Friday, 26 May 2017

Kenya: Afariki dunia baada ya kutabiri kifo chake


 Irene Chris aliolewa kwa harusi Agosti 2016 na mumewe Chris Mwangi - Mnamo January 2017,

Irene aliandika katika mtandao wa kijamii kwamba alikuwa akielekea mbinguni na kuwaomba watu kutuma salamu -Miezi minne baadaye, mwanamke huyo mrembo ameaga dunia na marafiki wake wamejua kuwa alikuwa na hisia kwamba angeaga dunia

Irene Chris, mkewe Chris Mwangi alikuwa na maono ya kifo chake. Alidokeza hata katika mitandao ya kijamii ingawa ni wachache waliofahamu.

Harusi ya Irene ilikuwa Agosti 2016 na ilihudhuriwa na marafiki na familia yake. Katika ujumbe alioweka katika mtandao wa kijamii, miezi kadhaa baada ya kufanya harusi,

Irene aliwaomba marafiki wake kumtuma salamu kwa kusema kuwa alikuwa akielekea mbinguni.
Wengi marafiki wake walimkosoa kwa kusema hilo na kumwambia kuondoa ujumbe huo pamoja na kukoma kuzungumzia kifo.

Wengine walipizilia mbali ujumbe huo kwa kusema ulikuwa utani. Katika ujumbe mwingine, alisema alikuwa akikumbuka marafiki wake waliokufa. Lakini hakuna aliyeshikanisha jumbe hizo kwamba alikuwa akiwaaga kwaheri.

Irene alizikwa nyumbani mwa mumewe Wanyororo, Lanet, Kaunti ya Nakuru Alhamisi Mei 25 na kuacha mumewe na mtoto wake wa wiki mbili.

Related Posts:

  • Wapelekwa kortini kwa tuhuma za kuiba kanisani WAKAZI wa wawili wa Ubungo Riverside, Dar es Salaam, Ayubu Sanga (21) na Nafaife Kayinga (19) wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Mwanzo Kinondoni kwa tuhuma za kuiba vitu vyenye thamani Sh 1,025,000 katika Kanisa la… Read More
  • Diamond Platnumz ataja moja ya vigezo vya kujiunga na familia ya WCB Mwimbaji staa wa Bongofleva kutoka WCB Diamond Platnumz amefunguka kupitia 255 ya XXL ya Clouds FM na kusema kuwa sifa ya kwanza ya WCB ni kumtoa msanii kwenye hali ngumu ili waweze kufanikiwa wote kwa kuwa huwa na adabu na… Read More
  • Gerard Pique awaponda tena Real Madrid. Kama kuna kitu kinawakera mashabiki wa Real Madrid baasi ni mtu anayeitwa Gerard Pique, mlinzi huyu wa kati wa Barcelona amekuwa hawezi kuikalia kimya Real Madrid hata kama wamefungwa au wameshinda.Baada ya Real Madrid kufa… Read More
  • Ester Bulaya asema: Hamjatuziba midomo Mbunge wa Bunda Mjini Mh. Ester Bulaya ametoa salamu kwa Wabunge wa CCM pamoja na Spika Job Ndugai kutambua kwamba hata baada ya kumuadhibu kutohudhuria vikao bya bunge siyo silaha ya kuwafunga midomo.Bulaya amefunguka hayo… Read More
  • Wakamatwa na dawa za kulevya Mwanza Jeshi la Polisi Mwanza linawashikilia watu wanne baada ya kuwakuta na dawa za kulevya aina ya Mirungi mafungu 57 yenye ukubwa wa kilogramu 56.75 ambayo yalikuwa yamewekwa kwenye mabegi na magunia.Kamanda wa Polisi Mwanza, A… Read More

0 comments:

Post a Comment