Msanii wa muziki wa Bongo Fleva na mmoja wa Watu wanaoaminika kuwa ni Mbabe kama siyo Mtemi na Ngumi Jiwe wa kutukuka Kalapina jana wakati akihojiwa na Kipindi cha XXL kinachorushwa na Clouds fm aliamua kutema nyongo / kuvunja ukimya juu ya Kitendo cha Msanii mwenzake na mshikaji wake Roma Mkatoliki Kutekwa.
Kalapina ambaye anasifika mno kwa Usela / Uhuni na ukorofi ambao kiuhalisia kweli anauweza alianza kwanza kwa kumpa pole Roma Mkatoliki kwa yote yaliyomkuta ila hakusita pia kumlaumu kidogo Roma kwa kumwambia kuwa asingekubali kirahisi rahisi kubebwa na kuingizwa katika Gari na Kutekwa.
Ifuatayo ni nukuu Kuntu kabisa kutoka kwa Kalapina ambayo nadhani ni ujumbe tosha kwa Wazee wa Ununio mkabala na Mahaba Beach ( Watekaji )
“ Nakuambia Mimi nina hamu sana hao Watekaji siku wakosee tu waje waniteke Mimi kisha wajue kuwa kuna Watu tumebarikiwa kwa Ukorofi na Ukorofi tunaujua. Mimi wakija kama 10 na kutaka kuniteka basi nakuhakikishia lazima wakati wanafanikiwa kuniingiza katika Gari lao na kuniteka basi tayari name huku nyuma nitakuwa nimeshawaua Watatu au Wanne huku waliobaki nikiwaachia maumivu ya Kutukuka kabisa. Mdogo wangu Roma ulilegea sana na siku nyingine usifanye hivyo ukiona Mtu anataka kukuteka au ana nia mbaya nawe usimcheleweshe na badala yake mpe Kipondo / Kipigo pale pale “ mwisho wa kumnukuu Kalapina.
Friday, 16 June 2017
Home »
» Kalapina awapa salamu hizi waliomteka Roma Mkatoliki
Kalapina awapa salamu hizi waliomteka Roma Mkatoliki
Related Posts:
Muuza ndizi wa miaka 94 aliyeporwa Indonesia achangiwa pesaHaki miliki ya pichaFACEBOOK: TOMMYREZA CHOKOLATOZImage captionKind-hearted Indonesians reacted to Mr Suratman's plight in a strong show of support Watu nchini Indonesia wameungana kumsaidia mzee mmoja muuza ndizi ambaye anas… Read More
Panama yakata uhusiano na Taiwan na kuipendelea ChinaHaki miliki ya pichaCHINA NEWS SERVICEImage captionMawaziri wa Panama na Taiwan Panama imekata uhusiano wake wa muda mrefu na Taiwana na badala yake imeboresha uhusiano na China Serikalia ya Panama ilisema inatambua kuwa kun… Read More
Kiongozi wa upinzani Urusi atupwa jela kwa kuandaa maandamanoHaki miliki ya pichaAFP/GETTY IMAGESImage captionAlexei Navalny (kulia) ana nia ya kugombea urais mwaka ujao Kiongozi wa upinzani nchini Urusi Alexei Navalny amehukumia kifungo cha siku 30 jela kwa kukiuka sheria baada ya kua… Read More
Wakimbizi waugua kambini nchini IraqiHaki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionMaelfu ya watu wameukimbia mji wa Mosul baada ya kutokea mapigano ya kudhibiti mji huo Mamia ya watu wameugua na mtoto mmoja amepoteza maisha kwa kile kinachoelezwa kutokana na kul… Read More
Rais wa zamani wa Panama Ricardo Martinelli akamatwa MarekaniHaki miliki ya pichaREUTERSImage captionRicardo Martinelli anakana madai dhidi yake Rais wa zamani wa Panama Ricardo Martinelli amakamatwa katika jimbo la Florida nchini Marekani. Kikosi cha kudumisha sheria nchini Marekani … Read More
0 comments:
Post a Comment