Dodoma. Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema anatamani kupanda mabasi ya mwendo wa haraka yaliyoko jijini Dar es Salaam.
Pia, ameishauri kampuni ya usafiri ya Udart kuangalia uwezekano wa kuwekeza mjini
Dodoma.
Akizungumza leo (Jumanne) baada ya kukutana na maofisa wa Udart waliomkabidhi majarida ya kutimiza mwaka mmoja tangu kuanza shughuli za usafirishaji, Ndugai amesema siku akifika Dar es Salaam atahakikisha anapanda mabasi hayo, akiwataka wasaidizi wake kumkumbusha ili kujionea jinsi linavyoendeshwa.
Amesema kitendo cha mradi huo mkubwa kuendeshwa na Serikali kwa kushirikiana na mbia ambaye ni Mtanzania ni kielelezo kwamba Watanzania wanaweza.
Ndugai amewataka Udart kuboresha usafiri huo kwa kuongeza mabasi na kampuni hiyo kuangalia namna ya kuwa na mabasi mjini
Dodoma kwa kuwa ndiko yaliko makao makuu ya nchi na watu wameongezeka.
Mkuu wa Kitengo cha Habari Msaidizi wa Udart, Joe Beda amesema watafanya kila linalowezekana kuhakikisha mradi huo unakuwa endelevu kwa kuwa ni
moja ya miradi ya aina yake barani Afrika.
Tuesday, 30 May 2017
Home »
» Spika Ndugai atamani kupanda mabasi ya mwendo kasi
Spika Ndugai atamani kupanda mabasi ya mwendo kasi
Related Posts:
Serikali imezuia Passport za Chenge, Muhongo, Kafumu, Karamagi Serikali imeagiza, Mawaziri, Wanasheria Wakuu wa Serikali na Manaibu wao, Wakurugenzi wa idara za mikataba, na Makamishna wa madini, wanasheria wa Wizara ya Nishati na Madini na watumishi wengine wa Serikali na watu wote wa… Read More
Diamond afunguka mchango wa Wema Sepetu kwenye ‘Chibu Perfume’. Msanii wa muziki, Diamond platnumz amefunguka kuuzungumzia mchango wa malkia wa filamu, Wema Sepetu kwenye perfume yake ya ‘Chibu Perfume’.Diamond amekiambia kipindi cha XXL cha Clouds FM kuwa, yeye na Wema wanakutana na ku… Read More
Madee Awashangaa Mastaa Wapenda Kiki MKALI wa Ngoma ya Hela, Hamad Ally ‘Madee’ amewashangaa baadhi ya mastaa ambao katika Mwezi wa Mfungo wa Ramadhani wamekuwa na utamaduni wa kutoa vitu kwa jamii na kupiga picha kisha kujionesha kwenye mitandao ya kijamii ki… Read More
Pogba kutua Tanzania Klabu ya Everton inajiandaa kuja nchini Tanzania kwa ziara ya kujiandaa na msimu ujao wa ligi ambapo wakiwa hapa wtacheza na washindi wa kombe la Sports Pesa timu ya Gor Mahia kutoka nchini Kenya. Sasa Everton wanaweza … Read More
Alichosema Zitto Kabwe baada ya ripoti ya madini "Mwisho wa siku historia inaandikwa tu. Uzalendo ni kufanya jambo ambalo wengi hawakuelewi lakini wewe unajua Ni jambo sahihi na unakubali kutukanwa, kususubikwa, kusimangwa, kuzushiwa, nk. Unapambana tu. Mwisho wa siku wa… Read More
0 comments:
Post a Comment