Saturday, 10 June 2017

Mkude: Kwa dau hili nipo tayari kujiunga na Yanga

UNAWEZA ukashituka kidogo ila habari ndiyo hivyo anaweza kusaini Yanga kwa milioni 70 tu, Mkude ambaye mara kadhaa amewahi kuhusishwa kuwaniwa na Yanga ameamua kuweka wazi kuwa atatua ndani ya kikosi cha Yanga kwa ajili ya kukitumikia msimu ujao kwa kutoa sharti moja kubwa ambalo ni klabu hiyo kumpatia shilingi milioni 70.

Mkude kwa sasa yuko huru kujiunga na timu yoyote baada ya mkataba wake na Simba kudaiwa kumalizika hivi karibuni, ikiwa ni mwisho wa mkataba wake wa shilingi milioni 60 aliosaini kuitumikia Simba miaka miwili iliyopita.

Akizungumza kiungo huyo, amesema atakuwa tayari kusaini mkataba na klabu ya Yanga kwa dau la kuanzia milioni 70 kwenda juu kutokana na kiwango alichonacho kwa sasa. Simba wamempa ofa ya milioni 40-50 ila yeye amekataa kwa kigezo kwamba mkataba unaoisha walimpa milioni 60 kwa sasa lazima dau lipande.

“Kwa upande wangu nipo tayari kutua Yanga kwa dau la kuanzia milioni 70 na kuendelea hadi shilingi milioni 150 na siwezi kusaini chini ya hapo, nipo tayari kutua katika timu yoyote kwa kiasi ambacho tutakubaliana kwa kuwa kiwango changu kipo vizuri.

Nahodha huyo wa Simba amesema lolote linaweza kutokea kuanzia sasa: “Tusubiri kila kitu kitakuwa wazi muda si mrefu na wadau watajua nitasaini wapi kwa ajili ya msimu ujao, wasiwe na hofu.”

Related Posts:

  • MWIGULU ATETA NA POLISI MAUAJI KIBITI WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba, amefanya ziara ya kushtukiza wilayani Kibiti mkoani Pwani na kuteta kwa faragha na askari wa operesheni maalumu ya kuwasaka wauaji. Alisema  mauaji sasa yametosha … Read More
  • Tamko la mradi wa bomba la mafuta ghafi lasainiwa Rais Dkt John Pombe Magufuli na Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Museveni wakitia saini tamko la pamoja la kukamilika kwa majadiliano na vipengele vya mkataba wa utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima… Read More
  • Trump kuzuru Israel chini ya ulinzi mkali Rais wa Marekani Donald Trump anazuru Israel na Maeneo ya Wapalestina leo, akiendelea na ziara yake ya kikazi katika maeneo ya Mashariki ya Kati. Atafika maeneo hayo akitokea Saudi Arabia, mshirika muhimu wa Marekani, amba… Read More
  • Mwanamke akata uume wa kiongozi wa dini India   Mwanamke mmoja wa umri wa miaka 23 nchini India amekata uume ya wa kiongozi mmoja wa dini kwenye jimbo lililo kusini mwa nchi la Kerala, akidai kuwa alimbaka kwa miaka kadha. Polisi wanasema kuwa kiongozi huyo wa d… Read More
  • Libya yakabiliwa na vita vya ndani Taarifa kutoka nchini Libya zinaelez kwamba jeshi liloljitangaza kuwa la taifa hilo, ambalo linaunga mkono mamlaka yenye makao yake katika mji wa mashariki wa Tobruk,limefanya mashambuliuzi kadhaa ya anga dhidi ya vikosi pi… Read More

0 comments:

Post a Comment