Kegera Sugar hawaelewi lolote kuhusiana na mshambuliaji Mbaraka Yusuf, wanasema ni mali yao.
Msisitizo wa Kegera Sugar wanasema wanataka walipwe shilingi milioni 150 ili imuachie mshambuliaji huyo kwenda Azam FC ambako tayari amesaini.
Hatua hiyo imekuja siku chache tangu Meneja wa Kagera, Mohammed Hussein kupiga hodi kwenye Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), akidai mshambuliaji huyo amesajiliwa kimakosa.
Mbaraka alisaini mkataba wa kuichezea Azam hivi karibuni kwa dau la zaidi ya shilingi milioni 40 akiwa kwenye kambi ya Taifa Stars.
Kwa mujibu wa taarifa ambazo Championi Ijumaa limezipata kutoka ndani ya uongozi wa Kagera, mshambuliaji huyo aliingia makubaliano ya kusaini mkataba wa miaka miwili akiwa bado amebakiza mwaka mmoja.
Mtoa taarifa huyo alisema uongozi wa Kagera umekubali kumuachia mshambuliaji huyo kwa makubaliano ya kulipwa shilingi milioni 150 ambazo wanazihitaji wao.
Aliongeza kuwa, kama Azam hawatakubali kutoa fedha hizo, basi suala hilo litafika mbali ikiwemo Fifa kutokana na timu hiyo kumsainisha mchezaji akiwa ana mkataba bado wa miaka miwili.
Alipotafutwa Meneja wa Kagera, Mohammed Hussein kuzungumzia hilo, alikiri mchezaji huyo kuwa na mkataba na Kagera na kusema wameshapeleka malalamiko yao kwa TFF juu ya kitendo hicho.
SOURCE: CHAMPIONI
Friday, 16 June 2017
Home »
» Kagera Sugar yaibua mapya kuhusu mshambuliaji Mbaraka Yusuf
Kagera Sugar yaibua mapya kuhusu mshambuliaji Mbaraka Yusuf
Related Posts:
Nape amemjibu Makonda, Picha limeanza upyaaa Siku moja baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam kuhojiwa na kituo cha Star Tv kuhusu mambo kadha wa kadha likiwemo suala la uvamizi wa Clouds Media na kusema Hakupaswa kumuingilia kwakuwa wote ni watumishi... Basi Nape ame… Read More
Nyumba zateketea kwa moto Sengerema Sengerema. Nyumba za wavuvi ambazo idadi yake haijajulikana hadi sasa katika kisiwa cha uvuvi cha Nyamango Kata ya Bulyaheke halmashauri ya Buchosa wilayani hapa, zinateketea kwa moto ambapo chanzo chake hakijajul… Read More
Vijana wanne wambaka binti wa miaka 15 Watu watatu wanashikiliwa na jeshi la polisi huku mwingine mmoja akiendelea kutafutwa kwa tuhuma za kumbaka binti mmoja mwenye umri wa miaka 15 wilayani Ilemela, mkoani Mwanza.Akitoa taarifa hiyo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mw… Read More
Mtaji wa Soko la Hisa DSM waporomoka Ukubwa wa mtaji wa kampuni zilizoorodheshwa katika Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) umepungua kwa Shilingi Bilioni 380 kutoka Shilingi Trilioni 20.2 wiki iliyopita hadi Shilingi Trilioni 19.9 kwa wiki iliyoishia Mei 19 mw… Read More
Mbunge atinga bungeni na rundo la risiti Dodoma.Mbunge wa Viti maalum (Chadema), Rhoda Kunchela aliwasilisha bungeni furushi la risiti za mwenge wanazodaiwa kuchangishwa kwa nguvu, walimu na wafanyabiashara.Mbunge Kunchela aliomba kutoa hoja ili ijadiliwa na Bunge … Read More
0 comments:
Post a Comment