Home »
» Afc Leopards uso kwa uso na Gor Mahia kwenye fainali ya Sportpesa Super Cup
Washindi wa nusu fainali za SportPesa Super Cup zilizofanyika Juni 08, 2017 Jijini Dar es Salaam, wanatarajiwa kukutana uso kwa uso kwenye mechi ya fainali ya kuwania kombe la michuano ya SportPesa Super Cup siku ya Jumapili ya tarehe 11, Juni 2017 itakayochezwa kwenye dimba la Uhuru jijini Dar es Salaam.Katika mechi za nusu fainali, AFC Leopards walipambana na mabingwa wa Ligi kuu Tanzania bara, Klabu ya Yanga na kuwang’oa kwa mikwaju ya penati 4-2 huku Gor Mahia kwa upande wao wakiifungasha virago timu ya Nakuru All Stars FC kufuatia ushindi wa magoli 2-0 ambayo yalitiwa kimiani na mshambuliaji Medie Kagere na George Odhiambo. Timu za Yanga na Nakuru All Stars FC ambazo ziling’olewa kwenye hatua ya nusu fainali, zilikabidhiwa medali za shaba na kiasi cha dola za kimarekani 5000 wakati wenzao (Gor Mahia na AFC Leopards) ambao wamefuzu kucheza fainali wakiwania kiasi cha dola za kimarekani 30,000.Akizungumzia mshindano ya SportPesa Super Cup kwa ujumla, Mkurungezi wa Utawala na Utekelezaji SportPesa Tanzania Ndugu Abbas Tarimba alisema; “Michuano ilikuwa migumu ingawa timu zetu za Tanzania zimeaga katika hatua za awali lakini ni nafasi nzuri kwetu kama Tanzania kujipanga vizuri zaidi ili kuboresha sekta ya michezo na kufanya timu zetu kushika nafasi za juu maana kwa sasa tumeweza kutambua changamoto mbalimbali na jinsi ya kuzikabili.SportPesa ni kampuni nguli ya michezo ya kubashiri inayojulikana kimataifa yenye makao yake makuu nchini Kenya ambayo imeanza rasmi shughuli zake nchini Tanzania Mei 9 mwaka huu na mpaka sasa imeshaingia makubaliano rasmi ya udhamini na vilabu vya Simba, Yanga na Singida United ikiwa imejidhatiti katika kuinua ba kuendeleza sekta ya michezo nchini.
source:muungwana
Related Posts:
Mwanahabari mfichuzi wa mihadarati auwawa Mexico
Mwaandishi habari aliyeshinda matuzo mengi kuhusiana na taarifa zake nyingi ya ufichuzi wa shughuli za makundi, yanayojihusisha na ulanguzi wa dawa za kulevya nchini Mexico, ameuwawa.
Javier Valdez, aliuwawa na watu wenye … Read More
Upinzani Kenya watishia kususia uchaguzi mkuu
Mzozo mpya umeibuka kati ya tume huru ya uchaguzi nchini Kenya, na vinara wa mrengo wa upinzani wa NASA kuhusu utangazaji wa matokeo rasmi ya kura za Urais.
IEBC imeijibu mrengo wa upinzani wa Nasa kufuatia vitisho vyake v… Read More
'The Rock' kuwania urais Marekani
Aliyekuwa nyota wa mchezo wa miereka Marekani Dwayne Johnson maarufu 'The Rock' anataka kuwania urais nchini humo.
Katika mahojiano na jarida la GQ, nyota huyo wa uigizaji anasema kuwa amelifikiria sana wazo hilo.
Anasema… Read More
Milio ya risasi yatanda miji mikuu Ivory Coast
Ufyatulianaji mkali wa risasi umezuka katika miji miwili mikuu nchini Ivory Coast, wanajeshi wakiendelea kuasi kwa siku ya nne mtawalia.
Wanajeshi hao waliogoma wamefunga barabara nje ya kambi za jeshi katika mtaa wa kifah… Read More
Mahabusu aomba adhabu ya kifo cha kumiminiwa risasi Marekani
Mahabusu anayesubiri kunyongwa katika jela moja katika jimbo la Georgia nchini Marekani amewasilisha ombi la kuuawa kwa kuumiminiwa risasi kwa sababu kifo cha kuuawa kwa kudungwa sindano kina uchungu mno.
JW Leford amekuwa… Read More
0 comments:
Post a Comment