Monday 5 June 2017

Zitto njia panda uteuzi Anna Mghwira

Kiongozi wa Chama Cha Act-Wazalendo hajajua cha kujibu kuhusu suala la uteuzi wa Mwenyekiti wa Chama hicho  Anna Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro.
 Zitto amesema kuwa Chama hicho kitatoa tamko baada ya Mwenyekiti huyo kurejea nchini kutoka nje ya nchi alipokwenda .

"Nimekuwa naulizwa Sana kuhusu uteuzi wa Mwenyekiti wa Chama chetu kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro. Nimekuwa kimya Kwa sababu tumepokea Taarifa za uteuzi kutoka katika vyombo vya Habari. Mwenyekiti yuko nje ya nchi na kutokana na tofauti za masaa bado hatujawasiliana nae

Aliyeteuliwa ni Mwenyekiti wa Chama Taifa, sio mshauri au mwanachama tu. Ni mmoja wa viongozi wa juu wa Chama chetu. Uteuzi wake unahitaji kikao cha Kamati Kuu ya Chama kukaa na kujadili. Nitaweza kutoa Taarifa baada ya vikao vya Kamati Kuu ya Chama. Kwa sasa umma usubiri vikao Kwa mujibu wa Katiba ya Chama chetu" amesema Zitto.

SOURCE:MUUNGWANA

0 comments:

Post a Comment