Thursday 29 June 2017

SIKIA ALICHOKIONGEA RAIS MTEULE SUNGURA (AJUCSO )

Jana tarehe 28/6/2017 Chuo kikuu kishiriki cha AJUCO ambacho ni Tawi la SAUT ulifanyika uchaguzi wa kuwapata wabunge na Rais watakao hudumu kwa kipindi cha mwaka mmoja. Wagombe wengi walijitokeza kuwania nafasi za ubunge lakini kwa upande wa Urais  hali ilikuwa ngumu sana kwani wagombea watatu wa kinyang'nyilo cha urais walipatikana watatu tu ambao ni Mr. January, Mr. Adam na Lomituni, ambao baada ya mchujo Mr. January na  Mr. Adam ndyo waliingia kwenye kinyang'anyilo hicho na hatimaye baada ya safari ndefu ya kampeni,na hatimaye kupiga kura Mr.Adam alpata kura 143 na Mr. Sungura alipata kura 522 na kutangazwa mshindi wa kiti cha urais. Wabunge walioshinda ni pamoja na WAILES TYSON First year 'A', MWANYIKA FELIX First year 'B' na CHUMA MATHIAS Second year.
SIKILIZA SAUTI YA RAISI MTEULE NA ALIYEKUWA MPINZANI WAKE HAPO CHINI
AU CLICK LINK HII>>>>>>>>https://www.youtube.com/watch?v=MwEoRioHIv4

Sunday 25 June 2017

Mbwa mwenye sura mbaya zaidi duniani atajwa

Martha, ametajwa kuwa mbwa mwenye sura mbaya zaidi duniani.Haki miliki ya pichaEPA
Image captionMartha, ametajwa kuwa mbwa mwenye sura mbaya zaidi duniani.
Martha, ametajwa kuwa mbwa mwenye sura mbaya zaidi duniani.
Shindano la kila mwaka ambalo sasa liko katika mwaka wake wa 29 lilifanyika katika eneo la Petalum mjini Carlifornia.
Martha anayemilikiwa na Shirly Zindler aliwashinda wapinzani 13 na kupewa taji na pesa taslimu dola 1,500.
Mbwa huyo mwenye taya kubwa sasa atasafirishwa hadi mjini New York kwa maonyesho ya vyombo vya habari kulingana na waandalizi wa shindano hilo.
Maonyesho hayo ya Sonoma Marin yanasema kuwa shindano hilo huwashirikisha mbwa wengi ambao wameokolewa katika makaazi na maeneo ya kukuza mbwa kwa lengo la kuwauza.
Mbwa mwenye sura mbaya zaidi dunianiHaki miliki ya pichaEPA
Image captionMbwa mwenye sura mbaya zaidi duniani
Martha ni mbwa aliyeokolewa ambaye karibia awe kipofu kutokana na kupuuziliwa mbali alisema bi Zindler.
''Baada ya kufanyiwa upasuaji sasa anaweza kuona tena na hahisi uchungu wowote''.
Shirika la habari la AP limesema kua Martha aliibuka mshindi kwa kutembea katika ukumbi na kuwavutia majaji.
Majaji hao walimpatia ushindi mbwa huyo kutokana na hisia za watu, sura, tabia na hisia zake.
source:bbc

Saturday 24 June 2017

JIFUNZE HIKI: DOWNLOAD MOVIES NA MUSICS BURE YOUTUBE BILA KUWA NA DOWNLOADER YEYOTE

JINSI YA KUDOWNLOAD VIDEO  YEYOTE YOUTUBE BILA KUWA NA DOWNLOADER YEYEOTE

1) Go to www.youtube.com. Open the page of the video you want to download.


2) Add "ss" between the www. and the youtube.com section of the URL and hit enter. 


