Monday, 22 May 2017

Vijana wanne wambaka binti wa miaka 15


Watu watatu wanashikiliwa na jeshi la polisi huku mwingine mmoja akiendelea kutafutwa kwa tuhuma za kumbaka binti mmoja mwenye umri wa miaka 15 wilayani Ilemela, mkoani Mwanza.

Akitoa taarifa hiyo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza DCP Ahmed Msangi amesema kwamba tukio hilo limetokea tarehe 21/05/2017 majira ya saa moja kamili jioni katika maeneo ya mamlaka ya pamba, kata ya Kirumba ambapo inadaiwa kuwa binti huyo ambaye pia ni mkazi wa Kirumba alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na mtuhumiwa aliyejulikana kwa jina moja la Phili na walipanga wakutane katika maeneo hayo.

Inasemekana kuwa binti huyo alikutana na mpenzi wake mahali hapo kisha walikwenda sehemu yenye jumba bovu kuzungumza, wakiwa kwenye eneo hilo ghafla walitokea vijana wengine watatu t\wakishirikiana na Phili na kuanza kumfanyia ukatili kwa kumbaka.

Inasemekana kuwa wakati wakiendelea na ukatili huo binti alipiga yowe akiomba msaada kutoka kwa wananchi, wananchi walifika eneo la tukio na kumuokoa binti na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa mmoja aitwaye Fredy Remigius kisha walitoa taarifa polisi kuhusiana na tukio hilo.

Askari walifika katika eneo la tukio na kufanya msako mkali wa kuwatafuta watuhumiwa wengine huku wakishirikiana na wananchi na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa wengine wawili huku mmoja aliyekuwa na mahusiano ya kimapenzi na binti akifanikiwa kutoroka.

Amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Fredy Remigius miaka 20, mkazi wa Kitangiri, Jackson Joseph miaka 17, mkazi wa Mlimani B na Frank Haruni miaka 18.

Kamanda Msangi amesema mahojiano na watuhumiwa waliokamatwa yanaendelea na pindi uchunguzi ukikamilika watafikishwa mahakamani na kwamba majeruhi aliyebakwa amepelekwa hospitali ya mkoa wa Mwanza Sekou Toure kwa ajili ya matibabu na hali yake inaendelea vizuri.

Related Posts:

  • ACACIA WAPINGA UCHUNGUZI WA KAMATI VITA kubwa. Ndivyo unavyoweza kusema baada ya Rais Dk. John Magufuli kuanza kuchukua hatua kali dhidi ya usafirishaji wa mchanga unaodaiwa kuwa na dhahabu. Baada ya hatua hiyo ya Rais Magufuli, kumeanza kuibuka mambo kadh… Read More
  • Dola ya Marekani inateteleka WATUNGA sera kutoka Benki Kuu ya Marekani, wamesema wanafuatilia kilichoko katika uchumi wa taifa, kutokana na kuongezeka kiwango cha riba za benki nchini humo na imefanya thamani ya fedha za dola kushuka.Mchumi wa nchi hiy… Read More
  • LUKUVI ATANGAZA KITANZI KWA MADALALI WA ARDHI tarajia kuandaa sheria itakayowabana madalali katika sekta ya ardhi. Amesema lengo la sheria hiyo ni kuwabana madalali hao ambao wamekuwa wakiuza ardhi katika siku za mapumziko kutokana na sababu wanazozijua wao. Lukuv… Read More
  • TAMKO LA SERIKALI: WANAJESHI HAWANA HAKI YA KUTESA RAIA SERIKALI imesema hakuna sheria yoyote inayowapa haki wanajeshi kutesa raia au kuvunja sheria. Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Hussein Mwinyi, alitoa kauli hiyo wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu… Read More
  • Hatimaye simu mpya za Nokia 3310 zaingia madukani  Simu hizo mpya za Nokia 3310 zitakaa muda mrefu na chaji kuliko simu asiliSimu za Nokia 3310 zimeanza kuuzwa tena madukani, takriban miaka 17 baada ya simu hizo kuanza kuuzwa mara ya kwanza.Simu za sasa zina kamera ya… Read More

0 comments:

Post a Comment