,ambayo ni ya kwanza yanayolenga kupunguza hewa chafu.
Hatahivyo Marekani imekataa kukubaliana ikisema kuwa itatoa uamuzi wake wiki ijayo.
Bwana Trump ambaye alidai kwamba ongezeko la joto duniani ni ''mzaha'' mara kwa mara ametishia kujiondoa katika makubaliano hayo.
Huu ni mkutano wa kwanza wa G7 kuhudhuriwa na Trump katika ziara yake ya kwanza ya kigeni.
Viongozi wa G7 kutoka Uingereza, Marekani ,Canada Ufaransa ,Ujerumani ,Italy na Japan wamekubaliana kuhusu kukabilina na ugaidi .
Kwa nini hakuna makubaliano kuhusu mabadiliko ya tabia nchi?
Tarifa ya mwisho iliotolewa katika mkutano huo unaofanyika nchini Itali ilisema kuwa Marekani iko katika harakati ya kufanyia marekebisho sera zake, hivyobasi kuhusu makubaliano ya Paris haitajiunga na mataifa mengine kukubaliana na swala hilo.
Hatahivyo mataifa hayo ya G7 yaliapa kuonyesha umoja wao katika kuidhinisha makubaliano hayo ya Paris.
Kansela wa Ujerumani alisema kuwa ''mazungumzo kuhusu mabadiliko ya tabia nchi hayaridhishi ,akiongezea kuwa kuna hali ya mataifa sita dhidi ya ya taifa moja''.

Related Posts:

  • Rais wa FIFA aipongeza Yanga Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Kimataifa (FIFA), Gianni Infantino, Mei 24, mwaka huu alituma ujumbe Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuipongeza Young Africans ya Dar es Salaam kwa kutwaa ubingwa Ligi Kuu… Read More
  • TAMBUA VYUO VINAVYOTAMBULIKA NA NACTENIMEAMUA KUKUWEKEA ORODHA YA VYUO VINAVYOTAMBULIKA NA NACTE ILI KUEPUKA KUTAPELIWA NA VYUO FEKI. BONYEZA HAPA>>>>>>>>.ORODHA YA VYUO VINAVYOTAMBULIKA NA NACTE… Read More
  • Kenya: Afariki dunia baada ya kutabiri kifo chake  Irene Chris aliolewa kwa harusi Agosti 2016 na mumewe Chris Mwangi - Mnamo January 2017,Irene aliandika katika mtandao wa kijamii kwamba alikuwa akielekea mbinguni na kuwaomba watu kutuma salamu -Miezi minne baadaye… Read More
  • Yanga yapigwa faina ya milioni moja na TFF Kamati ya Saa 72 imekaa kupitia mambo mbalimbali na moja ya uamuzi wake ni kuhusiana na Yanga kugoma kuingia vyumbani.Mechi namba 206 (Yanga 1 Vs Toto Africans 0).Klabu ya Yanga imepigwa faini ya sh. 1,000,000 (milioni moja… Read More
  • Huu ndio ugonjwa unaomsumbua mbunifu wa nembo ya Taifa RIPOTI ya awali ya uchunguzi wa kiafya aliofanyiwa mbunifu wa Nembo ya Taifa (bibi na bwana), Francis Ngosha (86) katika Kitengo cha Magonjwa ya Dharura Hospitali ya Mkoa ya Amana, inaonyesha kuwa anakabiliwa na tatizo la l… Read More

0 comments:

Post a Comment