Tuesday, 23 May 2017

Madhara ya Mvua ya siku sita yaua 10, yabomoa nyumba 44

Tanga. Tathmini ya madhara yaliyotokana na na mvua zilizonyesha kwa siku sita mfululizo wiki iliyopita mkoani hapa zimeonyesha kuwa hadi sasa watu 10 wamekufa huku  nyumba 44 zikibomoka na nyingine 218 zikizingirwa na maji.

Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Tanga, Benedict Wakulyamba ametoa  taarifa

ya tahmini hiyo leo, Jumanne wakati akizumgumza na waandishi wa habari jijini hapa.

Wakulyamba amesema katika yaliyotokena na mvua hizo, watu 10 walimepoteza maisha baada ya kusombwa na mafuriko, kuangukiwa nyumba na kutumbukia kwenye mashimo  ambapo  saba kati yao  walikuwa wakazi wa Wilaya ya Korogwe, wawili Muheza na mwingine ni mkazi wa Jiji la Tanga huku 20  wakijeruhiwa.

Kwa mujibu wa kamanda huyo, nyumba 44  ziliezuliwa paa, 218 zilizingirwa na maji, 12 zikisombwa na mafuriko.

Amesema wilaya zilizoathirika zaidi ni Korogwe,Tanga na Lushoto huku Pangani,Mkinga

na Handeni zikipata athari  ndogo.

Kamanda huyo alisema katika mafuriko hayo,barabara zilizopo katika za Wilaya mbalimbali mkoani Tanga,zimeathirika kwa kubomoka,kuvunjika makaravati pamaoja na madaraja.

"Kama mnavyoona mvua bado zinaendelea, nawatahadharisha wanaokaa kwenye nyumba zilizopo mabondeni wasisubiri maji yaingie ili waokolewe, kuna wakati mwingine uokoaji unaweza kutofanikiwa na kujikuta mnaangamia,"amesema Wakulyamba.

source:mtanzania

Related Posts:

  • Watetezi watatu kulitetea Gazeti la Mawio BARAZA la Habari (MCT), Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC) na Umoja wa Vilabu vya Habari Tanzania (UTPC) vinakusudia kufungua kesi kwenye mahakama kupinga uamuzi wa serikali wa kulifunga gazeti la Mawio. Se… Read More
  • Vigogo wawili Waliotajwa Ripoti ya Makinikia wamwaga fedha Kanisani WABUNGE watatu, wakiwamo Andrew Chenge na William Ngeleja ambao Kamati ya pili ya Rais kuchunguza masuala ya kisheria na kiuchumi kuhusiana na makinikia Jumatatu iliyopita ilishauri wachunguzwe, jana walitoa mchango kwa k… Read More
  • Nchemba amtolea uvivu Tundu Lissu  Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba ‘amemvaa’ Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu kwamba amejaribu kutengeneza kila aina ya kichaka kukwamisha jitihada za Rais John Magufuli kupambana na usafirish… Read More
  • Simba yatumia Mil. 100/ kumshawishi Niyonzima NI UMAFIA TU! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya kiungo wa Yanga, Haruna Niyonzima kudaiwa kujiunga na Klabu ya Simba kwa mkataba wa miaka miwili baada ya kupewa ofa ya Sh. milioni 100. Habari zilizopatikana jana jioni … Read More
  • Ole Sendeka atuma salamu hizi kwa Lowassa Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Christopher Ole Sendeka amempongeza Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kwa kumpongeza Rais John Magufuli kufuatia uamuzi aliouchukua kuhusu mchanga wa madini yanayochimbwa nchini na kampuni ya Ac… Read More

0 comments:

Post a Comment