Kama kuna kitu kinawakera mashabiki wa Real Madrid baasi ni mtu anayeitwa Gerard Pique, mlinzi huyu wa kati wa Barcelona amekuwa hawezi kuikalia kimya Real Madrid hata kama wamefungwa au wameshinda.
Baada ya Real Madrid kufanikiwa kutetea ubingwa wa champions league wiki iliyopita walipongezwa na kila mtu ikiwemo klabu ya Barcelona ambao ndio waajiri wa beki huyo, kupitia Twitter Barca waliwapongeza Real Madrid.
Lakini kama ulidhani Barcelona kuipongeza Madrid ni Barcelona wote baasi umekosea sana kwani kwa Pique ni tofauti sana na anaona hakuna kitu na walichofanya Madrid hakiwafanyi kuwa bora kuliko wao.
Akiongea na kituo kimoja cha habari nchini Hisapania Pique amesema Real Madrid hawawezi kuigusa Barcelona hata kidogo “huwezi kufananisha walichoshinda katika miaka ya hivi karibuni na kile ambacho sisi tumeshinda”
Pique amewachana Real Madrid kwa kufanya bus parade akisema Real Madrid ni kawaida yao kusumbua watu na parade hizo wanapobebe ubingwa, akikumbushia mwaka 2011 ambapo Real Madrid walifanya bus parade walipobeba kombe la Copa del Rey.
Pique anaona hicho ndio kinawatofautisha wao na Real na ndio maana wao Barcelona wamebeba Copa Del Rey lakini hawakuona sababu ya kufanya “bus parade” kwani hawakutaka kuwasumbua watu na kombe dogo kama hilo lakini Real wangefanya hivyo.
Hii sio mara ya kwanza kwa Pique kuishambulia Real Madrid kwani kama unakumbuka hata katika mchezo kati ya Real Madrid na Bayern Munich Pique aliiponda Real Madrid kwa kuwaambia wanabebwa sana na waamuzi.
SOURCE:MUUNGWANA
Wednesday, 7 June 2017
Home »
» Gerard Pique awaponda tena Real Madrid.
Gerard Pique awaponda tena Real Madrid.
Related Posts:
Mnyika kula sahani moja na askari wa Bunge aliyemsukuma Mbunge wa Kibamba (Chadema), John Mnyika amesema atachukua hatua kwa kitendo cha kusukumwa kilichofanywa na askari wa Bunge mwishoni mwa wiki. Alisema atafanya hivyo mara baada ya kumaliza msiba wa mmoja wa waasisi wa c… Read More
Uwoya astushwa na habari za Ujauzito Sexy lady wa sinema za Kibongo, Irene Pancras Uwoya ‘Mama Krish’ amefungukia madai kuwa, kwa sasa ametengeneza urafiki wa muda na ndimu, samaki wabichi na ukwaju kwa kinachosemekana ni mjamzito.Huku akionesha kushtushwa na … Read More
PICHA: Jinsi Juventus walivyorejea kwao baada ya kipigo cha Real Madrid Baada ya kupoteza kwa kufungwa kwa mabao 4-1 dhidi ya Real Madrid katika fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, Juventus wamerejea nyumbani Italia.Pamoja na kuukosa ubingwa, mashabiki walionekana kuwapongeza wakiwapungia … Read More
Jeneza la mwili wa Ndesamburo lazuiwa kupitishwa barabarani Moshi. Jeshi la Polisi mkoa wa Kipolisi wa Moshi limezuia utaratibu wa kutoa heshima za mwisho kwa kuutembeza katika barabara za viunga vya manispaa hiyo, mwili aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema, Kilimanjaro… Read More
VIDEO:Aliyetengeneza Audio Wema na Mbowe VIDEO:Aliyetengeneza Audio Wema na Mbowe Baada ya Audio Ambayo imewekwa kwenye mtandao wa Jamii Forums Ikisikika sauti zinazosemekana kuwa ni Wema Sepetu na Freeman Mbowe Wakiongea Kimahaba Wakipanga kukutana Kwa ajili ya… Read More
0 comments:
Post a Comment