Example:


Original YouTube URL:  http://www.youtube.com/watch?v=ykF-rktutV4&list=CLTaJ1PHDR84I&feature=plcp


Modified YouTube URL: http://www.ssyoutube.com/watch?v=ykF-rktutV4&list=CLTaJ1PHDR84I&feature=plcp



3) This will redirect your browser to another site SaveFrom.net:


4) Choose the format of the video. Click on the link of the format. 
  
5) And your download will start in your downloader.



ENJOY YOUR TIME IN MUSICS AND MOVIES

Monday 19 June 2017

Watu wenye silaha washambulia eneo la watalii Mali

Le Campement Kangaba, eneo lililoshambuliwaHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionLe Campement Kangaba, eneo lililoshambuliwa
Vyombo vya Usalama nchini Mali vinasema vimeokoa zaidi ya wageni thelathini kutoka katika kituo kimoja cha Utalii, kilichokuwa kikishambuliwa na watu waliokuwa na silaha.
Waziri wa Ulinzi wa nchi hiyo Salif Traore amethibitisha kuuawa kwa watu wawili, baada ya watu wanaohisiwa kuwa ni wapiganaji wenye itikadi kali kushambulia eneo hilo la starehe la Le Campement Kangaba lililoko nje ya mji mkuu wa nchi hiyo Bamako.
Kwa mujibu wa Waziri huyo wa Usalama, mmoja wa washambuliaji hao alifanikiwa kutoroka, baada ya kujeruhiwa, huku akiacha bunduki na chupa zilizokuwa na vifaa vya milipuko.
Aidha amesema watu wawili akiwemo raia mmoja pia walijeruhiwa.
Majeshi ya Mali na Ufaransa yalifika katika eneo la tukio.
Wanajeshi wa Ufaransa eneo la tukioHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionWanajeshi wa Ufaransa eneo la tukio
Kituo hicho cha utalii ni maarufu nyakati za juma la wiki na kuwa kivutio kwa raia wa Mali wenye uwezo na wale wa kigeni wanaoishi Bamako.
Mapema mwezi huu, Ubalozi wa Marekani mjini Bamako ulionya uwezekano wa kutokea mashambulizi katika siku za baadaye katika majengo ya wanadiplomasia wa magharibi na maeneo mengine katika mji wa Bamako ambako raia wa nchi za magharibi wanapenda kwenda.
Wapiganaji wa Kiislamu wameendelea kufanya mashambulizi nchini Mali licha ya kupoteza maeneo yao wanayoyashikilia wakati wa uvamizi uliofanywa na majeshi ya muungano yaliyokuwa yakiongozwa na Ufaransa mwaka 2003.

Marekani yatoa majina ya wanajeshi waliouwawa baharini



The USS Fitzgerald, damaged by colliding with a Philippine-flagged merchant vessel, on 17 June 2017.Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionAjali hiyo ilisababisha shimo kubwa kweny meli ya kijeshi
Marekani imetangaza majina ya wanajeshi wake 7 ambao waliuawa wakati meli yao iligongana na ile ya mizigo katika eneo la bahari ya Japan siku ya Jumamosi.
Wanjeshi hao walipatikana katika maneo yaliyokuwa yamefurika maji ndani ya meli hiyo ya kivita ya USS Fitzgerald.
Wanajeshi wengine watatu walijeruhiwa kwenye kisa hicho ambacho kilitokea karibu na mji wa bandari wa Yokosuka.
Meli hiyo kwa sasa imepelekwa huko YokosukaHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionMeli hiyo kwa sasa imepelekwa huko Yokosuka
Wengi wa wanajeshi walikuwa wamelala wakati meli hizo ziligongana. Marekani inasema kuwa inafanya uchunguzi.
Wanajeshi hao waliripotiwa kutoweka baada ya ajali hiyo.
Kamanda wa meli ya kijeshi Joseph P Aucoin aliwaambai waandishi wa habari kuwa ajali hiyo ilisababisha shimo kubwa kwenye meli ya kijeshi.
Wanajehsi hao saba ni pamoja na:
  • Dakota Kyle Rigsby, 19
  • Shingo Alexander Douglass, 25
  • Ngoc T Truong Huynh, 25
  • Noe Hernandez, 26
  • Carlos Victor Ganzon Sibayan, 23
  • Xavier Alec Martin, 24
  • Gary Leo Rehm Jr, 37
Map showing location of USS Fitzgerald crash - 17 June 2017
Image captionRamani inayoonyesha eneo la ajali

