Monday, 5 June 2017

Walinzi wa Netanyahu na wa rais wa Togo wazozana Liberia

Netanyahu alitaja kuwepo kwake kama wa kihistoriaHaki miliki ya pichaEPA
Image captionNetanyahu alitaja kuwepo kwake kama wa kihistoria
Mkutano kati ya waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu na rais wa Togo Faure Gnassingbé, ulilazimika kupangwa upya baada ya mvutano uliotokea kati ya walinzi wa viongozi hao.
Mtandao wa Times of Israel ulisema kuwa mvutano huo ulitokea wakati walinzi wa Israel walikataa kuwaruhusu walinzi wa Togo kuingia mkutano ambapo viongozi hao walikuwa wakutane mjini Monrovia nchini Liberia.
Bwana Gnassingbe na Netanyahu walikuwa wanahudhuria mkutano wa Jumuiya ya nchi za Afrika magharibi (Ecowas).
Hata hivyo bwana Netanyahu alitaja kuwepo kwake kama wa kihistoria
"Hii ndiyo mara ya kwanza Ecowas kumualika kiongozi kutoka nje ya Afrika kuwahutubia. Ninatoa shukran zangu nyingi. Israel imerudi Afrika kwa njia kubwa, Netanyahu alinukuliwa akisema na gazeti la Jurusalem Post.

Related Posts:

  • Vigogo wawili Waliotajwa Ripoti ya Makinikia wamwaga fedha Kanisani WABUNGE watatu, wakiwamo Andrew Chenge na William Ngeleja ambao Kamati ya pili ya Rais kuchunguza masuala ya kisheria na kiuchumi kuhusiana na makinikia Jumatatu iliyopita ilishauri wachunguzwe, jana walitoa mchango kwa k… Read More
  • Ajinyonga kisa ugumu wa maisha Kijana Paulo Ezekiel, amejinyonga kutokana na kile kinachodaiwa ugumu wa maisha.Paulo (17) alikuwa anaishi na wazazi wake Mtaa wa Mazinge Kata ya Ndembezi mjini Shinyanga, alifariki dunia juzi usiku kutokana na kudaiwa kuji… Read More
  • Mwanajeshi wa Korea Kaskazini ahamia K. Kusini kwa kuogelea Mwanajeshi mmoja wa Korea Kaskazini ametorokea Korea Kusini kupitia kuvuka mto Han kwa kuogelea ,ikiwa ni mara ya pili kwa raia wa taifa hilo kuhamia kwa majirani zao.Mkuu wa Jeshi nchini Korea Kusini amesema kuwa mwanajesh… Read More
  • Watetezi watatu kulitetea Gazeti la Mawio BARAZA la Habari (MCT), Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC) na Umoja wa Vilabu vya Habari Tanzania (UTPC) vinakusudia kufungua kesi kwenye mahakama kupinga uamuzi wa serikali wa kulifunga gazeti la Mawio. Se… Read More
  • Mawaziri wawili wabanwa CHAMA cha ACT-Wazalendo kimelaumu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba na Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama kufuatia kitendo cha Jeshi la Polisi kutumia nguvu kutawanya ma… Read More

0 comments:

Post a Comment