Wednesday, 7 June 2017

Ester Bulaya asema: Hamjatuziba midomo

Mbunge wa Bunda Mjini Mh. Ester Bulaya ametoa salamu kwa Wabunge wa CCM pamoja na Spika Job Ndugai kutambua kwamba hata baada ya kumuadhibu kutohudhuria vikao bya bunge siyo silaha ya kuwafunga midomo.

Bulaya amefunguka hayo akiwa Mkoani Kilimanjaro na kusema kwamba uamuzi uliofanya na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, Wabunge CCM pamoja na Spika wa bunge haujawatendea haki wananchi wao kwa sababu ni kwa muda mrefu watakosa wawakilishi bungeni ingawa siyo mwisho kwa wao kupigania haki na kuwatumikia wananchi kwa njia zingine.

"Wamekosea sana kwa sababu wananyima wananchi wetu haki ya kupata wawakilishi wa matatizo yao bungeni. Ingawa tayari tumekwishaweza kujipanga namna ya kwenda kuwatumikia na kupeleka maendeleo kwa katika kipindi hichi ambacho tutakuwa nje ya bunge. Lakini niweke wazi adhabu hii kutolewa siyo silaha ya kutuifanya kuacha kupigania demokrasia na haki. Bulaya alifunguka.

Aidha Bulaya ametupa lawama kwa Mh. Ndugai na kudai kuwa ni kiongozi asiyeweza kuzuia hasira ndio maana amekuwa na maamuzi ya kuhukumu haraka wakati yeye ni baba anayepaswa kuwa na subira na uvumilivu wa kuongoza.

Mbunge  Bunda Mjini, Mh. Esther Bulaya pamoja na Halima Mdeewa Kawe wamesimamishwa kuhudhuria vikao vyote vya Bunge vinavyoendelea mpaka mkutano ujao wa Bunge la Bajeti la mwaka  2018/19 kwa kile kinachodaiwa kuonyesha utomvu wa nidhamu ndani ya bunge.

source:muungwana

Related Posts:

  • Nchemba amtolea uvivu Tundu Lissu  Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba ‘amemvaa’ Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu kwamba amejaribu kutengeneza kila aina ya kichaka kukwamisha jitihada za Rais John Magufuli kupambana na usafirish… Read More
  • Simba yatumia Mil. 100/ kumshawishi Niyonzima NI UMAFIA TU! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya kiungo wa Yanga, Haruna Niyonzima kudaiwa kujiunga na Klabu ya Simba kwa mkataba wa miaka miwili baada ya kupewa ofa ya Sh. milioni 100. Habari zilizopatikana jana jioni … Read More
  • Ole Sendeka atuma salamu hizi kwa Lowassa Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Christopher Ole Sendeka amempongeza Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kwa kumpongeza Rais John Magufuli kufuatia uamuzi aliouchukua kuhusu mchanga wa madini yanayochimbwa nchini na kampuni ya Ac… Read More
  • Vigogo wawili Waliotajwa Ripoti ya Makinikia wamwaga fedha Kanisani WABUNGE watatu, wakiwamo Andrew Chenge na William Ngeleja ambao Kamati ya pili ya Rais kuchunguza masuala ya kisheria na kiuchumi kuhusiana na makinikia Jumatatu iliyopita ilishauri wachunguzwe, jana walitoa mchango kwa k… Read More
  • Watetezi watatu kulitetea Gazeti la Mawio BARAZA la Habari (MCT), Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC) na Umoja wa Vilabu vya Habari Tanzania (UTPC) vinakusudia kufungua kesi kwenye mahakama kupinga uamuzi wa serikali wa kulifunga gazeti la Mawio. Se… Read More

0 comments:

Post a Comment