Thursday, 25 May 2017

Wanafunzi 33 Meatu wamekatisha masomo kutokana na Ujauzito

Responsive image
Mimba imekuwa ni chanzo kimojawapo kinachochangia kurudisha nyuma ustawi wa elimu hapa nchini.
Wanafunzi 33 wa sekondari wilayani Meatu mkoani Simiyu wamekatisha masomo yao baada ya kupata ujauzito katika kipindi cha mwaka 2016 hadi mwezi April mwaka huu.
Afisa Elimu sekondari wilaya ya Meatu, Estomih Makyara ametoa takwimu hizo katika kikao cha baraza la madiwani baada ya hoja kutolewa na baadhi ya madiwani wakimtuhumu mwalimu wa shule ya sekondari kumpa ujauzito mwanafunzi.
madiwani wameshauri uwepo wa mabweni kwa ajili ya wanafunzi wa kike huku wakisisitiza kuchukuliwa kwa hatua kali kwa watakaobainika kuwapa ujauzito wanafunzi.

Related Posts:

  • Ally Mayay, Mtemi kuwania urais TFF  MAYAY Ally Mayay anatarajia kuchukua nafasi ya kuwania Urais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).Taarifa zinaeleza Mayay ambaye ni mchezaji wa zamani wa Yanga na Taifa Stars, atachukua fomu hizo leo. MTEMI Wa… Read More
  • Simba yatumia Mil. 100/ kumshawishi Niyonzima NI UMAFIA TU! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya kiungo wa Yanga, Haruna Niyonzima kudaiwa kujiunga na Klabu ya Simba kwa mkataba wa miaka miwili baada ya kupewa ofa ya Sh. milioni 100. Habari zilizopatikana jana jioni … Read More
  • Zitto aukataa Urais TFF Ijumaa ya Aprili 21, mwaka huu, gazeti la michezo na burudani nchini, Mwanaspoti, liliandika habari kwenye ukurasa wake wa kwanza yenye kichwa: "Zitto ajitosa Urais TFF, Rage amkubali." Upande wangu, licha ya kwamba hab… Read More
  • Nchemba amtolea uvivu Tundu Lissu  Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba ‘amemvaa’ Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu kwamba amejaribu kutengeneza kila aina ya kichaka kukwamisha jitihada za Rais John Magufuli kupambana na usafirish… Read More
  • Hoja 6 moto mkali kwa serikali bungeni MJADALA wa mapendekezo ya makadirio ya bajeti ya serikali kwa mwaka wa fedha wa 2017/2018 unatarajiwa kuhitimishwa leo mjini hapa huku hoja sita zikionekana kuwa mtihani mgumu kwa serikali kuzitolea majibu kesho wakati in… Read More

0 comments:

Post a Comment