Monday, 5 June 2017

Mataifa sita ya Kiarabu yavunja uhusiano wao na Qatar

Mji mkuu wa Qatar, DohaHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMji mkuu wa Qatar, Doha
Mataifa sita ya Kiarabu, zikiwemo Saudi Arabia, Misri, Bahrain, Umoja wa Milki za Kiarabu na Yemen, yamekata uhusiano wao wa kidiplomasia na Qatar yakiilaumu kwa kuvuruga uthabiti katika eneo hilo.
Nchi hizo zimeilaumu Qatar kwa kuunga mkono makundi ya kigaidi, likiwemo kundi la Islamic State (IS).
Shirika moja nchini Saudi Arabia linasema kuwa taifa hilo limefunga mipaka yake na kusitisha usafiri wa ardhini, baharini na angani.
Lilinukuu maafisa wa Saudia wakisema kuwa hatua hiyo ni ya kulinda usalama wa nchi kutokana na hatari za ugaidi na itikadi kali.
Kile ambacho kwa wiki kadhaa kimekuwa kikichochea mzozo baina ya mataifa ya Ghuba sasa kimelipuka kuwa mzozo kamili wa kidiplomasia.
Katika tangazo la pamoja, Saudi Arabia ilikuwa ya kwanza kusema kuwa inavunja mahusiano yake ya Qatar mapema Jumatatu , mara moja ikafuatiwa na Bahrain, Muungano wa Milki za kiarabu Misri na Yemen.
Hatua za kwanza za mzozo huu zilionekana kujitokeza mwezi Mei wakati Qatar iliposema shirika lake rasmi la habari lilidukuliwa pamoja na kauli ambayo haikuwa sahihi iliyosemekana kutolewa na mtawala wake, iliyoonekana kwenye mtandao ikisifu kundi la wanawamgambo wa Iran na Lebanon la Hezbollah.

Taifa la Qatar

Mji Mkuu: Doha

  • 2.7 milioni Idadi ya watu
  • 11,437 sq km Ukubwa wa eneo
  • Kiarabu Lugha
  • Kiislamu Dini
  • 78.5 Umri wa watu kuishi
  • Riyal Sarafu
Getty Images
Misri nayo imefunga anga zake na bandari kwa Qatar, kwa mujibu wa wizara ya mashauri ya nchi kigeni.,
Milki ya nchi za kiarabu imewapa wanadiplomasia wa Qatar saa 48 kuondoka nchini humo.
Rais wa Marekani Donald Trump alikutana na Rais wa Misri Abdel Fattah al-Sisi (kushoto) na Mfalme Salman wa Saudi Arabia nchini Saudia wiki mbili zilizopitaHaki miliki ya pichaEPA
Image captionRais wa Marekani Donald Trump alikutana na Rais wa Misri Abdel Fattah al-Sisi (kushoto) na Mfalme Salman wa Saudi Arabia nchini Saudia wiki mbili zilizopita
Abu Dhabi inaishutumu Qatar kwa kufadhili ugaidi na itikadi kali.
Shirila la taifa la habari nchini Bahrain nalo limesema kuwa nchi hiyo inataka uhusiano na Qatar kwa kuvuruga usalama wake na kuingilia ndani masuala yake ya ndani.
Qatar na nchi nyingine za GhubaSOURCE:BBC

Related Posts:

  • Mauaji Pwani yamepangwa: Mbunge Dodoma. Mauaji katika wilaya za Kibiti na Rufiji jana yaliibuka bungeni kwa mara ya pili, wakati mbunge wa Rufiji (CCM), Mohamed Mchengerwa alipoeleza siri ya mipango na kiini chake.“Nataka niseme na Rais wangu ajue. Mambo … Read More
  • Kashfa nzito zaikumba Wizara ya maliasili BAADHI ya wabunge wamelalamikia vitendo vinavyofanywa na Wizara ya Maliasili na Utalii, kukamata na kupiga mnada mifugo inayoingia kwenye hifadhi za taifa. Kutokana na vitendo hivyo, watunga sheria hao wameishauri serik… Read More
  • Ujumbe wa Diamond Baada ya Ivan kufariki Dunia Kupitia ukurasa wake wa Instagram Diamond Platnumz ameandika ujumbe huu "Mbele yako, Nyuma yetu" Ujumbe huo ni baada ya Aliyekuwa mume wa Zarina Hassan ‘Zari The Bosslady’, Ivan Semwanga kufariki dunia akiwa hospitali nchi… Read More
  • Mbunifu wa Nembo ya Taifa ahamishiwa Hosptali ya Muhimbili Mzee Francis Ngosha ndiye mchoraji na mbunifu wa nembo ya taifa maarufu kama Bibi na Bwana, S iku mbili zilizopita aliliripotiwa kuwa anaishi maisha ya Magumu huko Buguruni jijini Dar es salaam. Kibanda alichokuwa akiishi… Read More
  • Wajumbe wa kamati Iliyomng'oa Muhongo walitishwa RAIS Dk. John Magufuli amebainisha kuwa licha ya kamati ya Kuchunguza Makontena ya Mchanga wenye Madini (makinikia) kupewa ulinzi mkali, kulikuwapo vitisho na hata baadhi ya wajumbe kutaka kuhongwa. Akizungumza jana wak… Read More

0 comments:

Post a Comment