Friday, 26 May 2017

Adhabu kali kwa Raia Wanaoishi bila ndoa Burundi

Pierre-Nkurunziza Rais wa Burundi
Watu wanaoishi katika mahusiano ya mume na mke bila kufunga ndoa nchini Burundi wameamrishwa kwamba wawe wameoana rasmi ifikapo mwishoni mwa mwaka huu la sivyo wataaadhibiwa vikali.

Msemaji wa Wizara ya mambo ya ndani na elimu Terence Ntahiraja amesema amri hiyo itasaidia kile alichokitaja kuwa ni ongezeko la watu nchini Burundi.

Amesema mahusiano yasiyo rasmi yamesababisha wasichana wengi wa shule kupata ujauzito na wanaume kupata fursa ya kuwa na mahusiano ya wanawake wengi kwa mkupuo.

Rais Pierre Nkurunziza, ambaye ni muumini wa kilokole , hivi karibuni alianzisha kampeni ya kitaifa ya maadili mema.

Waziri Ntarihaja ameambia AFP kwamba ndoa zilizorasmishwa kanisani au katika afisi ya serikali ndiyo suluhu pekee kwa tatizo la ongezeko kubwa la watu nchini humo na kwamba ni jukumu la kizalendo.

"Tunawataka raia wa Burundi wafahamu kwamba kila mtu anawajibikia maisha yake, na tunataka utulivu na utawala wa sheria humu nchini," alisema.

"Juhudi zote zinafanywa kwa kufuata mkakati wa kuwafunza raia wawe wazalendo," alisema, akirejelea mpango huo wa kueneza uzalendo uliozinduliwa na Rais Nkurunziza.

Haijabainika ni adhabu gani ambayo watapewa wale ambao hawatakuwa wamerasmisha ndoa zao kufikia mwisho wa mwaka huu.

source:muungwana

Related Posts:

  • Zitto njia panda uteuzi Anna Mghwira Kiongozi wa Chama Cha Act-Wazalendo hajajua cha kujibu kuhusu suala la uteuzi wa Mwenyekiti wa Chama hicho  Anna Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro. Zitto amesema kuwa Chama hicho kitatoa tamko baada ya Mwen… Read More
  • Uwoya astushwa na habari za Ujauzito Sexy lady wa sinema za Kibongo, Irene Pancras Uwoya ‘Mama Krish’ amefungukia madai kuwa, kwa sasa ametengeneza urafiki wa muda na ndimu, samaki wabichi na ukwaju kwa kinachosemekana ni mjamzito.Huku akionesha kushtushwa na … Read More
  • PICHA: Jinsi Juventus walivyorejea kwao baada ya kipigo cha Real Madrid  Baada ya kupoteza kwa kufungwa kwa mabao 4-1 dhidi ya Real Madrid katika fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, Juventus wamerejea nyumbani Italia.Pamoja na kuukosa ubingwa, mashabiki walionekana kuwapongeza wakiwapungia … Read More
  • Mataifa sita ya Kiarabu yavunja uhusiano wao na QatarHaki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionMji mkuu wa Qatar, Doha Mataifa sita ya Kiarabu, zikiwemo Saudi Arabia, Misri, Bahrain, Umoja wa Milki za Kiarabu na Yemen, yamekata uhusiano wao wa kidiplomasia na Qatar yakiilaum… Read More
  • VIDEO:Aliyetengeneza Audio Wema na Mbowe VIDEO:Aliyetengeneza Audio Wema na Mbowe Baada ya Audio Ambayo imewekwa kwenye mtandao wa Jamii Forums Ikisikika sauti zinazosemekana kuwa ni Wema Sepetu na Freeman Mbowe Wakiongea Kimahaba Wakipanga kukutana Kwa ajili ya… Read More

0 comments:

Post a Comment