Wednesday, 7 June 2017

Gerard Pique awaponda tena Real Madrid.

Kama kuna kitu kinawakera mashabiki wa Real Madrid baasi ni mtu anayeitwa Gerard Pique, mlinzi huyu wa kati wa Barcelona amekuwa hawezi kuikalia kimya Real Madrid hata kama wamefungwa au wameshinda.

Baada ya Real Madrid kufanikiwa kutetea ubingwa wa champions league wiki iliyopita walipongezwa na kila mtu ikiwemo klabu ya Barcelona ambao ndio waajiri wa beki huyo, kupitia Twitter Barca waliwapongeza Real Madrid.

Lakini kama ulidhani Barcelona kuipongeza Madrid ni Barcelona wote baasi umekosea sana kwani kwa Pique ni tofauti sana na anaona hakuna kitu na walichofanya Madrid hakiwafanyi kuwa bora kuliko wao.

Akiongea na kituo kimoja cha habari nchini Hisapania Pique amesema Real Madrid hawawezi kuigusa Barcelona hata kidogo “huwezi kufananisha walichoshinda katika miaka ya hivi karibuni na kile ambacho sisi tumeshinda”

Pique amewachana Real Madrid kwa kufanya bus parade akisema Real Madrid ni kawaida yao kusumbua watu na parade hizo wanapobebe ubingwa, akikumbushia mwaka 2011 ambapo Real Madrid walifanya bus parade walipobeba kombe la Copa del Rey.

Pique anaona hicho ndio kinawatofautisha wao na Real na ndio maana wao Barcelona wamebeba Copa Del Rey lakini hawakuona sababu ya kufanya “bus parade” kwani hawakutaka kuwasumbua watu na kombe dogo kama hilo lakini Real wangefanya hivyo.

Hii sio mara ya kwanza kwa Pique kuishambulia Real Madrid kwani kama unakumbuka hata katika mchezo kati ya Real Madrid na Bayern Munich Pique aliiponda Real Madrid kwa kuwaambia wanabebwa sana na waamuzi.

SOURCE:MUUNGWANA

Related Posts:

  • Ronaldo ameithibitishia dunia Ubabe wake!!! Cristiano Ronaldo ameithibitishia dunia yeye ni mchezaji wa aina yake baada ya kuweka rekodi ya kuwa mfungaji Bora wa Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa misimu mitano mfululizo. Ronaldo amefunga mabao mawili wakati Real Madrid … Read More
  • Msanii mpya wa WCB ampigia saluti Alikiba Msanii mpya kutoka WCB, Lava Lava, amefunguka mambo mengi kuhusu muziki wake pamoja na kueleza jinsi anavyomkubali muimbaji Alikiba ambaye ni mpinzani mkubwa wa bosi wake, Diamond Platnumz. Muimbaji huyo ambaye anafanya vi… Read More
  • Giggy Aumbuka! 'amefanya' alichojiapiza hatofanya tena IKIWA imepita miezi michache tangu ajiapize kuwa hatakuja kujichora tattoo ya mwanaume yeyote atakayekuwa naye katika uhusiano, muuza sura kwenye video mbalimbali za wasanii wa Bongo Fleva, Gift Stanford ‘Gigy Money’ ame… Read More
  • Islamic State yakiri kufanya shambulio Londona Kikosi maalumu cha kupambana na ugaidi London Polisi nchini Uingereza wamekuwa wakifanya msako kwenye makazi manne mjini London hadi usiku wa manane kama sehemu ya uchunguzi juu ya shambulio la Jumamosi ambapo watu saba … Read More
  • Yanga yaminyana na Mdhamini wake YANGA juzi ilipiga hodi kwa wadhamni wao Kampuni ya SportPesa kuomba watanguliziwe Sh milioni 400 kwa ajili ya mishahara ya wachezaji wake. Timu hiyo, inadaiwa mishahara ya miezi mitatu na wachezaji wake walioiwezesha kuch… Read More

0 comments:

Post a Comment