Marekani yashambulia na kuiangusha ndege ya jeshi la Syria

US F/A-18E Super HornetHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionNdege sawa na hii yaA F/A-18E Super Hornet ya Syria ndiyo iliangushwa
Muungano unaoongozwa na Marekani nchini Syria umeangusha ndege ya jeshi la Syria katika mkoa wa Raqqa.
Jeshi la Syria lilisema kuwa ndege yake ya kijeshi ilikuwa katika harakati za kushambulia kundi la Islamic State wakati ilishambuliwa siku ya Jumapili.
Imesema kuwa kisa hicho kitakuwa cha athari katika vita dhdi ya ugaidi.
Marekani ilisema kuwa ilichukua hatua za kujilinda baada ya serikali ya Syria kuangusha mabomu karibu na wapiganaji wanaoungwa mkono na Marekani.
Kisa hicho kilitokea mji wa Ja'Din ambao unashikiliwa na vikosi vya Syrian Democratic Forces (SDF).
Wapiganaji wa SDF wanaoungwa mkono na muungano unaoongozwa na Marekani wamezingira ngome ya IS huko Raqqa.
Saa mbili kabla ya ndege hiyo kuangushwa, Marekani ilisema kuwa vikosi watiifu kwa raisi wa Syria Bashar al-Assad viliwashambulia wapiganaji wa SDF na kuwajeruhi kadha.
Mapema mwezi huu, Marekani iliangusha ndege isiyo na rubani ya seriikali ya Syria, baada ya ndege hiyo kushambulia vikosi karibu na kivuko cha mpaka cha al-Tanf kwenye mpaka kati ya Syria na Iraq.

Tambua Madhara ya Ulaji wa Chipsi

Chips ni aina ya chakula ambacho hupendwa na watu wengi na pia ni miongoni mwa vyakula vyenye mafuta mengi. chips pia inasemekana ni miongoini mwa vyakula ambavyo hupikwa katika joto la juu zaidi ya 300 degree.

Chips ni chakula chenye mafuta mengi na mafuta yanapoingia mwilini huenda kuzunguka sehemu ya mwili wa mwanadamu. kama ni mtu ambaye mazoezi pia hufanyi madhara yake ni kupata magonjwa ya moyo. hivi sasa idadi kubwa ya vijana wanaugua magonjwa mengi yanayo sababishwa na mkusanyiko wa mafuta katika miili yao amabayo huchangiwa na kuto kufanya mazoezi madhara yake mafuta kuziba mirija

Mafuta yakiliwa sana husababisha kuzidi mwilini.
Pia inasadikika mafuta yaliyopo katika chipsi katika sahani moja ya chisi ya moto endapo utaamua kuchuja kuna uwezekano wa kupata nusu glasi ya mafuta ya kupikia. Kwa hali hii ujue ni hatari.

Na mwili huwa hatupi kinachofaa, na badala yake kama hakitumiki wakati huo basi huhifadhiwa kwa matumizi ya baadaye. Ndio maana tunapokula vyakula vyingi vyenye mafuta mengi hutupelekea kuongeza unene na uzito.

Unene huwa ni chanzo cha magonjwa mengi ,Kwani (High Blood pressure) hutokana na kuwa na mafuta mengi mwilini ambayo hupelekea mirija ya kusafirisha damu kuwa na mafuta. Hii husababisha njia ya kupitia damu kuwa nyembamba hivyo kusababisha nguvu ya ziada itumike kusukuma damu hiyo ili isambae mwilini kama inavyotakiwa. Nguvu hii ya ziada huongeza au kupunguza mapigo ya moyo.

