Mwanasheria Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Baptister Marco (54) amepandishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu mashtaka matatu ya kuishi na kufanya kazi nchini bila kuwa na kibali.
Mwendesha Mashtaka wa Uhamiaji, Novatus Mlay alimemsomea mashtaka hayo leo Jumatano kwa Hakimu Mkazi Mkuu, Victoria Nongwa.
Akisoma hati ya mashtaka, Mlay alidai kuwa Mei 19, 2017 huko Kinondoni katika ofisi ya uhamiaji, Marco akiwa raia wa Burundi alikutwa nchini bila kuwa na kibali cha kumuwezesha kuishi.
Marco katika shtaka la pili amedaiwa kuwa siku hiyo alikutwa akifanya kazi kama Mwanasheria Mkuu wa TBS bila ya kuwa na kibali kinachomruhusu kufanya kazi hapa nchini.
Katika shtaka la tatu, Mlay alidai kuwa, Julai 6 mwaka 2011 katika ofisi ya Uhamiaji ya Dar es Salaam iliyopo Wilaya ya Ilala, mshtakiwa huyo akiwa raia wa Burundi alitoa taarifa za uongo kuhusu maelezo yake binafsi wakati akijaza fomu ya kuomba hati ya kusafiria namba CT (5)(Ai).
Wakili Mlay alisema kitendo hicho cha kutoa taarifa za uongo kilimuwezesha Marco kupata hati ya kusafiria ya Tanzania yenye namba AB 474856 huku akijua kufanya hivyo ni kinyume cha sheria za nchi.
Baada ya kusomewa mashtaka hayo, alikana na upande wa mashtaka ulidai kuwa upelelezi bado haujakamilika.
Mshtakiwa alitakiwa kuwa na wadhamini wawili wanaoaminika ambao kila mmoja atasaini bondi ya Sh 20 milioni na alikamilisha. Kesi imeahirishwa hadi Juni 21, 2017 kwa ajili ya kutajwa.
Wednesday, 7 June 2017
Home »
» Mwanasheria Mkuu wa TBS Afikishwa Mahakamani
Mwanasheria Mkuu wa TBS Afikishwa Mahakamani
Related Posts:
ALIVYOAPISHWA RAIS WA CHUO KIKUU CHA AJUCO RAIS WA AJUCO NA MAKAMU WAKE Hatimaye ile siku iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu ni leo tarehe 1/7/2017 katika ukumbi wa NYERERE 0NE ,ambapo rais aliyeshinda kiti cha urais katka chuo kikuu cha AJUCO MR. SUNGURA amea… Read More
JIFUNZE HIKI: DOWNLOAD MOVIES NA MUSICS BURE YOUTUBE BILA KUWA NA DOWNLOADER YEYOTE JINSI YA KUDOWNLOAD VIDEO YEYOTE YOUTUBE BILA KUWA NA DOWNLOADER YEYEOTE 1) Go to www.youtube.com. Open the page of the video you want to download. 2) Add "ss" between the www. and the youtube.com section … Read More
Watu wenye silaha washambulia eneo la watalii MaliHaki miliki ya pichaREUTERSImage captionLe Campement Kangaba, eneo lililoshambuliwa Vyombo vya Usalama nchini Mali vinasema vimeokoa zaidi ya wageni thelathini kutoka katika kituo kimoja cha Utalii, kilichokuwa kikishambuliwa… Read More
Mbwa mwenye sura mbaya zaidi duniani atajwaHaki miliki ya pichaEPAImage captionMartha, ametajwa kuwa mbwa mwenye sura mbaya zaidi duniani. Martha, ametajwa kuwa mbwa mwenye sura mbaya zaidi duniani. Shindano la kila mwaka ambalo sasa liko katika mwaka wake wa 29 lili… Read More
SIKIA ALICHOKIONGEA RAIS MTEULE SUNGURA (AJUCSO )Jana tarehe 28/6/2017 Chuo kikuu kishiriki cha AJUCO ambacho ni Tawi la SAUT ulifanyika uchaguzi wa kuwapata wabunge na Rais watakao hudumu kwa kipindi cha mwaka mmoja. Wagombe wengi walijitokeza kuwania nafasi za ubunge laki… Read More
0 comments:
Post a Comment