Wednesday, 14 June 2017

Mzee Akilimali ataka kumpiku Manji, atangaza kuwania uenyekiti Yanga

AKILIMALI

Katibu Mkuu wa Baraza la Wazee wa Yanga, Ibrahimu Akilimali ametangaza kuwania nafasi ya uenyekiti wa klabu ya hiyo iliyoachwa wazi hivi karibuni na aliyekuwa mwenyekiti wa klabu hiyo, Yusuf Manji.

Hivi karibuni Manji alitangaza kujiuzulu kwenye nafasi yake hiyo ili aweze kupumzika kutokana na matatizo mbalimbali aliyokumbana nayo siku chache zilizopotia.

Lakini pia maamuzi hayo ya Manji  yalikuja ikiwa ni muda mfupi tu umepita tangu alipotangaza kutaka kuikodi timu hiyo kwa muda wa miaka 10, lakini akakukumbana na changamoto kibao kutoka kwa baadhi ya wanachama wa klabu hiyo na kuamua kusitisha mpango wake huo.

Akilimali alisema anaamini amefikia uamuzi huo ili aweze kuleta mabadiliko makubwa ya ndani ya klabu hiyo kuanzia pale Manji alipoishia.

Alisema licha ya kutokuwa bilionea kama ilivyokuwa kwa Manji lakini anaamini kwa kutumia utajiri wake wa hekima na busara alizonazo ataiongoza klabu hiyo kwa mafanikio makubwa, kwa hiyo amewataka wanachama kutulia.

“Manji keshaondoka Yanga akapumzike kutokana na matatizo yaliyompata hivi karibuni kwa hiyo siyo vizuri kuanza kuumiza vichwa kuwa mambo yatakuaje bila ya yeye.

“Yanga ni timu kubwa, jina lake na nembo yake tu chanzo kikubwa cha kuingizia mapato endapo atapatikana kiongozi mwenye uchungu na maendeleo ya Yanga na asiwe mpigaji.


“Kwa hiyo, katika uchaguzi ujao ambao utafanyika ili kuziba nafasi iliyoachwa na Manji, nitagombea nafasi hiyo kwani uwezo wa kuipa Yanga mafanikio ninao,” alisema Akilimali.

Related Posts:

  • Wabunge Wakataa Kutoa Rambirambi Nyingine. Mbunge wa Geita Vijini Joseph Msukuma (CCM) ameliomba Bunge kuazimia kutoa rambirambi kutokana na vifo vya watoto 10 vilivyotokea jimboni kwake vilivyosababishwa na mvua zilizonyesha mwishoni mwa wiki.Ombi hilo limesababish… Read More
  • Ratiba ya Sportpesa Super Cup Sport Pesa Cup 5/6 Singida united Vs FC leopardYanga Vs Tusker fc6/5 Simba Vs Nakuru All StarJang`ombe boys vs Gor mahiaNusu fainali tarehe 8Bingwa wa mechi kati ya Singida united vs AFC leopard atacheza na bingwa kati ya… Read More
  • Nikki wa Pili ampongeza Rais Magufuli Msanii wa Nikki wa Pili, amempongeza Rais Magufuli kwa kitendo alichokifanya leo cha kumtumbua Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Mwijarubi Muhongo na kumwambia Mungu amsimamie katika kupambana na ufisadi.Niki ameto… Read More
  • Nape amposti Rais Magufuli na kuandika Ujumbe huu Mbunge wa Mtama mapema leo hii baada ya Rais John Magufuli kumfuta kazi Waziri wa Nishati na Madini Professa Sospita Muhongo kutokana na wizara yake kutowajibika na kashafa ya Makontena ya Mchanga wa w Dhahabu. Rais Mag… Read More
  • Trump asababisha Al Jazeera kufungiwa Saudi Arabia Saudi Arabia imeifungia mitandao ya Al Jazeera na Magazeti ya Qatar baada ya Rais wa Qatar Tamim Bin Hamad Al-Thani kusema anaishangaa Saudi Arabia kumkaribisha Rais wa Marekani Donald Trump kauli iliyopingwa na Mfalme wa … Read More

0 comments:

Post a Comment