Mapigo ya moyo yanapoongezeka sana ni hatari na yanapo pungua sana pia ni hatari.
Hivyo basi ni vizuri kwa watumiaji wa chipsi kujitahidi kutumia kwa kiasi kidogo au kuacha kabisa vile vile mazoezi pia ni muhimu ili kupunguza mrundikano wa mafuta katika mwili.

Pia inasemekana kuwa wanasayansi wamegundua kuwa chipsi husababisha kukuza hips hivyo kwa wanaume wengi hawatapenda kuwa katika hali hiyo, hivyo ni muhimu kujiepusha na pia isije ikawa kichocheo kwa wanawake kutumia sana ili kukuza sehemu hizo za maumbile bali wapunguze kutumia chipsi pamoja na kufanya mazoezi ili kuweka mwili katika hali ya kuepuka magonjwa yasiyo ya lazima.pia ulaji wa chips kupita kiasi husababisha wanaume na wanawake kuzeeka mapema.

Mwanajeshi wa Korea Kaskazini ahamia K. Kusini kwa kuogelea

Mwanajeshi mmoja wa Korea Kaskazini ametorokea Korea Kusini kupitia kuvuka mto Han kwa kuogelea ,ikiwa ni mara ya pili kwa raia wa taifa hilo kuhamia kwa majirani zao.

Mkuu wa Jeshi nchini Korea Kusini amesema kuwa mwanajeshi huyo aliogelea na kupitia eneo moja jembamba sana la maji ya mto huo yalio na kasi kubwa baada ya kuvalia boya lilolomsaidia kuelea.
Wiki iliopita mwanajeshi mwengine wa Korea Kaskazini alipitia mpaka unaolindwa sana unaogawanya mataifa hayo mawili.

Wanajeshi walikuwa wakihamia Korea Kusini katika kiwango cha mmoja kwa mwaka.

Mwanajeshi huyo aliyedaiwa kuwa na miaka ya ishirini alipatikana katika eneo la Gimpo, Magharibi mwa mji mkuu wa Korea Kusini Seoul, kulingana na chombo cha habari cha Yonhap.

Alipiga kelele akisema ''musiniue'', niko hapa kuhama ,kwa mwanajeshi wa Korea Kusini ambaye alikuwa amemuona, kilisema chombo cha habari cha Yonhap.

Mwanajeshi huyo sasa atahojiwa na maafisa wa kijeshi, Korea Kaskazini na Kusini ziko katika vita baradi tangu mzozo kati yao umalizike 1953 kupitia makubaliano.

Seoul inasema kuwa zaidi ya raia 30,000 wa Korea Kaskazini wamehamia kusini tangu kumalizika kwa vita vya Korea, wengi wao kupitia China ambayo ina mpaka mrefu na Korea Kaskazini.


Ajinyonga kisa ugumu wa maisha

Kijana Paulo Ezekiel, amejinyonga kutokana na kile kinachodaiwa ugumu wa maisha.

Paulo (17) alikuwa anaishi na wazazi wake Mtaa wa Mazinge Kata ya Ndembezi mjini Shinyanga, alifariki dunia juzi usiku kutokana na kudaiwa kujinyonga kwa kamba juu ya mti jirani na nyumbani kwao.

Tukio hilo lilitokea majira ya saa kumi alfajiri baada ya marehemu kutoka nje ya geti la nyumba yao na kuelekea kwenye mti huo kisha kijipiga kitanzi kunakodaiwa kusababisha kifo chake.

Akizungumza tukio hilo jana, baba mzazi wa marehemu, Ezekiel alisema awali kijana wake alikuwa na ugomvi na marafiki zake ambao ni madereva bodaboda, lakini huo ulisuluhishwa na akaendelea na majukumu yake.

