Dodoma. Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Simbachawene amewaonya wakuu wa mikoa na wilaya kutotumia vibaya madaraka yao ya kukamata watu walio kwenye himaya zao.
Ametoa onyo hilo leo (Ijumaa) alipojibu maswali ya wabunge waliotaka kufanyika marekebisho ya sheria inayowapa mamlaka wakuu hao ya kuwakamata na kuwaweka ndani wananchi wanaowatuhumu kwa lolote.
Licha ya kubainisha kwamba sheria hiyo haina tatizo, waziri amesisitiza: "Ukamataji unatakiwa ufanywe kwa mtu aliyetenda kosa la jinai au anayehatarisha usalama. Isiwe kwa show-off tu. Na mhusika anatakiwa kufikishwa mahakamani mara moja, asishikiliwe tu."
Amesisitiza kwamba wakuu hao ni wawakilishi wa Serikali kwenye maeneo yao, hivyo hawatakiwi kutumia vibaya madaraka waliyokasimiwa.
Katika siku za karibuni wakuu wa mikoa na wilaya wamekuwa wakilalamikiwa kuwaweka watu kizuizini pasipo kuwa na sababu za msingi, miongoni mwao wakiwamo waandishi wa habari.
Friday, 16 June 2017
Home »
» Waziri wa Tamisemi atoa onyo hili kwa wakuu wa mikoa na wilaya
Waziri wa Tamisemi atoa onyo hili kwa wakuu wa mikoa na wilaya
Related Posts:
ACACIA WAPINGA UCHUNGUZI WA KAMATI VITA kubwa. Ndivyo unavyoweza kusema baada ya Rais Dk. John Magufuli kuanza kuchukua hatua kali dhidi ya usafirishaji wa mchanga unaodaiwa kuwa na dhahabu. Baada ya hatua hiyo ya Rais Magufuli, kumeanza kuibuka mambo kadh… Read More
TAMKO LA SERIKALI: WANAJESHI HAWANA HAKI YA KUTESA RAIA SERIKALI imesema hakuna sheria yoyote inayowapa haki wanajeshi kutesa raia au kuvunja sheria. Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Hussein Mwinyi, alitoa kauli hiyo wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu… Read More
LOWASSA, LIPUMBA WAGONGANA MSIBANI WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Lowassa na Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) anayetambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Profesa Ibrahim Lipumba wamekutana ana kwa ana kwenye mazishi ya mwanasiasa mkongwe na Mey… Read More
Hatimaye simu mpya za Nokia 3310 zaingia madukani Simu hizo mpya za Nokia 3310 zitakaa muda mrefu na chaji kuliko simu asiliSimu za Nokia 3310 zimeanza kuuzwa tena madukani, takriban miaka 17 baada ya simu hizo kuanza kuuzwa mara ya kwanza.Simu za sasa zina kamera ya… Read More
LUKUVI ATANGAZA KITANZI KWA MADALALI WA ARDHI tarajia kuandaa sheria itakayowabana madalali katika sekta ya ardhi. Amesema lengo la sheria hiyo ni kuwabana madalali hao ambao wamekuwa wakiuza ardhi katika siku za mapumziko kutokana na sababu wanazozijua wao. Lukuv… Read More
0 comments:
Post a Comment