Home »
» Afc Leopards uso kwa uso na Gor Mahia kwenye fainali ya Sportpesa Super Cup
Washindi wa nusu fainali za SportPesa Super Cup zilizofanyika Juni 08, 2017 Jijini Dar es Salaam, wanatarajiwa kukutana uso kwa uso kwenye mechi ya fainali ya kuwania kombe la michuano ya SportPesa Super Cup siku ya Jumapili ya tarehe 11, Juni 2017 itakayochezwa kwenye dimba la Uhuru jijini Dar es Salaam.Katika mechi za nusu fainali, AFC Leopards walipambana na mabingwa wa Ligi kuu Tanzania bara, Klabu ya Yanga na kuwang’oa kwa mikwaju ya penati 4-2 huku Gor Mahia kwa upande wao wakiifungasha virago timu ya Nakuru All Stars FC kufuatia ushindi wa magoli 2-0 ambayo yalitiwa kimiani na mshambuliaji Medie Kagere na George Odhiambo. Timu za Yanga na Nakuru All Stars FC ambazo ziling’olewa kwenye hatua ya nusu fainali, zilikabidhiwa medali za shaba na kiasi cha dola za kimarekani 5000 wakati wenzao (Gor Mahia na AFC Leopards) ambao wamefuzu kucheza fainali wakiwania kiasi cha dola za kimarekani 30,000.Akizungumzia mshindano ya SportPesa Super Cup kwa ujumla, Mkurungezi wa Utawala na Utekelezaji SportPesa Tanzania Ndugu Abbas Tarimba alisema; “Michuano ilikuwa migumu ingawa timu zetu za Tanzania zimeaga katika hatua za awali lakini ni nafasi nzuri kwetu kama Tanzania kujipanga vizuri zaidi ili kuboresha sekta ya michezo na kufanya timu zetu kushika nafasi za juu maana kwa sasa tumeweza kutambua changamoto mbalimbali na jinsi ya kuzikabili.SportPesa ni kampuni nguli ya michezo ya kubashiri inayojulikana kimataifa yenye makao yake makuu nchini Kenya ambayo imeanza rasmi shughuli zake nchini Tanzania Mei 9 mwaka huu na mpaka sasa imeshaingia makubaliano rasmi ya udhamini na vilabu vya Simba, Yanga na Singida United ikiwa imejidhatiti katika kuinua ba kuendeleza sekta ya michezo nchini.
source:muungwana
Related Posts:
Rais Magufuli amlilia Mwasisi wa Chadema
Rais John Magufuli amepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha mmoja wa waasisi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo, (Chadema) Phillemon Ndesamburo huku akimtaja marehemu kuwa alikuwa kiongozi mwenye hekima na aliyez… Read More
Mbunifu wa Android azindua simu mpya ya EssentialHaki miliki ya pichaESSENTIAL PHONEImage captionSinu ya Essential hutumia mfumo wa Android na imeanza kuuzwa nchini Marekani kwa dola $699.
Andy Rubin, ambaye ni miongoni mwa watu waliobuni programu ya software Android ya Goo… Read More
Vifaru vya Urusi vinavyotia wasiwasi mataifa ya Nato barani Ulaya
Haki miliki ya pichaAFPImage captionArmata ni kifaru cha kisasa ambacho kinachukua nafasi ya vifaru vya enzi za muungano wa Usovieti
Urusi imeunda vifaru vipya ambavyo vimeifanya Norway kuanza kufikiria upya mfumo wake wa k… Read More
Ndugai amkumbuka kwa majonzi Ndesamburo
Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema anamkumbuka marehemu Phillemon Ndesamburo aliyekuwa mbunge wa Moshi Mjini (Chadema) kwa uchapakazi wake na mapenzi yake makubwa kwa wapiga kura wake.“Nimepokea kwa masikitiko t… Read More
Kambi ya Upinzani Bungeni uvunjwe
MBUNGE wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbles Lema (Chadema), amelitaka Bunge kuvunja Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kutokana na maoni ya kambi hiyo kutosikilizwa.Lema amedai kuna kuchujwa kwa maneno yanayochangiwa na wabunge w… Read More
0 comments:
Post a Comment