Wednesday, 14 June 2017

Aliyekuwa gavana wa Rio de Janeiro afungwa miaka 14 kwa ufisadi

Rio de Janeiro's Governor Sergio Cabral smiles as he visits the site of the construction of a new tunnel to the Transolimpica expressway in Rio de Janeiro, Brazil, on November 08, 2013.Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionSergio Cabral alihudumu mihula miwili kama gavana wa Rio kuanzia mwaka 2007 hadi 2014.
Aliyekuwa gavana wa jimbo la Rio de Janeiro nchini Brazil, amehukumiwa kifungo cha miaka 14 gerezani kwa ufisadi na ulanguzi wa pesa.
Sergio Cabral alihudumu mihula miwili kama gavana wa Rio kuanzia mwaka 2007 hadi 2014.
Analaumiwa kwa kupokea hongo kutoka kwa makampuni ya ujenza ili kuyapa zabuni za pesa nyingi.
Jaji Sergio Moro, alisema kuwa hakukuwa na ushahidi wa kutosha kumshtaki mkewe, Adriana Ancelmo
Cabral alikamatwa mwezi Novemba kama sehemu ya oparesheni iliyofahamka kama Car Wash, iliyohusu uchunguzi mkubwa, ambayo ilisababisha kukamatwa kwa wanasiasa mashuhuri na wafanyibiashara nchini Brazil.
Cabral ni mwanachama wa cham cha Democratic Movement Party, cha rais Michel Temer ambaye pia anafanyiw uchunguzi unaohusu ufisadi.
Jaji Moro alisema kuwa gavana huyo wa zamani alikuwa amechukua dola 813,000.
Hata hivyo jaji amesema kuwa pesa hizo hazijapatikana na huenda Cabral alizihamisha kabla ya akaunti zake kufungwa.

Related Posts:

  • Diamond afunguka mchango wa Wema Sepetu kwenye ‘Chibu Perfume’. Msanii wa muziki, Diamond platnumz amefunguka kuuzungumzia mchango wa malkia wa filamu, Wema Sepetu kwenye perfume yake ya ‘Chibu Perfume’.Diamond amekiambia kipindi cha XXL cha Clouds FM kuwa, yeye na Wema wanakutana na ku… Read More
  • Hawa wote motoni KIMENUKA! RAIS John Magufuli ameagiza kukamatwa na kuhojiwa kwa waliokuwa mawaziri, kamishina wa madini, wanasheria wakuu (AG) na waliokuwa watumishi katika idara mbalimbali za serikali zilizoruhusu usafirishaji wa madini … Read More
  • Wananchi watema cheche, wataka Marais wastaafu wachunguzwe Mikoani. Wananchi katika maeneo mbalimbali nchini wamemshauri Rais John Magufuli kufanya mabadiliko ya Katiba na kuhakikisha diplomasia ya uchumi haivurugiki kutokana na sakata la mchanga wa madini (makinikia).Wakitoa maoni… Read More
  • Mwanamke ajichinja kwa chupa MWANAMKE aliyefahamika kwa jina la Saada Elias (24) mkazi wa Mtaa wa Mabambase katika Manispaa ya Shinyanga alifariki dunia kwa kujikata koromeo kwa chupa ya soda. Mwanamke huyo alijiua kwa chupa ikiwa ni muda mfupi baa… Read More
  • Korea Kaskazini yamwachilia huru MmarekaniHaki miliki ya pichaREUTERSImage captionWazazi wa Otto Warmbier waliohifia usalama wa mwana wao kufuatia kuongezeka kwa uhsama kati ya Marekani na Korea Kaskazini Korea Kaskazini imemwachilia huru mwanafunzi Mmarekani Otto Wa… Read More

0 comments:

Post a Comment