Msanii wa Bongo Fleva, Jay Moe ameeleza changamoto alizokumbana nazo shule hadi kupelekea kutoa albamu ya Ulimwengu Ndio Mama, licha ya hiyo kuna vitu ambavyo anajivunia ikiwemo kusoma shule moja na Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Joseph Kabila.
Rapper huyo amesema kutokana na kukulia maisha ya kishua hadi unafika wakati ambao anaenda boarding school alikuwa hajui kama kuna nyumba za udongo nchini zaidi ya kuziona kwenye movie za Vietnam.
Ameeleza kuwa wakati anaenda Mbeya kuanza form one mwaka 1993 ndipo alianza kuona nyumba za udongo kitu kilichomfanya kuanza kulia lakini baba yake na ndugu zake walipomueleza kuwa amekua hivyo hana budi kuachana na mambo ya kitoto na kupambana.
“Siku ya kwanza nilipofika Irambo (secondary) jamaa wameniibia begi la mamisosi, kwa hiyo kule ndipo nilipojifunza maisha kiasi kwamba nilipofika form three mzee wangu alitaka anihamishie Dar es Salaam lakini ikamwambi hapana mimi nabaki, nimeshazoea ingawa maisha ni magumu,” Jay Moe amekiambia kipindi cha The Play List cha Times FM.
“Kingine kinacho-inspire image mimi nimesoma na Joseph Kabila ambaye ni Rais wa kongo, nimesoma na Cesi, nimesoma na Clara ambao wote ni watoto wa mzee Kabila. Mimi nikiwa form two Jose ndio anamaliza form six na alikuwa kaka mkuu wa shule, kwa hiyo nilijifunza kama huna mama basi, kuna ulimwengu ambao utakufunza kama mama,” amesema Jay Moe.
Saturday, 10 June 2017
Home »
» Jay Moe: Mimi na Rais Kabila tumesoma shule moja
Jay Moe: Mimi na Rais Kabila tumesoma shule moja
Related Posts:
Jeneza la mwili wa Ndesamburo lazuiwa kupitishwa barabarani Moshi. Jeshi la Polisi mkoa wa Kipolisi wa Moshi limezuia utaratibu wa kutoa heshima za mwisho kwa kuutembeza katika barabara za viunga vya manispaa hiyo, mwili aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema, Kilimanjaro… Read More
Mnyika kula sahani moja na askari wa Bunge aliyemsukuma Mbunge wa Kibamba (Chadema), John Mnyika amesema atachukua hatua kwa kitendo cha kusukumwa kilichofanywa na askari wa Bunge mwishoni mwa wiki. Alisema atafanya hivyo mara baada ya kumaliza msiba wa mmoja wa waasisi wa c… Read More
PICHA: Jinsi Juventus walivyorejea kwao baada ya kipigo cha Real Madrid Baada ya kupoteza kwa kufungwa kwa mabao 4-1 dhidi ya Real Madrid katika fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, Juventus wamerejea nyumbani Italia.Pamoja na kuukosa ubingwa, mashabiki walionekana kuwapongeza wakiwapungia … Read More
Uwoya astushwa na habari za Ujauzito Sexy lady wa sinema za Kibongo, Irene Pancras Uwoya ‘Mama Krish’ amefungukia madai kuwa, kwa sasa ametengeneza urafiki wa muda na ndimu, samaki wabichi na ukwaju kwa kinachosemekana ni mjamzito.Huku akionesha kushtushwa na … Read More
VIDEO:Aliyetengeneza Audio Wema na Mbowe VIDEO:Aliyetengeneza Audio Wema na Mbowe Baada ya Audio Ambayo imewekwa kwenye mtandao wa Jamii Forums Ikisikika sauti zinazosemekana kuwa ni Wema Sepetu na Freeman Mbowe Wakiongea Kimahaba Wakipanga kukutana Kwa ajili ya… Read More
0 comments:
Post a Comment