Wednesday, 7 June 2017

Wapelekwa kortini kwa tuhuma za kuiba kanisani

WAKAZI wa wawili wa Ubungo Riverside, Dar es Salaam, Ayubu Sanga (21) na Nafaife Kayinga (19) wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Mwanzo Kinondoni kwa tuhuma za kuiba vitu vyenye thamani Sh 1,025,000 katika Kanisa la T.A.G Kinondoni.

Akisoma mashitaka hayo mbele ya Hakimu Ester Kihiyo msoma Mashitaka Dorah Chambo, alidai kwamba washitakiwa wote kwa pamoja walitenda kosa hilo mnamo Aprili 16, 2017 majira ya saa saba mchana maeneo ya Kanisa la T.A.G Kinondoni Biafra.

Alidai washitakiwa waliiba mkoba uliokuwa na fedha taslimu Sh 160,000, simu tatu aina Samsung J7, Techno Jpad, Huawei na vitambulisho mbalimbali ikiwemo leseni ya udereva vyote vikiwa na thamani ya Sh 1,025,000 mali ya Doris Mackenzie.

Washitakiwa wote walikana mashitaka hayo na kurudishwa rumande, baada ya kushindwa kutimiza mashariti ya dhamana walipohitajika kila mmoja kuwa na wadhamini wawili, watakaoahidi dhamana ya Sh milioni 2. Kesi hiyo itatajwa tena Juni 13 mwaka huu.

Related Posts:

  • VIDEO:Aliyetengeneza Audio Wema na Mbowe VIDEO:Aliyetengeneza Audio Wema na Mbowe Baada ya Audio Ambayo imewekwa kwenye mtandao wa Jamii Forums Ikisikika sauti zinazosemekana kuwa ni Wema Sepetu na Freeman Mbowe Wakiongea Kimahaba Wakipanga kukutana Kwa ajili ya… Read More
  • Uwoya astushwa na habari za Ujauzito Sexy lady wa sinema za Kibongo, Irene Pancras Uwoya ‘Mama Krish’ amefungukia madai kuwa, kwa sasa ametengeneza urafiki wa muda na ndimu, samaki wabichi na ukwaju kwa kinachosemekana ni mjamzito.Huku akionesha kushtushwa na … Read More
  • Mataifa sita ya Kiarabu yavunja uhusiano wao na QatarHaki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionMji mkuu wa Qatar, Doha Mataifa sita ya Kiarabu, zikiwemo Saudi Arabia, Misri, Bahrain, Umoja wa Milki za Kiarabu na Yemen, yamekata uhusiano wao wa kidiplomasia na Qatar yakiilaum… Read More
  • Zitto njia panda uteuzi Anna Mghwira Kiongozi wa Chama Cha Act-Wazalendo hajajua cha kujibu kuhusu suala la uteuzi wa Mwenyekiti wa Chama hicho  Anna Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro. Zitto amesema kuwa Chama hicho kitatoa tamko baada ya Mwen… Read More
  • PICHA: Jinsi Juventus walivyorejea kwao baada ya kipigo cha Real Madrid  Baada ya kupoteza kwa kufungwa kwa mabao 4-1 dhidi ya Real Madrid katika fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, Juventus wamerejea nyumbani Italia.Pamoja na kuukosa ubingwa, mashabiki walionekana kuwapongeza wakiwapungia … Read More

0 comments:

Post a Comment