Korea Kusini inasema kuwa imekishambulia ''kifaa'' kutoka Korea Kaskazini kilichorushwa katika eneo lisilo la kijeshi.
Takriban risasi 90 zilifyatuliwa zikielekezwa kwa kifaa hicho ambacho kufikia sasa hakijajulikana kilikuwa nini hasa.
Korea Kaskazini imerusha ndege zisizokuwa na rubani katika mpaka huo siku za hapo awali.
Katika taarifa, jeshi la Korea Kusini limesema kuwa jeshi lake linaweka ulinzi mkali.
Kisa hicho kinajiri wakati ambapo kuna wasiwasi mkubwa katika rasi ya Korea.
Siku ya Jumapili Pyongyang ilitekeleza kile ilichodai kuwa jaribio lililofanikiwa la kombora la masafa ya kadri.
Jaribio hilo linajiri wiki moja baada ya Korea Kaskazini kufanyia majaribio kile ilichodai kuwa ni kombora jipya linaloweza kubeba kichwa cha nyuklia, ambalo lina uwezo wa kushambulia Marekani.
Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa linatarajiwa kufanya kikao cha faragha kuhusu Korea Kaskzini siku ya Jumanne jioni.
Katika taarifa siku ya Jumatatu ,lilikubali kuchukua hatua muhimu ikiwemo vikwazo ili kuishinikiza Korea Kaskazni kusitisha hatua yake .
Ongezeko hilo la wasiwasi linajiri wakati ambapo kuna rais mpya Korea Kusini .
Moon Jae alikula kiapo cha kuchukua mamlaka mapema mwezi huu baada ya mtangulizi wake Park Geun Hye kushtakiwa.
Kwa sasa anakabiliwa na mashtaka ya ufisadi.
Bwana Moon anapendelea majadiliano na Korea Kaskazini ikilinganishwa na mtangulizi wake.
Maafisa wa Korea Kusini hawakusema iwapo walikishambulia ama kukikamata kitu hicho kilichorushwa katika eneo hilo ambalo ni marufuku kwa shughuli zozote za kijeshi lakini visa kama hivyo vimetokea hapo awali.
Mnamo mwezi Januari 2016 wanajeshi waliopo mpakani mwa Korea Kusini waliishambulia ndege moja isiokuwa na rubani.
Mnamo 2014, maafisa wa Korea Kusini walisema kuwa walipata ndege mbili zisizokuwa na rubani katika eneo ambalo ni marufuku kwa shughuli za kijeshi karibu na Paju na nyengine katika kisiwa karibu na eneo linalozozaniwa la baharini kati ya mataifa hayo ya Korea.
Tuesday, 23 May 2017
Home »
» Korea Kusini yashambulia kifaa cha Korea Kaskazini
Korea Kusini yashambulia kifaa cha Korea Kaskazini
Related Posts:
Dereva Bodaboda afariki dunia huku akiwa amembeba Askari
Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga leo limewatawanya madereva bodaboda zaidi ya 100 waliokuwa wanaandamana kuelekea eneo la Ibinzamata kwenye msibani kwa dereva mwenzao Joel Mamla (26) ambaye alifariki dunia jana akiwa amempa… Read More
MAANDAMANO:Bobaboda watawanywa kwa mabomu ya machozi
Jeshi la polisi mkoani Shinyinga limelazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya madereva Bobaboda ambao walikuwa wakiaandamana kuonyesha kupinga kitendo cha polisi baada ya dereva bodaboda mmoja kufariki wakisema kifo c… Read More
Gerard Pique awaponda tena Real Madrid.
Kama kuna kitu kinawakera mashabiki wa Real Madrid baasi ni mtu anayeitwa Gerard Pique, mlinzi huyu wa kati wa Barcelona amekuwa hawezi kuikalia kimya Real Madrid hata kama wamefungwa au wameshinda.Baada ya Real Madrid kufa… Read More
Breaking: ACT-Wazakendo watoa Maamuzi kuhusu Anna Mghwira
Haya ndio maamuzi waliotoa ACT- wazalendo kuhusu Anna Mghwira
SOURCE:MUUNGWANA
… Read More
Wapelekwa kortini kwa tuhuma za kuiba kanisani
WAKAZI wa wawili wa Ubungo Riverside, Dar es Salaam, Ayubu Sanga (21) na Nafaife Kayinga (19) wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Mwanzo Kinondoni kwa tuhuma za kuiba vitu vyenye thamani Sh 1,025,000 katika Kanisa la… Read More







0 comments:
Post a Comment