Wednesday, 14 June 2017

HIKI HAPA: alichokisema John Bocco

Bocco (kulia) akikabidhiwa jezi ya Simba na rais wa klabu hiyo Evans Aveva, imeteka vichwa vya habari vya mitandao mbalimbali ambapo mashabiki wa Simba wameonyesha kufurahishwa na usajili huyo.

UONGOZI wa Simba, jana umetangaza rasmi kumsajili aliyekuwa mshambuliaji wa Azam, John Bocco baada ya tetesi za muda mrefu kuhusiana na suala hilo. Mara baada ya zoezi hilo, Bocco amefunguka kuwa atahakikisha anaendeleza moto wake wa kuzifumania nyavu kwa timu yoyote ile atakayokutana nayo kwenye michuano ya Ligi Kuu Bara ikiwemo Yanga.

Bocco amejiunga na Simba kwa mkataba wa miaka miwili akitokea Azam sambamba na aliyekuwa kipa wa timu hiyo, Aishi Manula na beki wa kulia, Shomari Kapombe ambao wote wamejiunga kwa mikataba ya miaka miwili.

Akizungumza na Championi Jumatano, Bocco alisema kuwa tangu ajiunge na Simba baada ya miaka 11 ndani ya Azam, kamwe hawezi kuwa adui kwa mashabiki wa timu hiyo kutokana na kuwafunga mara nyingi.

“Unajua kazi yangu kubwa ni kufunga, sasa sidhani kama ukiifunga timu fulani halafu ukajiunga nayo wanakuwa maadui zako. Ile ilikuwa natimiza majukumu ya kazi yangu wakati nipo Azam kama nilivyokuwa nazifunga timu zingine, hata sasa hivi nipo Simba nikikutana na timu yoyote nitaifunga tu kama Mungu akipenda.

“Nashukuru Mungu, uongozi na mashabiki wa Simba kwa jumla, kikubwa nimekuja kufanya kazi kwa sababu naamini watasajili wachezaji wengine wazuri, nguvu niliyokuwa nayo ambayo nitaiongeza kwa wenzangu tutaweza kufanya vizuri, naomba Mungu anisaidie maisha ya mafanikio zaidi kuliko nilipotoka,” alisema Bocco. Bocco anaungana na Aishi Manula, Shomary Kapombe, Yusuph Mlipili na Jamal Mwambeleko kuwa wachezaji wapya waliosajiliwa na klabu hiyo kwa ajili ya msimu ujao ambapo ukiondoa mashindano ya ndani, Simba itashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Related Posts:

  • Gavana asema al-Shabab huenda wakateka eneo la KenyaImage captionRamani ya Somalia Viongozi wa eneo la mashariki nchini Kenya wameonya kwamba maeneo ya taifa hilo huenda yakanyakuliwa na wapiganaji wa Al-Shabab. Gavana wa kaunti ya Wajir ambayo inapakana na taifa la Somalia a… Read More
  • Marekani kufanya majaribio ya kudungua komboraImage captionMfumo wa kudungua makombora wa Marekani uliopelekwa Korea Kusini Idara ya jeshi nchini Marekani kwa mara ya kwanza itajaribu kudungua kombora la masafa marefu lililo na uwezo wa kufyatuliwa kutoka bara moja hadi … Read More
  • Dwayne 'The Rock' Johnson kuwania urais Marekani mwaka 2020?Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionMwigizaji na mwanamiereka Dwayne 'The Rock' Johnson Dwayne 'The Rock' Johnson kuwania urais mwaka 2020? Dwayne 'The Rock' Johnson alitangaza kuwa atawania urais wa Marekani mwaka … Read More
  • Bomba la kupitisha pombe kujengwa UjerumaniHaki miliki ya pichaAFPImage captionPombe itakuwepo kwa wingi katika tamasha hilo Waandalizi wa Tamasha maarufu la muziki wa rock nchini Ujerumani wamewahakikishia wateja zaidi ya elfu 75 kwamba, katu! hawatokumbwa na kiu ya … Read More
  • Trump 'atengwa' na wenzake G7Image captionRais Trump ametengwa na wenzake kuhusiana na makubaliano ya tabia nchi yaliofakiwa mjini Paris Viongozi katika mkutano wa G7 wametofautiana kuhusu taarifa ya mabadiliko ya tabia nchi. Viongozi sita walikubaliana… Read More

0 comments:

Post a Comment