Tuesday, 13 June 2017

Wakimbizi waugua kambini nchini Iraqi

Maelfu ya watu wameukimbia mji wa Mosul baada ya kutokea mapigano ya kudhibiti mji huoHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMaelfu ya watu wameukimbia mji wa Mosul baada ya kutokea mapigano ya kudhibiti mji huo
Mamia ya watu wameugua na mtoto mmoja amepoteza maisha kwa kile kinachoelezwa kutokana na kula chakula chenye vijidudu vyenye kusababisha magonjwa walipokuwa kwenye kambi karibu na mji wa Mosul.
Watu wamedaiwa kutapika na kuhara baada ya mlo wa futari baada ya mfungo wa Ramadhani.
Kambi ya Hasansham U2, kati ya mji wa Mosul na Irbil, huwapatia watu hifadhi wakitokea Iraq wakikimbia wapiganaji wa IS.
Wapiganaji wa IS wako mbioni kuzunguka magharibi mwa mji wa Mosul.
Shirika linalohudumia wakimbizi, UNHCR limesema kuwa visa takriban 800 vya maradhi vimerekodiwa huku watu wengine 200 wakipelekwa hospitali.
Kambi hiyo ni moja kati ya 13 zilizojengwa na UNHCR katika eneo la Mosul kwa ajili ya kuwatunza watu wanaokimbia kutoka mjini na maeneo ya vijiji.
Kambi hiyo inatunza watu 6235.
Vikosi vya Iraq, vikiungwa mkono na vikosi vinavyoongozwa na majeshi ya Marekani walianza Operesheni ya kuuchukua mji wa Mosul kutoka kwa wapiganaji wa IS mwezi Oktoba mwaka jana.

source:bbc






Related Posts:

  • Rais wa FIFA aipongeza Yanga Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Kimataifa (FIFA), Gianni Infantino, Mei 24, mwaka huu alituma ujumbe Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuipongeza Young Africans ya Dar es Salaam kwa kutwaa ubingwa Ligi Kuu… Read More
  • Huu ndio ugonjwa unaomsumbua mbunifu wa nembo ya Taifa RIPOTI ya awali ya uchunguzi wa kiafya aliofanyiwa mbunifu wa Nembo ya Taifa (bibi na bwana), Francis Ngosha (86) katika Kitengo cha Magonjwa ya Dharura Hospitali ya Mkoa ya Amana, inaonyesha kuwa anakabiliwa na tatizo la l… Read More
  • Yanga yapigwa faina ya milioni moja na TFF Kamati ya Saa 72 imekaa kupitia mambo mbalimbali na moja ya uamuzi wake ni kuhusiana na Yanga kugoma kuingia vyumbani.Mechi namba 206 (Yanga 1 Vs Toto Africans 0).Klabu ya Yanga imepigwa faini ya sh. 1,000,000 (milioni moja… Read More
  • Kenya: Afariki dunia baada ya kutabiri kifo chake  Irene Chris aliolewa kwa harusi Agosti 2016 na mumewe Chris Mwangi - Mnamo January 2017,Irene aliandika katika mtandao wa kijamii kwamba alikuwa akielekea mbinguni na kuwaomba watu kutuma salamu -Miezi minne baadaye… Read More
  • TAMBUA VYUO VINAVYOTAMBULIKA NA NACTENIMEAMUA KUKUWEKEA ORODHA YA VYUO VINAVYOTAMBULIKA NA NACTE ILI KUEPUKA KUTAPELIWA NA VYUO FEKI. BONYEZA HAPA>>>>>>>>.ORODHA YA VYUO VINAVYOTAMBULIKA NA NACTE… Read More

0 comments:

Post a Comment