Mwanajeshi mmoja wa Korea Kaskazini ametorokea Korea Kusini kupitia kuvuka mto Han kwa kuogelea ,ikiwa ni mara ya pili kwa raia wa taifa hilo kuhamia kwa majirani zao.
Mkuu wa Jeshi nchini Korea Kusini amesema kuwa mwanajeshi huyo aliogelea na kupitia eneo moja jembamba sana la maji ya mto huo yalio na kasi kubwa baada ya kuvalia boya lilolomsaidia kuelea.
Wiki iliopita mwanajeshi mwengine wa Korea Kaskazini alipitia mpaka unaolindwa sana unaogawanya mataifa hayo mawili.
Wanajeshi walikuwa wakihamia Korea Kusini katika kiwango cha mmoja kwa mwaka.
Mwanajeshi huyo aliyedaiwa kuwa na miaka ya ishirini alipatikana katika eneo la Gimpo, Magharibi mwa mji mkuu wa Korea Kusini Seoul, kulingana na chombo cha habari cha Yonhap.
Alipiga kelele akisema ''musiniue'', niko hapa kuhama ,kwa mwanajeshi wa Korea Kusini ambaye alikuwa amemuona, kilisema chombo cha habari cha Yonhap.
Mwanajeshi huyo sasa atahojiwa na maafisa wa kijeshi, Korea Kaskazini na Kusini ziko katika vita baradi tangu mzozo kati yao umalizike 1953 kupitia makubaliano.
Seoul inasema kuwa zaidi ya raia 30,000 wa Korea Kaskazini wamehamia kusini tangu kumalizika kwa vita vya Korea, wengi wao kupitia China ambayo ina mpaka mrefu na Korea Kaskazini.
Monday, 19 June 2017
Home »
» Mwanajeshi wa Korea Kaskazini ahamia K. Kusini kwa kuogelea
Mwanajeshi wa Korea Kaskazini ahamia K. Kusini kwa kuogelea
Related Posts:
Mataifa sita ya Kiarabu yavunja uhusiano wao na QatarHaki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionMji mkuu wa Qatar, Doha Mataifa sita ya Kiarabu, zikiwemo Saudi Arabia, Misri, Bahrain, Umoja wa Milki za Kiarabu na Yemen, yamekata uhusiano wao wa kidiplomasia na Qatar yakiilaum… Read More
Mataifa sita ya Kiarabu yavunja uhusiano wao na QatarHaki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionMji mkuu wa Qatar, Doha Mataifa sita ya Kiarabu, zikiwemo Saudi Arabia, Misri, Bahrain, Umoja wa Milki za Kiarabu na Yemen, yamekata uhusiano wao wa kidiplomasia na Qatar yakiilaum… Read More
PICHA: Jinsi Juventus walivyorejea kwao baada ya kipigo cha Real Madrid Baada ya kupoteza kwa kufungwa kwa mabao 4-1 dhidi ya Real Madrid katika fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, Juventus wamerejea nyumbani Italia.Pamoja na kuukosa ubingwa, mashabiki walionekana kuwapongeza wakiwapungia … Read More
Uwoya astushwa na habari za Ujauzito Sexy lady wa sinema za Kibongo, Irene Pancras Uwoya ‘Mama Krish’ amefungukia madai kuwa, kwa sasa ametengeneza urafiki wa muda na ndimu, samaki wabichi na ukwaju kwa kinachosemekana ni mjamzito.Huku akionesha kushtushwa na … Read More
Zitto njia panda uteuzi Anna Mghwira Kiongozi wa Chama Cha Act-Wazalendo hajajua cha kujibu kuhusu suala la uteuzi wa Mwenyekiti wa Chama hicho Anna Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro. Zitto amesema kuwa Chama hicho kitatoa tamko baada ya Mwen… Read More
0 comments:
Post a Comment