Maelfu ya wafanyabiashara wa Soko kuu la Jijini Mwanza, Mlango mmoja pamoja na Buzuruga, Juni 5 mwaka huu wametishia kufanya mgomo usiokuwa na kikomo yakiwemo maandamano, kwa lengo la kupinga upandishwaji wa gharama za kodi ya pango la biashara bila kushirikishwa.
Baada ya halmashauri ya Jiji la Mwanza na Manispaa ya Ilemela, kupandisha kodi ya pango kutoka shilingi 50,000 hadi 4000,000/=, wafanyabiashara hao wanaangua vilio, ili Serikali iweze kuwasikiliza
Kilio cha wafanyabiashara hao kimetolewa mbele ya waandishi wa habari katika eneo la soko kuu la Mwanza, baada ya baadhi yao kusitisha shughuli za kujitafutia kipato, kutokana na uzito wa ongezeko la kodi hiyo.
Kutokana na kilio hicho Ofisi ya Rais, tawala za mikoa na Serikali za mitaa kupitia barua yenye kumbukumbu No. CB 78/237/01 ya Machi 10 mwaka huu, tayari imeshaiagiza Ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza kushughulikia hoja hizo.
Kwa mantiki hiyo Channel, ikalazimika kuwatafuta wakurugenzi wa halmashauri ya Jiji la Mwanza na Manispaa ya Ilemela kuzungumzia suala hilo, ambapo baada ya kupatikana wakasema kuwa msimamo wa kodi hizo hautabadilishwa na atakayeshindwa kulipa aachie eneo.
Tuesday, 30 May 2017
Home »
» Wafanya biashara jijini Mwanza watishia kufanya mgomo Juni tano mwaka huu
Wafanya biashara jijini Mwanza watishia kufanya mgomo Juni tano mwaka huu
Related Posts:
Watu 8 wafariki baada ya kimbunga kugonga Afrika KusiniHaki miliki ya pichaIMAGE COPYRIGHTImage captionAlex De Kock alipiga picha hii akitazama kimbunga hicho kutoka kilima cha Signal Hill mjini Cape Town Watu 8 wamefariki baada ya kimbunga kikali kugonga mji wa Cape Town, Afrika… Read More
Mwanamke akamatwa China akiwa na mikoba iliyotengenezwa kwa cocaineHaki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionMwanamke akamatwa China akiwa na mikoba iliyotengenezwa na cocaine Maafisa wa forodha mjini Shanghai nchini China, wanasema kuwa wamemkamata mwanamke ambaye alijaribu kusafirisha m… Read More
Sudan kumhukumu kifo mwanaharaki wa haki za BinadamuHaki miliki ya pichaAMNESTYImage captionMkereketwa wa haki za binadamu, Bw. Sudan Mudawi Ibrahim Adam Mwanaharakati mmoja maarufu nchini Sudan Bw. Mudawi Ibrahim Adam, angali amesalia ndani ya jela, baada ya kuzuiliwa na waku… Read More
Kwa taarifa yako, ndoa inaimarisha moyoImage captionUvalishanaji pete Utafiti nchini Uingereza umebaini kwamba ndoa inaleta afya ya moyo. Utafiti uliofanywa kwa zaidi ya miaka 13 kwa zaidi ya watu laki tisa ambao wana matatizo aina tatu ya moyo, umebaini kwamba w… Read More
Raia kulipwa kuuwa panya MynmarImage captionPanya wavamizi Maelfu ya panya wamevamia vijiji kadhaa katika manispaa ya mji wa Nga Pu Taw, kusini magharibi mwa jimbo la Ayeyarwady nchini Mynmar. Vyombo vya habari nchini humo, vinasema kuwa vyakula na mimea … Read More
0 comments:
Post a Comment