Wednesday, 14 June 2017

Lissu Amtolea Uvivu JK kuhusu kusaini mikataba ya Madini

Mwanasheria Mkuu wa Chadema Tundu Lissu ameitaka Serikali kumjumuisha Rais Mstaafu kwenye tuhuma za Makontena ya Mchenga wa Dhahabu,

Akichangia bungeni katika hotuba ya bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2017/18, Lissu amesema kuwa wakati wa kusaini mikataba ya madini Kikwete alikuwa ni Waziri wa Maji, Nishati na Madini.

“Katika taarifa hii ya jana wamependekeza watu fulani fulani washtakiwe makamishna, mwanasheria mkuu, Chenge (Mbunge wa Bariadi Andrew), Ngeleja (Wiliam- Sengerema) jamani naombeni niwaambie kitu ili  wabunge muwe na maarifa,”amesema na kuongeza:

“Mtu wa kwanza kusaini mikataba na leseni za madini alikuwa ni Meja Jakaya Mrisho Kikwete, Agosti 5 mwaka 1994 alisaini leseni ya Bulyankulu inayopingwa leo hii wakati akiwa Waziri wa Maji, Nishati na Madini wakati huo hakuwa na kinga ya urais.”

Amesema wakati aliposaini leseni na mikataba hiyo alikuwa hana kinga kwa masuala ambayo aliyafanya.

“Rais (Kikwete) alisaini si ya Bulyankulu pekee ya Nzega, ya Geita hizo leseni zina saini ya Kikwete anaponaje kwa mapendekezo haya? Anaponaje kama kweli mnataka kuwashughulikia watu walioshiriki kwenye mambo haya?”amehoji.

“Mbona mnachagua chagua hizi? Leseni na hizi sheria tangu mwaka 1999 tumesema tatizo kubwa ni sheria.”

Amemtaka Spika wa Bunge, Job Ndugai kama anataka kukumbukwa wakati wa uongozi wake basi asikubali kupitisha miswada ya sheria kwa hati ya dharura.

Akijibu swali hilo, Ndugai amesema atairuhusu miswada hiyo ya madini na gesi iingie bungeni kwa hati ya dharura.

“Kwanza wanaoamua siyo mimi tu ni kamati ya uongozi ya Bunge, lakini kama itakuja kwa hati ya dharura hii (madini) itaruhusiwa kwasababu moja tu tunaibiwa sana.” amesema.

Related Posts:

  • LOWASSA, LIPUMBA WAGONGANA MSIBANI WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Lowassa na Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) anayetambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Profesa Ibrahim Lipumba wamekutana ana kwa ana kwenye mazishi ya mwanasiasa mkongwe na Mey… Read More
  • LUKUVI ATANGAZA KITANZI KWA MADALALI WA ARDHI tarajia kuandaa sheria itakayowabana madalali katika sekta ya ardhi. Amesema lengo la sheria hiyo ni kuwabana madalali hao ambao wamekuwa wakiuza ardhi katika siku za mapumziko kutokana na sababu wanazozijua wao. Lukuv… Read More
  • TAMKO LA SERIKALI: WANAJESHI HAWANA HAKI YA KUTESA RAIA SERIKALI imesema hakuna sheria yoyote inayowapa haki wanajeshi kutesa raia au kuvunja sheria. Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Hussein Mwinyi, alitoa kauli hiyo wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu… Read More
  • MADIWANI WANNE CCM WATUMBULIWA Na Ibrahim Yassin – KYELA CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mbeya kimewasimamisha uanachama madiwani wake wanne wilayani Kyela huku 14 wakipewa onyo kali kwa kuhusishwa na usaliti. Akizungumza   na gazeti hi… Read More
  • UKWELI KUHUSU SINDANO ZA UZAZI WA MPANGO WATU wengi leo hii hupenda kufanikiwa maishani. Wengi wakiwa na utajiri na wenzi bora wa maisha kitu kikubwa wanachokitamani ni kuzaa na kuwa na familia yenye furaha. Ili uwe na familia bora ni vyema pia kuzingatia mpango w… Read More

0 comments:

Post a Comment