Alisema chanzo cha kifo chake hakijafahamika vizuri, lakini mara kwa mara alikuwa akilalamika kuwa maisha ni magumu.

"Ilipofika majira ya saa 10 usiku nilisikia mlango wa chumba cha kijana wangu ukifunguliwa, nikajua ametoka kwenda kujisaidia lakini muda mrefu ulipopita bila kusikia amerudi, ndipo nikatoka nje na kukuta geti la uani likiwa wazi, nikaanza kumtafuta bila mafanikio", alisema.

Aliongeza:
"Niliporudi ndani nikamwamsha mama yake mzazi na wadogo zake wa kike, tukaanza kumsaka ndipo tukamuona akiwa juu ya mti jirani na nyumba yetu, akiwa ameshafariki kwa kujinyonga na kamba".

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Jumanne Murilo, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa hakuna mtu yeyote anayeshikiliwa na jeshi la hilo kuhusiana na tukio hilo.

Alisema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha maiti katika Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga na unatarajiwa kuzikwa leo kwenye Makaburi ya Mtaa wa Dodoma mjini hapa.

Chanzo: Nipashe

Mawaziri wawili wabanwa

CHAMA cha ACT-Wazalendo kimelaumu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba na Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama kufuatia kitendo cha Jeshi la Polisi kutumia nguvu kutawanya maandamano ya watu wenye ulemavu jijini Dar es Salaam juzi.

Chama hicho pia kimemtaka Waziri Mwigulu kuiomba radhi jumuiya ya watu wenye ulemavu kutokana na kitendo hicho.

Aidha, ACT imemtaka Waziri Mhagama kuhakikisha madai ya watu wenye ulemavu yanasikilizwa na kutolewa majibu.

Polisi walitumia mabomu ya machozi kuwatawanya watu wenye ulemavu waliokuwa wamefunga Barabara ya Sokoine jijini Dar es Salaam Ijumaa, kabla ya kukamata 40 kati yao, akiwamo mwanamke mmoja.

Walemavu hao walikuwa na lengo la kwenda kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala kuwasilisha malalamiko ya bajaj zao kukamatwa kamatwa na askari wa usalama barabarani.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam kuhusu tukio hilo, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa ACT-Wazalendo, Ado Shaibu alisema wanalaani vikali Jeshi la Polisi kutumia nguvu "kubwa" kwa watu wenye ulemavu ambao hawakuwa na silaha yoyote.

"Tunamtaka Waziri mwenye dhamana ya Jeshi la Polisi, Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba kuiomba radhi jumuiya ya watu wenye ulemavu hapa nchini kwa kitendo cha Jeshi la Polisi na kuhakikisha vitendo kama hivi havirudiwi tena," alisema Shaibu.

Shaibu alisema Waziri Mhagama naye anapaswa kuhakikisha madai ya walemavu yanasikilizwa.

Pia ACT iliitaka Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kuchukua hatua kali kwa jeshi hilo kufuatia vitendo vilivyofanywa na askari wake dhidi ya walemavu.

Alisema madai ya watu wenye ulemavu yanalindwa na mikataba ya kimataifa pamoja na sheria za nchi, ikiwamo ibara ya tisa ya Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Watu wenye ulemavu ya mwaka 2006.

Alisema ibara hiyo inatoa haki kwa watu wenye ulemavu kuondolewa vikwazo vya kimiundombinu vinavyozuia uwezo wao wa kwenda watakako.

Alisema hata ibara ya 15 ya mikataba husika inazuia mateso na adhabu zinazokwenda kinyume na utu wa watu wenye ulemavu.

WATU 40"Tunaamini kwa dhati kuwa Jeshi la Polisi lingeweza kuwakamata na kuwazuia watu hao wenye ulemavu ambao hawakuwa na silaha yoyote, bila kutumia nguvu kubwa kama walivyofanya," alisema Shaibu.

