MWIM-BAJI wa Mu-ziki wa Injili, Emmanuel Mbasha ameibuka na kusema kuwa amekubaliana na yote kwa aliyekuwa mkewe, Flora Mbasha ili kuepuka yaliyompata mzazi mwenzake na Zari, Ivan Ssemwanga wa Uganda ya kufariki dunia kwa shambulio la moyo.
Akipiga stori na Over Ze Weekend baada ya habari kuzagaa kwamba ana msongo wa mawazo unaosababishwa na aliyekuwa mkewe, Flora ambaye kwa sasa ni mke wa mtu, alikanusha vikali akisema yupo sawa na hawezi kuwa hivyo kwa kuwa amekubaliana na kila kilichotokea.
“Sitaki kupata tatizo la moyo na tangu mwanzo hata kabla hatujaachana kwa talaka mahakamani mawazo mabaya yalikuwa yakinijia nikayakataa kwa sababu ningeyasikiliza ningejikuta nikiziharibu ndoto zote za maisha yangu, nilishayakubali yote, nimeshazoea hiyo hali” alisema Mbasha.
Aliendelea kueleza kuwa sababu za kumweka Flora kwenye ukurasa wake wa Instagram siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwake aliyokuwa akiadhimisha Juni Mosi, mwaka huu na kumtakia mema ni kutokana na upendo tu kwani siku hiyo huwa inamkumbusha mengi waliyokuwa wakiyafanya.
“Nakumbuka kila tarehe moja ya mwezi wa sita kila mwaka tulivyokuwa tunaifurahia, namnunulia zawadi tunafanya pati kidogo nyumbani au sehemu yoyote,.
“Kuposti kwangu huko nimeshangaa watu maneno yamewatoka sana kwa kweli, niliposti kiroho safi tu na kwa upendo maana nilishayakubali matokeo, sina msongo wa mawazo maana najua ni hatari naweza nikapoteza uhai kama ilivyotokea kwa mume wa Zari, Ivan nikashindwa kutimiza ndoto zangu za kuwa mfanyabiashara mkubwa na mtumishi wa Mungu mku-bwa sana duniani,” alisema.
source:muungwana
Monday, 5 June 2017
Home »
» Mbasha ahofia kupata shambulio la moyo.
Mbasha ahofia kupata shambulio la moyo.
Related Posts:
PICHA: Kwa mara ya kwanza Rayvanny amempost mtoto wake na Ujumbe mzito Mwimbaji staa wa Bongofleva kutoka WCB Rayvanny leo May 31, 2017 kupitia account yake ya Instagram kwa mara ya kwanza amepost picha ya mtoto wake Jaydan ikiwa ni kumtambulisha kwa mashabiki wake. Rayvanny aliandika… Read More
Daktari wa upasuaji matiti afungwa jela miaka 15 Daktari wa upasuajia wa matiti Ian Paterson amefungwa jela miaka 15 kwa kufanya upasuaji usio muhimu. Paterson, mwenye umri wa miaka 59, aliwafanyia upasuaji wanawake tisa na mwanamume mmoja baada ya kuwadanganya k… Read More
Imevujaa!! Kumbe John Bocco alikuwa anahitajika Azam Golikipa namba moja wa Azam FC Aishi Manula amesema, John Bocco ‘Adebayor’ bado alikuwa anahitajika ndani ya kikosi cha Azam. Manula amesema, licha ya timu yake kusajili wachezaji wengi wa kigeni miaka ya hivi karibuni … Read More
Kipa Mcameroon aomba Kibarua Yanga KIPA Youthe Rostand amewaambia viongozi wa Yanga SC waache kumuogopa na wamuite mezani wazungumze kama kweli wana nia ya kumsajili.Kumekuwa na tetesi za muda mrefu kwamba kipa huyo Mcameroon ambaye timu yake iliyomleta n… Read More
HATIMAYE:Niko tayari kuondoka Barcelona- Iniesta Nohodha wa Barcelona, Andres Iniesta bado ana ndoto za kuzeekea kwenye Liga ya La Liga, huku akisema kwamba iwapo atatakiwa kuondoka yupo tayari kufanya hivyo. Iniesta mwenye miaka 33 mkataba wake unamalizika katikati… Read More
0 comments:
Post a Comment