Jeshi la polisi mkoani Shinyinga limelazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya madereva Bobaboda ambao walikuwa wakiaandamana kuonyesha kupinga kitendo cha polisi baada ya dereva bodaboda mmoja kufariki wakisema kifo chake kimesababishwa polisi.
Kwa mujibu wa mashuhuda wanasema tukio hili limetokea leo majira ya saa moja asubuhi hadi saa sita mchana ambapo askari polisi walikuwa wakipimana nguvu na bodaboda hao kwa kutupiana mawe na mabomu, hali ambayo ilipelekea kusitisha shughuli za kijamii mjini hapo.
Akizungumzia tukio hilo Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Shinyanga Jumanne Murilo, alisema wameamua kuzuia maandamano hayo kwa sababu yana hatarisha hali ya usalama na maandamano hayo siyo halali, ambapo hawakupaswa kufanya hivyo, bali walitakiwa kutii sheria bila shuruti, na kufuata taratibu za kudai kuonewa, na siyo kutishia kuharibu amani.
"Tumeamua kufanya hivi ili kuzuia kitendo cha watu wachache ambao wametaka kuvuruga amani, kwa kuwapiga mabomu na maji ya kuwasha, ili kuhakikisha utulivu unatawala," alisema Murilo
Hata hivyo jeshi hilo halikuishia hapo , bali lilikwenda hadi nyumbani kwenye msiba alipokuwa akiishi marehemu, na kuutawanya kwa kuwa kamata bodaboda na pikipiki zao hali iliyozua taharuki zaidi.
Wednesday, 7 June 2017
Home »
» MAANDAMANO:Bobaboda watawanywa kwa mabomu ya machozi
MAANDAMANO:Bobaboda watawanywa kwa mabomu ya machozi
Related Posts:
Pogba kutua Tanzania Klabu ya Everton inajiandaa kuja nchini Tanzania kwa ziara ya kujiandaa na msimu ujao wa ligi ambapo wakiwa hapa wtacheza na washindi wa kombe la Sports Pesa timu ya Gor Mahia kutoka nchini Kenya. Sasa Everton wanaweza … Read More
Hawa wote motoni KIMENUKA! RAIS John Magufuli ameagiza kukamatwa na kuhojiwa kwa waliokuwa mawaziri, kamishina wa madini, wanasheria wakuu (AG) na waliokuwa watumishi katika idara mbalimbali za serikali zilizoruhusu usafirishaji wa madini … Read More
Serikali imezuia Passport za Chenge, Muhongo, Kafumu, Karamagi Serikali imeagiza, Mawaziri, Wanasheria Wakuu wa Serikali na Manaibu wao, Wakurugenzi wa idara za mikataba, na Makamishna wa madini, wanasheria wa Wizara ya Nishati na Madini na watumishi wengine wa Serikali na watu wote wa… Read More
Wananchi watema cheche, wataka Marais wastaafu wachunguzwe Mikoani. Wananchi katika maeneo mbalimbali nchini wamemshauri Rais John Magufuli kufanya mabadiliko ya Katiba na kuhakikisha diplomasia ya uchumi haivurugiki kutokana na sakata la mchanga wa madini (makinikia).Wakitoa maoni… Read More
Diamond afunguka mchango wa Wema Sepetu kwenye ‘Chibu Perfume’. Msanii wa muziki, Diamond platnumz amefunguka kuuzungumzia mchango wa malkia wa filamu, Wema Sepetu kwenye perfume yake ya ‘Chibu Perfume’.Diamond amekiambia kipindi cha XXL cha Clouds FM kuwa, yeye na Wema wanakutana na ku… Read More
0 comments:
Post a Comment