Tuesday 13 June 2017

Kiongozi wa upinzani Urusi atupwa jela kwa kuandaa maandamano

Alexei Navalny (right) speaks after a hearing in a court in Moscow. Photo: 12 June 2017Haki miliki ya pichaAFP/GETTY IMAGES
Image captionAlexei Navalny (kulia) ana nia ya kugombea urais mwaka ujao
Kiongozi wa upinzani nchini Urusi Alexei Navalny amehukumia kifungo cha siku 30 jela kwa kukiuka sheria baada ya kuandaa maandamano
Alikamatwa nyumbani kwake mjini Moscow siku ya Jumatatu kabla ya kufanyika kwa maandamano ya kupinga ufisadi nchini Urusi.
Mamia ya watu walikamhwa wakati wa maandamano hayo yaliyofanyika kote nchini.
Polisi wa kupamba na maandamano walikuwa wakiwakamata waandamanaji kutoka kwa umati, kwa mujibu wa mwandjshi wa BBC aliyekuweko.
Russian police officers detain a young woman participating in an unauthorised opposition rally in centre of Saint Petersburg on June 12, 2017Haki miliki ya pichaAFP
Image captionVijana wakamatwa mjini St Petersburg
Mahakama ya Moscow iltangaza umuzi wake jana Jumatatu na kukataa wito wa mawakili wa Navalny kufuta kesi hiyo.
Kiongozi huyo wa upinzani mwenyr umri wa miaka 42 baadaye alithibitisha hukumu yake katika mtandao wa twitter.
Polisi mjini Moscow wanasema kuwa takriban watu 5000 walishiriki maandamano hayo mjini humo.
Police detain a participant of an unauthorised opposition rally in Tverskaya Street in central Moscow, Russia, 12 June 2017Haki miliki ya pichaEPA
Image captionMwandamanaji akikamatwa mjini Moscow




0 comments:

Post a Comment