"Jeshi la Polisi lilipaswa kuwaongoza walemavu hao hadi Manispaa ya Ilala kwenda kuwasilisha kilio chao."Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ilala, Salum Hamduni aliliambia Nipashe mwishoni mwa wiki iliyopita kuwa askari wake walilazimika kutumia mabomu kama njia ya kuwakamata watu hao.

Kamanda Hamduni alisema kutokana na kitendo hicho, polisi ilikuwa ikiwashikilia watu 40 akiwamo mwanamke mmoja.

Kamanda Hamduni alisema baada ya polisi kufika eneo hilo na kutoa amri mara tatu ya kuwataka kutawanyika, walemavu walikaidi.

Alisela ukaidi huo uliwaacha polisi wakiwa hawana njia nyingine zaidi ya kutumia mabomu ya machozi.Alisema nguvu hiyo ya kutumia mabomu ilikuwa na lengo la kurahisisha ukamataji wa watu hao waliokaidi amri ya polisi kutawanyika

Watetezi watatu kulitetea Gazeti la Mawio

BARAZA la Habari (MCT), Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC) na Umoja wa Vilabu vya Habari Tanzania (UTPC) vinakusudia kufungua kesi kwenye mahakama kupinga uamuzi wa serikali wa kulifunga gazeti la Mawio.

Serikali kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ilitangaza kulifunga gazeti hilo kwa miezi 24 kuanzia Alhamisi iliyopita, kwa kuchapisha taarifa zinazowahusisha marais wastaafu Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete kwenye sakata la mikataba mibovu ya madini.

Wakizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, wadau hao walisema hawajaridhika na hatua zilizochukuliwa na serikali katika kulifunga gazeti hilo kwa sababu ni kinyume cha mabadiliko ya Sheria ya Huduma ya Habari ya mwaka 2016.

Kaimu Katibu Mtendaji wa MCT, Pili Mtambalike, alisema kimsingi sheria hiyo haimpi waziri mamlaka ya kutoa adhabu kama aliyoitoa dhidi ya gazeti hilo.

Alisema hatua iliyochukuliwa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe, inalenga kuvinyima uhuru vyombo vya habari nchini.

Mtambalike alisema ni vema serikali kupitia Waziri Mwakyembe ikakaa chini na kutafakari upya na pia kufanya mazungumzo na uongozi wa gazeti hilo ili kutengua adhabu aliyoitoa.

"Serikali itengue uamuzi wake wa kulifungia gazeti la Mawio kwani unaenda kinyume cha Katiba pamoja na Sheria ya Huduma ya Habari ya mwaka 2016 kwa kuwa haimpi waziri mamlaka ya kutoa adhabu kama hiyo," alisema.Alisema zaidi: "Kwa sababu hakuna sehemu ya kupeleka rufani dhidi ya uamuzi wa waziri katika Sheria ya Huduma za Habari, endapo hakutakuwa na mazungumzo kati ya gazeti husika na waziri, sisi tutakwenda mahakamani kwa kushirikiano na Mawio kuonyesha haki zilizokiukwa juu ya hatua hiyo.

"Ikumbukwe kwamba vyombo vya habari, yakiwamo magazeti, hufanya shughuli zao kwa mujibu wa sheria na Katiba inasema wazi chini ya ibara ya 18 kwamba Watanzania wote wana haki ya kutafuta, kupokea na kutoa habari na maoni kwa njia yoyote, hivyo kwa mujibu wa sheria na vipengele hivyo vya Katiba, serikali inapaswa kuondoa marufuku yake dhidi ya gazeti la Mawio."

Naye Mkurugenzi wa THRDC, Onesmo Olengurumwa, alisema sehemu ya sheria ambayo waziri alitumia kulifunga gazeti hilo haina uhusiano na sehemu ambayo imewekwa kosa.